Vincent Aboubakar avunjiwa mkataba Al Nassrna kisa Ronaldo

Vincent Aboubakar avunjiwa mkataba Al Nassrna kisa Ronaldo

Klabu ya Al Nassr imevunja mkataba na mshambuliaji Vincent Aboubakar kwa makubaliano ya pande zote mbili ili kutoa nafasi moja ya mchezaji wa kigeni kwa ajili ya kumsajili Cristiano Ronaldo. Mamlaka ya soka ya Saudi Arabia inatuhusu wachezaji 8 tu wa kigeni lakini kwa sasa klabu hiyo ina jumla ya wachezaji 9 pamoja na Ronaldo hivyo Aboubakar amelazimika kufanyika kondoo wa kuteketezwa (sacrificial lamb). Kwa mujibu wa ripoti mshambuliaji huyo raia wa Cameroon amepokea ofa nzuri Barani Ulaya huku Manchester United ikiwa moja ya vilabu vinavyomlenga.

Read More
 Ronaldo aukataa ukubwa ndani ya Al Nassr

Ronaldo aukataa ukubwa ndani ya Al Nassr

 Rais wa Klabu ya Al Nassr, Musalli Al Muammar amesema kuwa staa wa timu hiyo Cristiano Ronaldo ameomba atendewe sawa na wachezaji wenzake ndani ya kikosi, asipendelewe. “Wakati wa makubaliano, Ronaldo aliomba atendewe sawa na wachezaji wengine kikosini, kwenye upande wa zawadi za motisha na kanuni za timu.”- Musalli Al Muammar Rais huyo wa Al Nassr ameongeza kuwa mshahara wake ni wa juu zaidi, huku akishindwa kutaja kiasi halisi cha fedha na kuongeza makubaliano yao yanamanufaa ya faida za kibiashara pia. “Makubaliano na Ronaldo hayaishii kwenye mpira pekee, atasaidia pia kwenye Al Nassr Club Academy mpango ambao tumepanga pamoja na kuiwakilisha historia ya klabu.”

Read More
 Cristiano Ronaldo atambulishwa na Klabu ya Al Nassr ya Saudi Arabia

Cristiano Ronaldo atambulishwa na Klabu ya Al Nassr ya Saudi Arabia

Staa wa Soka wa Ureno Cristiano Ronaldo amepokewa rasmi na ametambulishwa mbele ya mashabiki wa Club ya Al Nassr ya Saudi Arabia. Ronaldo aliyejiunga na Al Nassr kama Mchezaji huru baada ya kuvunja mkataba na Man United aliambatana na Familia yake kwa maana ya Watoto na Mpenzi wake Georgina Rodriguez. Timu ya Al Nassr iliyomsajili Ronaldo na Club ya Newcastle ya England zinamilikiwa na Mmiliki mmoja na inadaiwa kuwa katika mkataba wa Ronaldo kuna kipengele cha kwenda Newcastle kwa mkopo kama watafuzu kucheza UEFA Champignons League. Ronaldo, anakuwa mchezaji wa kwanza mwenye jina kubwa duniani kukipiga katika klabu hiyo kwenye historia ya maisha yake ya soka.

Read More
 Ronaldo awasili nchini Saudi Arabia

Ronaldo awasili nchini Saudi Arabia

Nyota mpya wa klabu ya Al-Nassr, Cristiano Ronaldo tayari amewasili nchini Saudi Arabia akiwa pamoja na familia yake akiambatana na watu wa mambo ya kiufundi na waandishi wa habari wakitua kutoka jijini Madrid. Kinachosubiriwa kwa sasa ni nyota huyo kutambulishwa rasmi na klabu ya Al-Nassr mbele ya umati wa mashabiki katika uwanja wa Mrsool Park, unaomilikiwa na klabu hiyo uliyopo ndani ya jiji la Riyadh, Saudi Arabia ambao unaingiza mashabiki 25,000. Ronaldo, atakuwa mchezaji wa kwanza mwenye jina kubwa duniani kukipiga katika klabu hiyo kwenye historia ya maisha yake ya soka.

Read More
 Cristiano Ronaldo kutambulishwa kesho na klabu ya Al-Nassr

Cristiano Ronaldo kutambulishwa kesho na klabu ya Al-Nassr

Aliyekuwa mchezaji wa Manchester United, Cristiano Ronaldo atatambulishwa rasmi na klabu ya Al-Nassr mbele ya umati wa mashabiki katika uwanja wa Mrsool Park, unaomilikiwa na klabu hiyo uliyopo ndani ya jiji la Riyadh, Saudi Arabia ambao unaingiza mashabiki 25,000. Ronaldo amewasili leo Saudi Arabia pamoja na familia yake akiambatana na watu wa mambo ya kiufundi na waandishi wa habari. Ronaldo atakuwa mchezaji wa kwanza mwenye jina kubwa duniani kukipiga katika klabu hiyo kwenye historia ya maisha yake ya soka. Vile vile waziri wa michezo wa Saudi Arabia Abdulaziz bin Turki Al-Feisal ameahidi atazisapoti klabu zote nchini humo endapo madili makubwa yatatokea.

