Catherine Kusasira Atishia Kujiondoa NRM Kufuatia Kudharauliwa na Viongozi wa Chama

Catherine Kusasira Atishia Kujiondoa NRM Kufuatia Kudharauliwa na Viongozi wa Chama

Msanii na mshauri wa Rais wa Uganda kuhusu masuala ya Kampala na wakazi wa Ghetto, Catherine Kusasira, ametishia kujiondoa ndani ya chama tawala cha NRM, akilalamikia kile alichokiita dharau na kutotambuliwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho. Kusasira amesema licha ya kujitolea kwa miaka karibu kumi kutetea chama na Rais Yoweri Kaguta Museveni, bado anakumbana na vikwazo na kudharauliwa, hasa na maafisa wa usalama na baadhi ya viongozi waandamizi wa NRM. “Nimechoka na dharau kutoka kwa baadhi ya watu ndani ya NRM. Mnathubutu kunizuia kukutana na Jenerali Nalweyiso? Nimejitolea kwa ajili ya chama, lakini ni Rais pekee anayetambua juhudi zangu. Wakati mwingine nawaza kuacha siasa kabisa,” alisema Kusasira. Msanii huyo ambaye hapo awali alitangaza nia ya kugombea kiti cha Mwakilishi wa Wanawake wa Buikwe, anaonekana kupoa kisiasa na sasa anaelekeza nguvu zake katika kukuza chama kwa njia ya ushawishi na kampeni za kijamii. Kwa sasa, Kusasira anasisitiza kuwa mchango wake unapaswa kutambuliwa na kuheshimiwa na viongozi wote wa chama, sio Rais peke yake. Kauli yake imezua mijadala mikali ndani ya chama, huku wachambuzi wa siasa wakitathmini athari za manung’uniko yake kwa taswira ya NRM miongoni mwa wasanii na vijana

Read More
 Catherine Kusasira awaasa wasanii wa kike Uganda kujitengana na matumizi ya vipodozi

Catherine Kusasira awaasa wasanii wa kike Uganda kujitengana na matumizi ya vipodozi

Mwimbaji wa bendi  Catherine Kusasira amewapa somo wasanii wa kike nchini Uganda kujiepusha na matumizi ya vipodozi kwenye miili yao. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Kusasiri anasema vipodozi ina kemikali hatari ambayo inazeesha ngozi haraka. Hitmaker huyo wa “I Love You” anadai kuwa hatumii vipodozi usoni mwake mbali na mafuta aina ya Vaseline. “Situmii vipodozi na ninawashauri waimbaji chipukizi kujiepusha kutumia kemikali kama hizo kwenye nyuso zao. Situmii vipodozi na ndio maana naonekana mdogo kila mara unaponiona,” alisema katika mahojiano na runinga moja nchini Uganda. Kusasira amesema alipata msukumo wa kuzingatia urembo wa asili kutoka kwa wasanii wakongwe nchini humo Mariam Ndagire na Neema Nalubega.

Read More
 Kalifah Aganaga akerwa na kitendo cha Catharine Kusasira kujidhalalisha mbele ya umma

Kalifah Aganaga akerwa na kitendo cha Catharine Kusasira kujidhalalisha mbele ya umma

Mwanamuziki wa dancehall kutoka nchini Uganda Kalifah Aganaga amesikitishwa na kitendo cha Catherine Kusasira kuangua kilio hadharani kwenye mahojiano yake hivi karibuni kutokana na ugumu wa maisha. Kwenye mahojiano na Spark TV, Aganaga amesema ni aibu kwa mwanamuziki huyo mkongwe kujidhalalisha mbele ya umma kama mtoto ikizingatiwa kuwa alitumia vibaya mshahara aliokuwa analipwa na serikali kipindi anahudumu kama mshauri wa rais Yoweri Museveni. Kauli ya aganaga inakuja mara baada ya catherine kusasira kunukuliwa akieleza masaibu kuwa tangu atemwe kama mshairi wa rais mwaka wa 2021 amekuwa akipitia kipindi kigumu kiuchumi kiasi cha madalali kupiga mnada mjengo wake wa kifahari na gari yake aina Land cruiser V8 kwa ajili ya kukamilisha madeni anayodaiwa.

Read More
 Catherine Kusasira akanusha kuwadharau mashabiki kwa vibunda vya pesa

Catherine Kusasira akanusha kuwadharau mashabiki kwa vibunda vya pesa

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Uganda Catherine Kusasira amekanusha madai ya kuwadharau watu mitandaoni baada ya kuonekana akijigamba na vibandu vya pesa. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni Kusasira amedai kitendo chake cha kuwaonesha mashabiki  kibunda cha pesa mtandaoni ilikuwa ni njia ya kutengeneza mazingira ya tamasha lake la muziki kuzungumziwa mtandaoni na sio vinginevyo. Mrembo huyo amesema pesa hizo alikopeshwa na promota Baalam kwa ajili ya kufadhili tamasha lake la muziki, hivyo hakuwa na nia ya kuwavunjia heshima mashabiki. Kauli yake imekuja mara baada ya mashabiki kumshambulia mtandaoni alipokiri kuwa nyumba yake inapigwa mnada hivi karibuni kutokana na madeni anayodaiwa na benki.

