Daddy Andre afunguka madai ya kuharibu wimbo wa Fred Sebata

Daddy Andre afunguka madai ya kuharibu wimbo wa Fred Sebata

Msanii kutoka nchini Uganda Daddy Andre amewajibu wanaodai kuwa aliharibu wimbo wa msanii mkongwe Lord Fred Sebatanoting uitwao Sam Wange. Kwenye mahojiano yake karibuni amesema alijaribu kuupa wimbo huo ladha ya kisasa kwa kutumia mdundo tofauti ila mashairi yake yalisalia yalivyo kwa kuwa wimbo wenyewe una hakimiliki. Msanii huyo ameongeza kuwa kama mwenye wimbo angelalamika na toleo lao basi angewashtaki kwa kuharibu wimbo huo uliofanya vizuri kipindi cha nyuma. Mwezi uliopita Daddy Andre na Sheebah Karungi walipata ukosoaji mkubwa mtandaoni kwa kuurudia wimbo wa Sam Wange wake Fred Sebata,hatua  ambayo ilichukuliwa kama kuwakosea wasanii wakongwe. Mashabiki walimshauri Daddy Andre kuwaheshimu wakongwe badala ya kufanya nyimbo zao bila kuzingatia ubora.

Read More
 DADDY ANDRE ATAKA WAANDISHI WA NYIMBO NA MAPRODYUZA KUPEWA KIPAU MBELE UGANDA

DADDY ANDRE ATAKA WAANDISHI WA NYIMBO NA MAPRODYUZA KUPEWA KIPAU MBELE UGANDA

Msanii na Prodyuza Daddy Andre amedai kwamba maprodyuza na waandishi wa nyimbo wanachukuliwa poa nchini uganda licha ya wao kuwa nguzo muhimu kwenye tasnia ya muziki. Katika mahojiano yake hivi karibuni Daddy Andre amekiri kutofaidi na kipaji chake cha uandishi wa nyimbo huku akipendekeza wasanii waanze kugawana na waandishi wa nyimbo asilimia 50 ya mapato ya nyimbo zao. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Kola” amesema uandishi wa nyimbo inahitaji ubunifu na muda mwingi ila mwisho wa siku waandishi wa nyimbo huambulia patupu jambo ambalo amedai sio cha kingwana. Hata hivyo ametoa wito kwa wabunge kutunga sheria itakayowalinda waandishi wa nyimbo na maprodyuza ila waanze kupata mgao wa mapato wa nyimbo wanazozifanyia kazi.

Read More
 DADDY ANDRE ATOA ILANI KWA NINA ROZ KUKOMA KUTUMIA NYIMBO ALIZOMUANDIKIA

DADDY ANDRE ATOA ILANI KWA NINA ROZ KUKOMA KUTUMIA NYIMBO ALIZOMUANDIKIA

Msanii na Prodyuza kutoka Uganda Daddy Andre ametoa onyo kwa Nina Roz kukoma kutumia nyimbo  alizomuandikia kipindi wanafanya kazi pamoja kwenye shows zake. Kupitia barua ya mawikili wake Daddy Andre amemtaka Nina Roz amlipe shillingi millioni 120 za Uganda la sivyo atamfungulia kesi mahakamani. Kulingana vyanzo vya karibu na Daddy Andre, prodyuza huyo anataka alipwe shillingi millioni 30 za Uganda kwa kila wimbo aliomuandikia Nina Roz. Nyimbo hizo ni kama Nangana, Billboard Kipande, Enyonta, na Andelle. Wawili hao walisaini mkataba wa kufanya kazi pamoja mwaka wa 2020 lakini walikuja wakaachana mwaka wa 2021 baada ya kuingia ugomvi na tangu wakati huo wamekuwa wakirushiana maneno makali kwenye mahojiano mbali mbali. Notisi hiyo ya Daddy Andre inakuja wakati huu Nina Roz amefungua kesi polisi akimtuhumu prodyuza huyo kumuibia gari aina Mark X. Inadaiwa Daddy Andre alichukua gari la Mrembo huyo kama malipo ya kazi ambayo prodyuza huyo alimfanyia kipindi wanafanya kazi pamoja.

Read More
 DADDY ANDRE ATUHUMIWA KUHUSIKA KWENYE WIZI WA GARI

DADDY ANDRE ATUHUMIWA KUHUSIKA KWENYE WIZI WA GARI

Msanii na Prodyuza kutoka nchini Uganda Daddy Andre ametuhumiwa kumuibia gari mpenzi wake wa zamani Nina Roz. Kulingana na kesi iliyowasilishwa kwa polisi Daddy Andre alimuomba Nina Roz gari atumie kwenye shughuli zake mwaka wa 2020 lakini alikataa kumrudisha gari hilo. Kwenye taarifa ya polisi, Nina Roz anadaiwa kununua gari hilo kwa mkopo mwaka 2020 ambapo alilipa shillingi millioni 10 za uganda kati ya shillingi millioni 21 alizokuwa anadaiwa. Taarifa hiyo imeeleza kuwa  Daddy Andre ambaye alikuwa shahidi wa Nina Roz wakati ananunua gari hilo alibadilisha umiliki wa gari na kuwa lake baada ya mpenzi wake huyo wa zamani kumpokeza shillingi millioni 11 za uganda akamilishe deni la gari hilo. Hata hivyo dalali aliyebadilisha usijali wa gari kutoka kwa Nina Roz kwenda Daddy Andre tayari ametiwa mbaroni huku polisi wakiendelea na uchunguzi kubaini ukweli kuhusu sakata hilo.

