Perplexity Yajitokeza kwa Ofa Kubwa ya Kununua Chrome

Perplexity Yajitokeza kwa Ofa Kubwa ya Kununua Chrome

Kampuni ya Perplexity, inayojulikana kwa app yake inayoshindana na ChatGPT, Grok, na DeepSeek, imeweka ofa ya Dola Bilioni 34.5 kununua browser maarufu ya Chrome. Google inahofia kuuza browser hii kwani inatumia Chrome kujiwekea faida, kuweka matangazo, na kukusanya data nyingi za watumiaji duniani. Hadi sasa, Google haijaonyesha muamko rasmi, na ina mpango wa kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama ya Marekani unaolenga kupunguza nguvu zake. Chrome ni browser inayotumika zaidi duniani ikilinganishwa na Safari na Firefox, na ni kitovu cha mawasiliano, matangazo, na matumizi ya AI. Perplexity inaamini kumiliki Chrome kutawapa mamilioni ya watumiaji, kuwapa nafasi ya kueneza huduma zao za AI na kuleta ushindani dhidi ya kampuni kubwa kama OpenAI. Ingawa thamani ya Perplexity ni Bilioni 20, kampuni hiyo imeonyesha nia kubwa kwa kutoa ofa ya Bilioni 34.5 kununua Chrome. Hii inaweza kuwa hatua kubwa ya kuipita ChatGPT kwa watumiaji wengi zaidi. Hali hii inaonyesha kampuni za AI zinafanya mikakati ya kununua browsers, huku OpenAI pia ikiandaa kuwa na browser yake binafsi.

Read More
 Google Yazindua Mfumo Mpya wa Kudhibiti Ad Blockers kwa Chrome

Google Yazindua Mfumo Mpya wa Kudhibiti Ad Blockers kwa Chrome

Kampuni ya teknolojia ya Google imeanzisha mfumo mpya wa kudhibiti na kuzuia matumizi holela ya extensions (viongezo) vinavyotumika kuzima matangazo kwenye kivinjari chake cha Chrome. Hatua hii inalenga kulinda mapato yanayotokana na matangazo, ambayo ni chanzo kikuu cha fedha kwa kampuni hiyo. Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Google, mfumo huo mpya utahakikisha kuwa extensions zote zinazozuia matangazo zinatekeleza sera mpya za usalama na uwazi. Hii ni pamoja na matumizi ya Manifest V3, mfumo wa kisasa unaolenga kudhibiti namna viongezo vinavyoingiliana na tovuti na taarifa za watumiaji. Hatua hiyo imeibua mjadala mkubwa miongoni mwa watumiaji wa intaneti na wapenda faragha, kwani wengi walitegemea extensions kama AdBlock na uBlock Origin kuondoa matangazo yanayokera na kurahisisha matumizi ya mtandao. Google imesema haitapiga marufuku moja kwa moja extensions zote za kuzuia matangazo, lakini zile ambazo hazitazingatia viwango vipya, zitafutwa kutoka kwenye Chrome Web Store. Kampuni hiyo imesisitiza kuwa inalenga kuweka uwiano kati ya faragha ya mtumiaji, utendaji wa kivinjari, na kulinda mazingira ya watengenezaji maudhui wanaotegemea mapato ya matangazo. Wadau wa teknolojia wameonya kuwa mabadiliko haya huenda yakapunguza uhuru wa watumiaji kuchagua namna wanavyotumia mtandao, huku wengine wakitafsiri kama juhudi za Google kuhakikisha kuwa matangazo yake yanaonekana zaidi kwa watumiaji wa Chrome duniani kote.

Read More