TYGA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LA KUMPIGA EX WAKE

TYGA AFUNGUKA KWA MARA YA KWANZA KUHUSU SAKATA LA KUMPIGA EX WAKE

Rapa kutoka nchini Marekani Tyga amefunguka kuhusu taarifa za kufunguliwa mashtaka kwa madai ya kumpiga ex wake Camaryn Swanson, Jumatatu wiki iliyopita. Tyga alijisalimisha kwenye mikono ya polisi mjini Los Angeles Jumanne  wiki iliyopita ambapo Tovuti ya TMZ ilidai kwamba tayari amefunguliwa mashtaka ya unyanyasaji wa nyumbani. Sasa baada ya kimya cha muda mfupi, Tyga ameamua kuweka wazi sakata hilo. Kupitia ukurasa wake wa instagram rapa huyo amekanusha kwa kusema madai hayo hayana ukweli wowote, kwani hakukamatwa na polisi na wala hakufunguliwa mashtaka yoyote bali alifika kituo hapo kujieleza. Kwa mujibu wa nyaraka za polisi wa Los Angeles, zinaonesha Michael Stevenson maarufu Tyga alishtakiwa kwa makosa ya uhalifu mnamo Oktoba 12 mwaka huu na aliachiwa masaa machache baadaye kwa dhamana ya shillingi millioni 5.5 za kenya.

Read More
 TYGA AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUMPIGA EX GIRLFRIEND WAKE

TYGA AFUNGULIWA MASHTAKA KWA KUMPIGA EX GIRLFRIEND WAKE

Staa wa muziki kutoka marekani Tyga amefunguliwa mashtaka kwa kumpiga mpenzi wake wa zamani Camaryn Swanson. Kwa mujibu wa tovuti ya TMZ, mrembo huyo alifika nyumbani kwa Tyga mishale ya saa 9 usiku Jumatatu wiki ambapo awali aliambiwa asifike nyumbani hapo. Taarifa zinaeleza kwamba Camaryn alikuwa amelewa, lakini Tyga alimruhusu aingie ndani kwa ajili ya kuzungumza naye. Baadaye zilianza kusikika kelele za Camaryn ambaye ameiambia polisi kwamba Tyga alikuwa akimrushia ngumi wakati wa majibizano yao. Mama yake mzazi alifika na kumchukua kisha kuwapigia simu polisi kutoa taarifa. Polisi walifika nyumbani kwa Tyga siku hiyo hiyo kwa ajili ya uchunguzi na Tyga ameripotiwa kuandikisha kutoa maelezo kwa upande wake ikiwa tayari amefunguliwa kesi ya unyanyasaji wa nyumbani. Camaryn ame-share picha zake za majeraha baada ya tukio hilo.

Read More