CHRIS ROCK: SITAONGELEA SAKATA LA WILL SMITH KUNIPIGA KOFI HADI NILIPWE
Mchekeshaji kutoka Marekani Chris Rock amesema hatozungumzia sakata la kuchapwa kofi na Will Smith hadi pale atakapolipwa pesa. Mchekeshaji huyo alizungumza hayo mbele ya wahudhuriaji wa onesho lake juzi Ijumaa, ambapo alisema “Mimi niko sawa, nina hii show nzima, lakini sitaongelea kuhusu hilo hadi pale ambapo nitalipwa. Maisha ni mazuri, nimerudisha hali yangu ya kusikia.” Kwa mujibu wa tovuti ya TMZ, wameichambua kauli hiyo na kusema kwamba pengine Chris Rock anataka kulipwa pesa ndefu kwa ajili ya kufanya mahojiano maalum kuhusu tukio lile. Au pia ana mpango wa kufungua kesi dhidi ya Will Smith ambapo atalipwa pesa ndefu.
Read More