Read More
 CATHERINE KUSASIRA ARUDI SHULENI, AJUTA KUTOKAMILISHA MASOMO YAKE

CATHERINE KUSASIRA ARUDI SHULENI, AJUTA KUTOKAMILISHA MASOMO YAKE

Msanii Catherine Kusasira bado anajutia hatua ya kutokamilisha masomo yake baada ya kudai kuwa amekosa kazi serikalini kutokana na ukosefu wa elimu ya kutosha. Katika mahojiano yake hivi karibuni Kusasira amesema angekuwa waziri katika serikali ya rais Yoweri Museveni kama angekuwa amemaliza masomo yake Hitmaker huyo wa “I love you” amesema anaumizwa na kitendo cha serikali kutompa kazi kutokana na yeye kukosa elimu licha ya kuwa na ukaribu na maafisa wakuu serikalini “It hurts me that I didn’t finish school early enough. I would be a minister or even the prime minister but I am limited by my academic qualifications. That’s why I went back to school,” Alisema. Catherine kusasira ambaye ni mshauri wa masuala ya ndani ya jiji la kampala kwa sasa amejiunga na chuo kikuu cha  Nkumba kuendeleza masomo yake.

Read More
 CATHARINE KUSASIRA ATAKA SERIKALI YA UGANDA KUMRUHUSU BOBI WINE KUTUMBUIZA

CATHARINE KUSASIRA ATAKA SERIKALI YA UGANDA KUMRUHUSU BOBI WINE KUTUMBUIZA

Mwanamuziki kutoka Uganda Catherine Kusasira ametoa wito kwa serikali ya nchini hiyo kumruhusu Bobi Wine kutumbuiza kwenye majukwaa ya muziki. Katika mahojiano yake hivi karibuni kusasira amesema ni wakati muafaka kwa bobi wine kurudi kwenye muziki kwa kuwa siasa zilikamilika kwani ndiyo chanzo kuu iliyomfanya azuiwe kutumbuiza kwenye majukwaa ya burudani. Aidha amesema kuwa Bobi Wine alizuiwa kutumbuiza kwa sababu alichanganyika muziki na siasa, jambo ambalo lilizua mvutano katika yake na serikali.  “Siasa ziliisha na Bobi Wine hana budi kuanza tena kazi yake ya muziki. Naamini sababu iliyomfanya kufungiwa kuimba ni siasa kwani alitumia muziki kutangaza ajenda zake za siasa. Kusasira ametoa kauli hiyo kufuatia mapokezi mabaya ambayo amekuwa akiyapata kwenye shoo zake ambazo alipangiwa kutumbuiza. Utakumbuka ni takriban miaka minne sasa tangu Bobi Wine apigwe marufuku kutumbuiza kwenye maeneo ya umma baada ya kutangaza  nia ya kuchuana na Rais Museveni kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2021.

Read More
 CATHERINE KUSASIRA AFUNGUKA KUFUNGIWA SHOWS NA MAPROMOTA KISA MSIMAMO WAKE WA KISIASA

CATHERINE KUSASIRA AFUNGUKA KUFUNGIWA SHOWS NA MAPROMOTA KISA MSIMAMO WAKE WA KISIASA

Mapromota wa muziki nchini Uganda wameacha kumzingatia msanii wa bendi Catherine Kusasira kwenye shoo zao, kwa hofu kuwa huenda akazua fujo na kupelekea matamasha yao ya muziki kutofanya vizuri. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Kusasira amesema hofu hiyo inatokana na mwelekeo wake wa kisiasa. “Si rahisi kwa mapromota kunishirikisha kwenye shoo zao. Siasa zimeathiri biashara zetu,” amesema “Niko katika kiwango ambacho lazima niombe promota anipee nafasi kwenye shoo au niwasihi mashabiki waje kwenye onesho langu,” ameongeza. Utakumbukwa Catherine Kusasira ni mfuasi mkubwa wa chama tawala nchini Uganda NRM na mwaka wa 2021 alikuwa moja ya kati wasanii waliomkingia kifua Rais Yoweri Museveni kutua uongozi wa nchi hiyo.

