AFCON 2025 Kuwa na Zawadi Kubwa Zaidi Katika Historia
Shirikisho la Soka barani Afrika, CAF, limezindua rasmi mfumo mpya wa zawadi kwa ajili ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON elfu mbili ishirini na tano, zitakazoandaliwa nchini Morocco. Kwa mujibu wa CAF, michuano hiyo itashirikisha mataifa ishirini na manne, huku jumla ya zawadi ya kifedha ikifikia shilingi bilioni 4. Timu itakayonyakua ubingwa wa mashindano hayo itajishindia shilingi bilioni 0.9, sawa huku timu itakayomaliza katika nafasi ya pili ikipata shilingi milioni 0.5. CAF imeeleza kuwa timu zitakazofuzu hatua ya nusu fainali zitapokea shilingi milioni 322 kila mmoja. Hatua hii inalenga kuongeza motisha kwa timu shiriki pamoja na kuimarisha ushindani katika mashindano hayo. Shirikisho hilo limesisitiza kuwa kuongezwa kwa viwango vya zawadi kutahakikisha mataifa yote ishirini na manne yanayoshiriki yanapata tuzo za kifedha, ikiwa ni sehemu ya dhamira ya CAF ya kusaidia maendeleo ya soka barani Afrika. Kwa ongezeko hilo la zawadi, AFCON elfu mbili ishirini na tano inatajwa kuwa mashindano yenye zawadi kubwa zaidi katika historia ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika.
Read More