Read More
 DADDY ANDRE AMTEUA EMMA CARLOS KUWA MENEJA WAKE

DADDY ANDRE AMTEUA EMMA CARLOS KUWA MENEJA WAKE

Msanii kutoka nchini Uganda Daddy Andre amemteua meneja Emma Carlos kusimamia muziki wake upande wa shows. Daddy andrea ambaye yupo chini ya Black Market Records amechukua hatua hiyo baada ya mapromota kulalamika kuwa amekuwa akikwepa baadhi ya shows zake jambo ambalo karibu limuaribie brand yake ya muziki. Emma Carlos atatakiwa kuhakikisha anachukua maombi ya shows za msanii huyo lakini pia atafuatilia kwa ukaribu ratiba  zake ili aweze kutumbuiza kwenye shows zake zote bila kukosa. Utakumbuka Emma Carlos ni moja kati ya mameneja wakongwe kwenye muziki nchini ikizingatiwa kuwa amesimamia kazi za wasanii wengi nchini akiwemo Coco Finger, Kalifah Aganagah Radio & Weasel na wengine wengi.

Read More
 BLACK MARKET RECORDS YAMTAKA PRODYUZA DADDY ANDRE KUFUFUA MUZIKI WA ANGELLA KATATUMBA

BLACK MARKET RECORDS YAMTAKA PRODYUZA DADDY ANDRE KUFUFUA MUZIKI WA ANGELLA KATATUMBA

Angella Katatumba ni moja kati wasanii ambao wamedumu kwenye tasnia muziki nchini uganda kwa muda mrefu. Licha ya kuanza muziki miaka 15 iliyopita, mrembo huyo mwenye umri wa miaka 46 amekuwa akipambana kuupeleka muziki wake kimataifa. Wakati alikutana na prodyuza Daddy Andre mwaka wa 2018 walirekodi wimbo wa pamoja uitwao “Tonelabira” ambao ulikuja ukawa mkubwa sana nchini Uganda mwaka wa 2019. Hata hivyo walikuja wakakosana vibaya baada ya wawili hao kuchanganya raha ya mapenzi na muziki, jambo lilompelekea Angella katatumba kusuasua kimuziki. Sasa taarifa mpya mjini ni kwamba lebo ya muziki ya Black Market Records imetoa rai kwa prodyuza Daddy Andre kumshika tena mkono Angella Katatumba  kama njia kufufua muziki wake. Kulingana na chanzo cha karibu na lebo ya Black Market, Daddy Andrea ana mpango wa kumtayarishia Angella Katatumba nyimbo nne kali mwaka  huu wa 2022 ambazo zitakuwa moto wa kuotea mbali. Utakumbuka wawili hao kwa sasa wana wimbo wa pamoja uitwao “Wendi” ambao unafanya vizuri kwenye chati mbali mbali nchini uganda.

Read More
 DADDY ANDRE AKANA KUTOKA KIMAPENZI NA VIDEO VIXEN BOBO SHAN

DADDY ANDRE AKANA KUTOKA KIMAPENZI NA VIDEO VIXEN BOBO SHAN

Msanii na prodyuza wa muziki kutoka nchini Uganda Daddy Andre amekanusha uvumi unaotembea kwenye mitandao ya kijamii kuwa anatoka kimapenzi na video vixen Bobo Shan ambaye anadaiwa ana uja uzito wake . Akiwa kwenye moja ya Interview Daddy Andrea  amesema uvumi huo hauna ukweli wowote ikizingatiwa kuwa hamfahamu kabisa mrembo huyo. Hitmaker “Omwana Bandi” amesema ikutokea yupo kwenye mahusiano mapya atatambulisha mpenzi wake kwa umma kwani hapendi kuficha mahusiano yake. Kauli Daddy Andre imekuja mara ya kudaiwa prodyuza yupo kwenye mahusiano ya kimapenzi na video vixen Bobo Shan ambaye watumiaji wa mitando ya kijamii walienda mbali zaidi na kuhoji kwamba ana uja uzito wake.

Read More
 DADDY ANDREA NA ANGELLA KATATUMBA WAFUFUA TENA PENZI LAO

DADDY ANDREA NA ANGELLA KATATUMBA WAFUFUA TENA PENZI LAO

Wasanii Angella Katatumba na Daddy Andrea walivunja uhusiano wao mwaka wa 2020 baada andrea kudinda kufanya vipimo vya HIV.   Kwenye mahojiano mbali mbali Daddy Andrea alithibitisha kwamba hajawahi mpenda Angella Katatumba na jambo hilo lilimsumbua sana mrembo huyo.   Andrea alienda mbali zaidi na kuanza mahusiano mapya na Nina Roz ila mahusiano yao yalikuja yakiingiwa na ukungu kwa madai ya usaliti na kumvunjiana heshima.   Sasa mapya yameibuka  baada ya Angella Katatumba kuthibitisha kwamba wamerudiana na Daddy Andrea kwenye moja ya interview.   Hitmaker huyo wa amesema amerudiana na mpenzi wake wa zamani Daddy Andrea baada ya prodyuza huyo kumuomba msamaha.   Wawili hao wamedai kwamba tayari wamerekodi wimbo wa pamoja uitwao Wendi ambao utatoka hivi karibuni.   Ikumbukwe daddy andrea na Angella Katatumba wapo chini ya lebo ya muziki ya black market records ambayo inasimamia kazi zao za muziki.    

Read More