Davido na Chioma wafunga ndoa

Davido na Chioma wafunga ndoa

Staa wa muziki kutoka Nigeria Davido ameripotiwa kufunga ndoa na mpenzi wake Chioma ambaye ni mzazi mwenza wa mtoto wao aliyefariki dunia “Ifeanyi”. Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari toka Nigeria. Ndoa hiyo inayotajwa kuwa ya kitamaduni ilifungwa nyumbani kwa baba yake Davido na ilihudhuriwa na watu wa familia za wawili hao pekee. Katika hafla hiyo, inaelezwa hakuna aliyekubaliwa kupiga picha wala kuchukua video. Pia inaelezwa, mahari ya Chioma ililipwa yote ingawaje alikuwa amekataa kuolewa na Davido kufuatia kifo cha mwanae ambaye alimtizamia kama ndiye aliyewaleta pamoja. Ndoa hiyo ilikuwa sharti ifungwe ili Ifeanyi ambaye alifariki kwenye swimming pool nyumbani kwao, aweze kuzikwa kama mmoja wa familia ya Davido, kulingana na tamaduni za jamii ya Igbo. Aidha, kabla ya kifo cha Ifeanyi, Davido na Chioma walikuwa tayari wametangaza rasmi kwamba watafunga ndoa mwakani 2023.

Read More
 Davido mbioni kufunga ndoa mwaka 2023

Davido mbioni kufunga ndoa mwaka 2023

Staa wa muziki kutoka nchini Nigeria Davido ameahidi kuwa mwaka 2023 atafunga ndoa na mpenzi wake Chioma. Davido amebainisha hayo akiwa na baby mama wake huyo pamoja na mchungaji wake Tobi Adegboyega huko Uingereza, alipoenda kumtambulisha Chioma kwa mchungaji huyo. “Our wife, our real wife,” anasikika Mchungaji Tobi akieleza, na Davido akaongezea, “Hundred per cent, going down 2023.” Mbali na hilo kupitia instastory ya Staa davido ameshare picha na video zikionesha mpenzi wake Chioma akipewa zawadi ya Mkoba na Mchungaji tobiadegboyega_Ambapo mkoba huo unatajwa kuwa na Thamani ya $90,000 zaidi ya million 9 za Kenya. Ikumbukwe, Davido na Chioma walianza mahusiano yao tangu mwaka 2017, na 2019 Davido alimvisha pete ya uchumba Chioma. Hata hivyo wakaja kuachana mwaka 2020, wakabaki kuwa walezi wa mtoto wao. Julai mwaka huu wakawa wanahusishwa kurudiana, kisha baadae wakathibitisha na sasa wamepanga kufunga pingu za maisha ifikapo mwakani.

Read More