Mke wa Bien Achoshwa na Maswali ya Kuzaa Mtoto
Mke wa msanii wa muziki Bien, Chiki Kuruka, ameonyesha kukerwa kwake na watu wanaoendelea kumuuliza na kumshinikiza kuhusu suala la kumzalia mume wake mtoto, akisema maswali hayo yamekuwa yakivuka mipaka ya heshima na faragha yake binafsi. Kupitia ujumbe aliouchapisha kwenye mitandao ya kijamii, amesema amechoshwa na kuulizwa mara kwa mara ni lini atapata mtoto, hasa pale maswali hayo yanapoulizwa hadharani na watu wasiomfahamu. Ameeleza kuwa licha ya baadhi ya watu kudai kuuliza kwa nia njema, wapo wengine wanaokwenda mbali zaidi kwa kutoa kauli zinazoumiza. Chiki amefichua kuwa amewahi kukutana na maoni kutoka kwa wanawake na wanaume wakimtaka Bien aoe au atafute mwanamke mwingine ili amzalie watoto, kauli alizosema si za haki na hazipaswi kuvumiliwa katika jamii ya sasa. Mke huyo wa Bien amesisitiza kuwa kama ambavyo jamii imekuwa ikiheshimu wazazi na kuwaacha nje ya mijadala isiyohusu umma, vivyo hivyo miili ya wanawake, hususan masuala ya uzazi, yanapaswa kuheshimiwa na kutojadiliwa hadharani bila ridhaa yao.
Read More