Mke wa Bien Achoshwa na Maswali ya Kuzaa Mtoto

Mke wa Bien Achoshwa na Maswali ya Kuzaa Mtoto

Mke wa msanii wa muziki Bien, Chiki Kuruka, ameonyesha kukerwa kwake na watu wanaoendelea kumuuliza na kumshinikiza kuhusu suala la kumzalia mume wake mtoto, akisema maswali hayo yamekuwa yakivuka mipaka ya heshima na faragha yake binafsi. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, amesema amechoshwa na kuulizwa mara kwa mara ni lini atapata mtoto, hasa pale maswali hayo yanapoulizwa hadharani na watu wasiomfahamu. Ameeleza kuwa licha ya baadhi ya watu kudai kuuliza kwa nia njema, wapo wengine wanaokwenda mbali zaidi kwa kutoa kauli zinazoumiza. Chiki amefichua kuwa amewahi kukutana na maoni kutoka kwa wanawake na wanaume wakimtaka Bien aoe au atafute mwanamke mwingine ili amzalie watoto, kauli alizosema si za haki na hazipaswi kuvumiliwa katika jamii ya sasa. Mke huyo wa Bien amesisitiza kuwa kama ambavyo jamii imekuwa ikiheshimu wazazi na kuwaacha nje ya mijadala isiyohusu umma, vivyo hivyo miili ya wanawake, hususan masuala ya uzazi, yanapaswa kuheshimiwa na kutojadiliwa hadharani bila ridhaa yao.

Read More
 CHIKI KURUKA AMKINGIA KIFUA BIEN WA SAUTI SOL KWA MADAI YA KUPANGA UZAZI

CHIKI KURUKA AMKINGIA KIFUA BIEN WA SAUTI SOL KWA MADAI YA KUPANGA UZAZI

Mke wa msanii Bien, Chiki Kuruka amemkingia kifua msanii huyo kutokana na kauli yake ya kutaka kumsaidia kupanga uzazi kwa kukata mshipa wake wa uzazi maarufu vesectomy. Akizungumza na Mpasho mrembo huyo amesema kauli hiyo ilitafsiriwa vibaya na waandishi wa habari kwani Bien alikuwa anajaribu kuwaelimisha wanaume kuhusu umuhimu wa kuwasaidia wake zao kwenye suala la kupanga uzazi. Katika hatua nyingine amekosoa vyombo vya habari kwa kuripoti habari za uwongo dhidi ya mume wake Bien huku akisisitiza haja ya waandishi kuwa mstari wa mbele katika kuzingatia maadili ya uandishi wa habari ikiwemo kuandika habari za ukweli na uhakika kama njia ya kuepusha upotoshaji. Utakumbuka mwezi Julai mwaka huu Bein alinukuliwa akisema yupo tayari kukata mshipa wa uzazi maarufu vasectomy punde atakapo pata watoto na mke wake Chiki Kuruka. Msanii huyo wa Sauti Sol ameenda mbali Zaidi na kusema kwamba upangaji uzazi barani Afrika ni swala ambalo limeachiwa wanawake, hivyo hawezi kumwachia mke wake mzigo huo pekee licha ya wanaume wengi kuogopa kufanyiwa vasectomy.

Read More