Diana Marua Ajitenga na Mwelekeo Mpya wa Muziki wa Bahati

Diana Marua Ajitenga na Mwelekeo Mpya wa Muziki wa Bahati

Mke wa msanii Bahati, Diana Marua, ameibua gumzo mtandaoni baada ya kujitenga wazi na mwelekeo mpya wa muziki wa mumewe unaohusisha maudhui yanayodaiwa kwenda kinyume na maadili ya jamii. Kupitia taarifa yake kwa mashabiki, Diana amesema anatambua na anaheshimu safari ya Bahati kama msanii na maamuzi anayochukua kwa ajili ya taaluma yake, lakini akasisitiza kuwa mtazamo wake binafsi ni tofauti. Ameeleza kuwa amejikita zaidi katika biashara, ushirikiano wa kibiashara na chapa zinazomwamini, hivyo lazima aendelee kujiwasilisha kwa njia inayoonyesha uwajibikaji, ukuaji na thamani anazoamini. Aidha, Diana ameongeza kuwa kwa heshima ya familia yake, washirika wake kibiashara na wale wanaomchukulia kama kielelezo, hatahusika na mwelekeo ambao Bahati amechukua katika muziki wake. Amesisitiza kuwa anaamini katika kupeana sapoti, lakini pia ni muhimu kulinda chapa yake na nafasi ambazo ameendelea kujenga katika tasnia ya burudani. Diana ametoa kauli hiyo baada ya Bahati kuachia wimbo wake mpya Seti, ujio wake wa kwanza tangu arejee kwenye muziki baada ya mapumziko, ambao hata hivyo umekosolewa vikali kutokana na maudhui yake yanayohamasisha ngono.

Read More
 Diana Bahati Aonyesha Utajiri wake Wakati Mumewe Akikumbwa na Kashfa

Diana Bahati Aonyesha Utajiri wake Wakati Mumewe Akikumbwa na Kashfa

Mke wa msanii Bahati, Diana Marua maarufu kama Diana B, amewajibu kimkakati wanaozidi kumbeza mume wake Bahati ambaye anahusishwa na kashfa ya kushindwa kutimiza ahadi yake ya kutoa KSh1 milioni kwa timu ya taifa, Harambee Stars. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diana alionekana akijivunia shopping ya mwezi mmoja iliyogharimu takribani KSh160,000. Bidhaa alizonunua zilijumuisha vyakula, bidhaa za nyumbani na mahitaji mengine ya familia yake. Hata hivyo, kilichowashangaza wengi ni pale alipoweka wazi wingi wa pesa taslimu alizokuwa nazo nyumbani. Diana alionekana akishika mirundo ya noti za KSh1,000, ambazo alidai zinafikia jumla ya KSh2 milioni. Wakati mashabiki wengine wakivutiwa na maisha ya kifahari anayoyaonesha, wengi walishangaa hatua yake ya kuonyesha kiasi kikubwa cha fedha hadharani, hasa ikizingatiwa kwamba Bahati anatupiwa lawama kwa kukosa kutimiza ahadi yake ya kifedha kwa wachezaji wa Harambee Stars baada ya ushindi wao mkubwa kwenye mashindano ya CHAN 2024. Mashabiki mtandaoni wamehoji uhalisia wa pesa hizo, wengine wakisema huenda ilikuwa njia ya Diana kutafuta kiki na kutetea hadhi ya kifamilia wakati jina la Bahati linatikiswa na shinikizo la mashabiki na wanamichezo.

Read More
 DIANA B AFUNGUKA KUHUSU UKIMYA WA MUME WAKE BAHATI

DIANA B AFUNGUKA KUHUSU UKIMYA WA MUME WAKE BAHATI

Mwanamuziki na mtayarishaji wa maudhui nchini Diana Bahati, amemkingia kifua mumewe Kevin Bahati, kwa madai ya kutotumia akaunti yake ya Instagram kwa muda mrefu. Akimjibu shabiki yake aliyetaka kufahamu kiini cha ukimya wa hitmaker huyo wa ngoma Adhiambo diana b kupitia ukurasa wake wa Instagram amesema ukimya wa bahati umetokana na msanii huyo kujikita zaidi kwenye masuala ya kifamilia kwani anatumia muda wake mwingi na watoto wake. Hapo awali, Bahati, alikuwa akiwafahamisha mashabiki wake kuhusu matukio yanayotokea kwenye maisha yake, huku akichapisha maudhui mengi kwenye ukurasa wake ndani ya siku moja. Kwa sasa, ukurasa wa Bahati hauna maudhui mapya tangu alipolia hadharani wiki mbili zilizopita kuhusu masaibu yake ya kisiasa, mara baada ya chama cha jubilee kumpokonya tiketiya kuwania ubunge wa mathare kwenye uchaguzi wa Agosti 9 mwaka huu. Tangu wakati huo, mwanamuziki huyo hajachapishaa kitu chochote kipya kwenye mitandao yake ya kijamii akiwaacha mashabiki zake njia panda.

Read More
 DIANA BAHATI AMTAMBULISHA MSANII WAKE MPYA CHINI LEBO YA MUZIKI YA DIANA B ENTERTAINMENT

DIANA BAHATI AMTAMBULISHA MSANII WAKE MPYA CHINI LEBO YA MUZIKI YA DIANA B ENTERTAINMENT

Mwanamitandao aliyegeukia muziki nchini Diana Bahati amemtambulisha msanii wake mpya wake mpya anayekwenda kwa jina la Vinny fleva. Kupitia ukurasa wake wa instagram Diana B amesema vinny flava atakuwa chini ya lebo yake ya muziki ya Diana B Entertainment ambayo itasimamia kazi zake zote za muziki huku akiwataka mashabiki zake wamkaribishe msanii huyo  ambayo kwa mujibu wake anakuja kubadilisha tasnia ya muziki nchini Kenya. Hata hivyo walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wameonekana kutofauti kimawazo na diana b ambapo wengi wamehoji amemuiga staa wa muziki nchini Nadia Mukami ambaye juzi kati alimtambulisha msanii wake aitwaye Latinoh chini lebo yake ya Sevens Hub Creative. Tayari Diana B ameachia wimbo wake mpya uitwao “Mubaba” ambao amemshirikisha msanii wake vinny fleva. Wimbo huo ni watatu kwa Diana B tangu aanze career yake ya muziki baada ya one day na Tuachana tu ambazo aliziachia mwishoni mwaka wa 2021.

Read More