Read More
 CATHERINE KUSASIRA AWAJIA JUU MAAFISA WA POLISI UGANDA

CATHERINE KUSASIRA AWAJIA JUU MAAFISA WA POLISI UGANDA

Mwanamuziki wa bendi nchini Uganda Catherine Kusasira ameitaka Idara ya polisi nchini humo kumuomba msamaha kwa kusitishwa onesho lake mapema wiki hii bila sababu za msingi. Katika video aliyochapisha kwenye mitandao yake ya kijamii Kusasira ametoa wito kwa serikali kuwachukulia hatua kali za kisheria maafisa wakuu wa polisi waliofuta show yake iliyokuwa imewavutia zaidi ya watu 3000 kwenye mkesha wa pasaka. Hitmaker huyo wa ngoma ya “I love you” amesema polisi walimvunjia heshima huku akisisitiza kuwa lazima wamuombe radhi kwa kitendo chao cha kusitisha show yake ghafla ikizingatiwa kuwa yeye ni mfuasi mkubwa wa chama cha nrm kilimchompelekea rais Yoweri Museveni kushinda uchaguzi wa mwaka wa 2021. Utakumbuka baada ya polisi kusimamisha show yake saa tatu usiku wa kuamkia jumatatu kuu ya pasaka mashabiki walighadhabishwa na hatua hiyo ambapo walivunja viti kwenye bustani ya Palms Park Ndejje, Kanaaba huku wengine wakitoweka na viti vingine jambo lilowaacha waandaji wa show hiyo wakikadiria hasara kubwa.

Read More
 EDDY YAWE AMTAKA CATHERINE KUSASIRA KUJIUNGA NA CHAMA CHA KISIASA CHA NUP

EDDY YAWE AMTAKA CATHERINE KUSASIRA KUJIUNGA NA CHAMA CHA KISIASA CHA NUP

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Eddy Yawe ametoa wito kwa msanii mwenzake Catherine Kusasira kujiunga na chama cha NUP kinachongozwa na Bob Wine. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Eddy Yawe amesema kama kweli Kusasira amechoshwa na chama tawala cha NRM,itakuwa ni jambo la busara kwa msanii huyo kujiunga na NUP, chama ambacho kinapigania demokrasia nchini Uganda. Kauli ya Eddy Yawe imekuja mara baada ya Catherine Kusasira kukiri hadharani kuwa Chama cha NRm kimemtelekeza licha ya kuingia kifua kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2021,  hivyo anafikiria kujiondoa kwenye chama hicho. Utakumbuka mwaka wa 2021 Catherine Kusasira alimkashifu Bob Wine hadharani kwa hatua ya kushindana na  Rais Yoweri Museveni kwenye uchaguzi mkuu uliopita nchini Uganda.

Read More
 CATHERINE KUSASIRA AFUNGUKA MAZITO KUHUSU CHAMA CHA KISIASA NCHINI UGANDA NRM

CATHERINE KUSASIRA AFUNGUKA MAZITO KUHUSU CHAMA CHA KISIASA NCHINI UGANDA NRM

Msanii mkongwe kwenye muziki nchini Uganda Catherine Kusasira amefunguka ya moyoni baada ya viongozi wa chama cha kisiasa nchini humo nrm kumtelekeza licha ya kutumia nguvu nyingi kuikinga kifua chama hicho kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2021. Kupitia waraka mrefu aliouandika kupitia mtandao wake wa Facebook msanii huyo, amedai kwamba yeye pamoja na wasanii wenzake hawakuthaminiwa vya kutosha kwa kazi nzuri waliyowekeza katika chama cha NRM. Kusasira  amekiri hadharani kutoridhika na wandani wa  chama cha NRM huku akifichua jinsi alivyopoteza marafiki, biashara, na mashabiki wakati akipigania chama hicho lakini cha kushangazwa mpaka sasa hajatuzwa kwa bidii yake. Hata hivyo amesema watu walioelekezwa kuwazawadi wale waliowekeza nguvu zao na kujitolea kwa ajili ya chama cha nrm wamepora pesa zote huku wakiwaacha wakiandamwa na madeni. Lakini pia Kusasira amemshauri rais Yoweri Kaguta Museveni kwamba watu anaowaamini watakuwa chanzo cha anguko lake. Ikumbukwe Catherine Kusasira sio staa wa kwanza kuwachana viongozi wa NRM ambao wamekuwa na mazoea ya kujitakia makuu kwani kipindi cha nyuma tuliwaona mastaa kama Buchaman, Full Figure, na  wengine wengi wakieleza malalamiko yao juu ya uongozi wa chama hicho.

Read More
 CATHERINE KUSASIRA AFUNGUKA SABABU ZA KUUZA GARI LAKE

CATHERINE KUSASIRA AFUNGUKA SABABU ZA KUUZA GARI LAKE

Mwanamuziki Catherine Kusasira aliuza gari lake aina ya Toyota Land cruiser V8 ambalo alizawadiwa na rais Yoweri Museveni. Inadaiwa kuwa mwanamama huyo aliuza gari lake kwa sababu alikuwa anaandamwa na madeni. Sasa akiwa kwenye moja ya interview Catherine Kusasira amejitokeza na kukanusha madai kuwa aliuza gari lake kutokana na madeni. Hitmaker huyo “I love you” amesisitiza kwamba alipiga mnada gari  lake kwa sababu watu wake wa karibu walikuwa wanamuonea wivu. Mwimbaji huyo wa zamani wa lebo ya muziki ya Eagles productions amedai kuwa kuna baadhi ya watu waliibua madai hayo kumuaharibia jina kwa sababu anamuunga mkono Rais Museveni. Hata hivyo Amethibitisha kuwa tayari ameagiza  gari jipya aina toyota SUV ambayo haitawafanya watu wawe na wivu

Read More