Diana B Awaacha Mashabiki Midomo Wazi kwa Matumizi ya Nyumbani ya Zaidi ya KES 119,000
Malkia wa mitandao ya kijamii, Diana B, ameonyesha kwa vitendo namna anavyotumia kwa busara pesa anazozikeshea na kuzitolea jasho kupitia kazi zake mbalimbali. Mkali huyo wa “Bibi ya Tajiri” amewaacha mashabiki wengi vinywa wazi baada ya kufichua kiasi kikubwa cha fedha alichotumia kwa ununuzi wa bidhaa za matumizi ya nyumbani kwa mwezi wa Januari. Kupitia Instastory yake, Diana B ameshare risiti ya manunuzi inayoonyesha alitumia jumla ya KES 119,009 kununua bidhaa mbalimbali za matumizi ya kila siku nyumbani. Hatua hiyo imekuja katika kipindi ambacho Wakenya wengi wanapitia changamoto za kiuchumi, hasa mwezi wa Januari unaojulikana kwa mzigo mkubwa wa karo za shule na mahitaji mengine.
Read More