Read More
 Cristiano Ronaldo ajiunga rasmi na klabu ya Al-Nassr ya Saudi Arabia

Cristiano Ronaldo ajiunga rasmi na klabu ya Al-Nassr ya Saudi Arabia

Klabu ya Al Nassr ya Saudi Arabia imethibitisha kumsajili gwiji wa soka raia wa Ureno, Cristiano Ronaldo kwa mkataba unaodumu hadi mwaka 2025. Habari za kusajiliwa kwake zimethibitishwa Ijumaa usiku na klabu hiyo kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii. Klabu imeandika “Mwanasoka mkubwa zaidi duniani amesainiwa rasmi,” ujumbe ulioambatana na picha za Ronaldo akiwa ameshikilia jezi ya Al Nassr. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 aliondoka Manchester United baada ya kusitishwa kwa kandarasi yake mwezi Novemba na amekuwa mchezaji huru tangu wakati huo baada ya kutofautiana na klabu hiyo kutokana na kushindwa kuhama msimu wa joto na mahojiano aliyoyafanya na mtangazaji maarufu Piers Morgan na kuzua taharuki kati yake na waajiri wake

Read More
 Cristiano Ronaldo afanya mazoezi kwenye uwanja wa Real Madrid

Cristiano Ronaldo afanya mazoezi kwenye uwanja wa Real Madrid

Aliyekuwa mchezaji wa Manchester United, Cristiano Ronaldo jana Disemba 14, 2022 alikuwa katika uwanja wa Real Madrid na kufanya mazoezi maalum chini kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti. Cristiano alikuwa pamoja na mwanawe na aliomba ruhusa ya kufanya mazoezi katika vituo vya Madrid baada ya Timu yake Kutolewa kwenye michuano ya Kombe la Dunia. Rais wa Real Madrid Florentino Perez na Timu yake walikubali ombi la Ronaldo bila kipingamizi kutoka na uhusiano mzuri kati yao. Ronaldo alifanya mazoezi ya peke yake tofauti na kikosi cha kwanza, cha Carlo Ancelotti. Kwa sasa hakuna mazungumzo yanayoendelea ya kumrejesha Real Madrid.

Read More
 Cristiano Ronaldo akanusha taarifa za kujiunga na Klabu ya Al Nassr

Cristiano Ronaldo akanusha taarifa za kujiunga na Klabu ya Al Nassr

Mshambuliaji wa timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo amekanusha taarifa za kuwa atajiunga na Klabu ya Al Nassr ya nchini Saudi Arabia mwezi January 2023. Ronaldo amesema “No, that’s not true — not true” baada ya mchezo wa Jana dhidi ya Switzerland. Klabu hiyo imetajwa kumuwekea CR7 Ofa ya ($200 million) zaidi ya KSh. Milioni 24.6 kwa mwaka mmoja ambapo mkataba wake unatajwa kuwa wa miaka miwili na nusu.

Read More
 Manchester United yatangaza kumaliza na Cristiano Ronaldo

Manchester United yatangaza kumaliza na Cristiano Ronaldo

Klabu ya Manchester United imetangaza kumalizana na nyota wake Cristiano Ronaldo. Man United imetoa taarifa rasmi usiku huu kwamba, pande zote mbili zimefikia makubaliano ya kuvunja mkataba na nyota huyo anatakiwa kuondoka haraka iwezekanavyo. Ronaldo anaondoka Man United kufuatia mahojiano yake na Piers Morgan ambayo yaliishambulia Klabu pamoja na menejimenti. Kwenye tamko lake la mwisho, CR7 amesema anaipenda Man United na anawapenda mashabiki, ila ni muda wa kutafuta changamoto mpya.

Read More
 RONALDO AMEVURUGA KIWANGO CHA BRUNO FERNANDES MAN UNITED

RONALDO AMEVURUGA KIWANGO CHA BRUNO FERNANDES MAN UNITED

Cristiano Ronaldo kurejea ndani ya Manchester United kumesababisha mshambuliaji wa timu hiyo, Bruno Fernandes kupoteza ubora wake. Hayo ni maoni ya nguli wa timu hiyo, Andy Cole ambaye ameeleza kuwa Wareno hao wanapata shida kucheza pamoja. Fernandes alikuwa staa wa timu na kuonyesha ubora wa juu lakini ameshindwa kuwa katika ubora wa juu msimu huu. “Kila kitu kimebadilika, Bruno hajawa yule alivyokuwa, ni kama ana hofu ya Ronaldo, nafikiri hatakiwi kuwa na hofu kwa kuwa wote ni wachezaji wakubwa,” alisema Cole.

Read More