EP ya Diamond Platnumz “First Of All” yashinda tuzo Marekani

EP ya Diamond Platnumz “First Of All” yashinda tuzo Marekani

EP ya Diamond Platnumz “First Of All” ama FOA imeshinda tuzo ya album bora ya mwaka 2022 kwenye tuzo za African Entertainment Awards USA (AEAUSA) zilizotolewa usiku wa kuamkia leo huko Marekani. Kwenye tuzo hizo za 8, FOA ilikuwa imeingia kwenye kipengele cha album bora ya mwaka ambapo ilikuwa ikichuana na album nyingine kama “Rave & Roses” ya Rema, “Catch Me If You Can” ya Adenkunle Gold, “Affection” ya Magasco Bboy pamoja na “The Guy” ya Mi Abaga FOA Ep ilitoka rasmi Machi 12, mwaka 2022 ikiwa na jumla ya ngoma 10 huku wanamuziki wanne tu wakiwa wamepewa shavu la kusikika kwenye project hiyo ambao ni Zuchu, Mbosso, Adenkunle Gold na Jaywillz.

Read More
 KHADIJA KOPA AVUNJA KIMYA CHAKE KUHUSU ISHU YA DIAMOND KUTOKA KIMAPENZI NA ZUCHU

KHADIJA KOPA AVUNJA KIMYA CHAKE KUHUSU ISHU YA DIAMOND KUTOKA KIMAPENZI NA ZUCHU

Moja kati ya headlines zinazo gonga vichwa vya habari mtandaoni ni issue inayomtaja mwanamuziki diamond platnumz kutaka kumuoa mwanamuziki mwenzake zuchu , sakata ambalo kila mtu analizungumzia katika namna yake. Sasa mama mzazi wa zuchu, Khadija Kopa amezungumzia kile kinachoitwa penzi jipya mtandaoni kati ya binti yake, Zuchu na Diamond Platnumz. Kwenye mahojiano Kopa  ambaye ni Malkia wa muziki wa Taarab nchini tanzania amepuuzilia mbali madai hayo na kusema aliwasiliana na bintiye na akamueleza hali halisi kuwa huo ni uvumi tu usio na msingi. Zuchu alimhakikishia mama yake kuwa Diamond amekuwa akimuonyesha heshima kubwa na hakuna chochote kinachoendelea kati yao. “Wakati ule Zuhura aliniambia Diamond anamheshimu sana na hajawahi hata siku moja kuniambia vitu vya kipuzi. Nilishtuka maanake watu walikuwa wanavumisha kupita kiasi” amesema na kuongeza; “Nilishangaa mbona walivumisha kupita kiasi, mimi mwenyewe sikushughulika sana, nilimuuliza Zuhura mbona watu walivumisha sana ama kuna kitu chochote. Aliniambia hamna wala hajawahi kuvunjiwa heshima hata siku moja, mimi nilichukulia kama kitu cha kawaida” alisema Khadija Kopa. Aliendelea kwa kusema; “Diamond mimi ananiona kama mama yake kusema ukweli, tangu zamani, kabla hata huyo Zuchu hajaenda Wasafi, amenichukulia kama mama yake”.

Read More
 ZARI AVUNJA UKIMYA TAARIFA ZA KUOLEWA

ZARI AVUNJA UKIMYA TAARIFA ZA KUOLEWA

Mrembo Zari The Bosslady amewataka mashabiki wake kupuuzia taarifa zinazodai kuwa ameolewa. Zari ambaye ni baby mama wa msanii wa BongoFleva amesema picha hizo zinazodaiwa ni za ndoa yake, zimetoka kwenye kuandaa video ya msanii chipukizi wa muziki wa Injili. Utakumbuka mwaka wa 2020 ilisemekana kuwa Zari pia ameolewa na mwanaume aitwaye ‘King Bae’ lakini baadaye alikuja kuweka wazi hilo halikuwa kweli. Mwanamama huyo wa watoto watano sasa ni miongoni mwa wanawake wenye nguvu ya ushawishi Afrika Mashariki, huku akiwa na followers zaidi ya milioni 9.7 kwenye mtandao wa Instagram.

Read More
 AMBER LULU: NAMTAMANI SANA JUX

AMBER LULU: NAMTAMANI SANA JUX

Msanii wa Bongofleva Amber Lulu amemtaja Juma Jux kuwa ndio mwanaume anayetamani kupata naye mtoto kwa sababu ana akili, yupo smart na atamuongoza vyema lakini pia amekuwa akimfuatilia msanii huyo kwa muda mrefu. Mrembo huyo ambaye anafanya poa na singo yake mpya iitwayo Nimeachika amesema amepanga kuzaa watoto 5 kila mmoja na baba yake sababu akizaa na baba mmoja kisha akafariki yeye ataishia kupata tabu na watoto. Ikumbukwe pia Amber Lulu kipindi cha nyuma alishaweka wazi kutamani kuwa kwenye mahusiano na Diamond Platnumz, lakini hata hivyo nafasi ya kuwa na Diamond inaonekana ni nyembamba sababu baada ya hitmaker huyo wa Naanzaje kuzaa watoto 4 na wanawake tofauti amekiri hivi karibuni kuwa kwa sasa kuwa kwenye mahusiano na wanawake sio kipaumbele chake bali nguvu amezielekeza kwenye kuzidi kufanya kazi ili kuendelea kufanikiwa kiuchumi.

Read More
 DIAMOND PLATINUMZ APEWA JEZI NA TIMU KUBWA USA

DIAMOND PLATINUMZ APEWA JEZI NA TIMU KUBWA USA

Msanii mwenye tuzo nyingi zaidi Afrika Mashariki na Kati Diamond Platnumz amepewa heshima kubwa na timu ya Mpira wa Marekani inayofahamika kama washington NFL. Diamond amekabidhiwa jezi namba 99 huku ikipambwa na jina lake mgongoni Platnumz. Timu hiyo ambayo inashikilia nafasi ya pili kwenye Ligi ya mpira wa Marekani imechapisha picha hizo za Diamond kwenye ukurasa wao wa Instagram na kuandika “diamond platnumz repping the Burgundy & Gold” Diamond Platnumz anakuwa msanii wa pili kutoka bara la Afrika kukabidhiwa Jezi na timu kubwa za mpira duniani baada ya siku chache zilizopita burna boy kupewa jezi na klabu ya Manchester United Diamond kwa sasa yupo nchini Marekani kwaajili ya ziara ya kimuziki ambapo mpaka sasa ameshatumbuiza kwenye miji miwili.

Read More
 CAMILA CABELLO AFIKISHA MAUZO YA DIAMOND KUPITIA WIMBO WA “HAVANA”

CAMILA CABELLO AFIKISHA MAUZO YA DIAMOND KUPITIA WIMBO WA “HAVANA”

Wimbo wa msanii camila cabello kutoka nchini Cuba uitwao “Havana” uliotoka mwaka wa 2017 ambao amemshirikisha rappa Young Thug, umefanikiwa kuuza (units) millioni 10 ambayo ni ngazi ya juu kabisa. Camila ambaye ni member wa kundi bora la muziki kuwahi kutoka ulimwenguni la fifty harmony, kutokana na hatua hiyo chama cha Recording Industry Association of America (RIAA) kimekabidhi tuzo maalumu yaani (Plaque) maarufu kwa jina Almasi au (Diamond). Camila Cabello anakuwa msanii wa kwanza kutoka Cuba kufikia mafanikio hayo makubwa kupitia wimbo mmoja. Lingine usilo lijua kuhusu “Havana” ni kuwa, rappa Young Thug ambaye ndiye kashirikishwa kwenye wimbo huo, hakutaka kutia verse yake katika havana kutokana na kutoielewa wimbo huo lakini kwa shinikizo la mama yake mzazi alifanya. Kwenye mahojiano na HipHop DX, Thug ameeleza kwamba hakuamini kama wimbo huo ungefanya vizuri kutokana na kuwa havikua vitu vyake lakini anafurahishwa kuona amekuwa moja ya watu walioshiriki katika wimbo huo ambao umetunukiwa tuzo maalumu ya Diamond na RIAA.

Read More