Mtangazaji Dr. Ofweneke Aahirisha Tamasha la Isukuti Baada ya Madai ya Fitina

Mtangazaji Dr. Ofweneke Aahirisha Tamasha la Isukuti Baada ya Madai ya Fitina

Mtangazaji maarufu Dr. Ofweneke ametangaza kuahirisha tamasha lake la Isukuti, lililokuwa limekusudiwa kuileta pamoja jamii ya Waluhya. Kupitia mitandao yake ya kijamii, Ofweneke amesema ameafikia uamuzi huo baada ya madai kuwa kuna watu wanaomsingizia kwamba anahujumu juhudi za kuimarisha mshikamano wa jamii hiyo. Amesisitiza kwamba lengo lake kuu lilikuwa ni kutumia tamasha hilo kama jukwaa la kuunganisha jamii, na siyo kuibua mgawanyiko. Ameomba wafuasi wake kuwa na subira hadi atakapotangaza tarehe mpya ya kurejea kwa tamasha hilo, akieleza kuwa kwa sasa anatoa nafasi kwa maandalizi ya matamasha makubwa ambayo yatasaidia kuonyesha mshikamano wa jamii ya Luhya. Tamasha la Isukuti lililopangwa na Ofweneke lilikuwa limepewa uzito mkubwa kutokana na nafasi yake katika kukuza urithi wa jamii ya Luhya. Hata hivyo, kuahirishwa kwake kumefungua mjadala mpana kuhusu changamoto za umoja miongoni mwa jamii mbalimbali nchini Kenya. Kauli ya Ofweneke imejiri siku chache baada ya mchekeshaji Eddie Butita kutoa changamoto kwa waandaaji wa matamasha ya kitamaduni ya jamii wa Luhya, akiwataka kuungana badala ya kusambaratika katika matamasha madogo. Butita alitolea mfano tamasha kubwa la jamii ya Luo, ambalo limekuwa likitambulika kama moja ya hafla kubwa na zenye ushawishi nchini Kenya..

Read More
 Dr. Ofweneke apata kigugumizi baada ya kuitishwa millioni 70 kumleta Burna Boy Kenya

Dr. Ofweneke apata kigugumizi baada ya kuitishwa millioni 70 kumleta Burna Boy Kenya

Mchekeshaji Dr. Ofweneke ameshangazwa na kiasi cha pesa alichotakiwa kulipa kwa ajili ya kumleta Burna Boy kutumbuiza nchini Kenya. Kupitia ukurasa wa Instagram Ofweneke amesema uongozi wa Burna Boy kupitia mama yake mzazi Bose Ogulu ulimtaka alipe kiasi cha shillingi millioni 70 kumpata msanii huyo kutumbuiza kwenye mkesha wa kukaribisha mwaka mpya wa 2023. “Weeh tried reaching out to the mum for a new year’s event … he is now charging Ksh 70 M,” alisema Dr. Ofweneke. Hata hivyo kauli hiyo imezua mjadala mzito miongoni watumiaji wa mitandao ya kijamii wengi wakitamtaka mchekeshaji huyo kuwapa nafasi wasanii wa Kenya kwenye onesho lake lijalo badala ya kuwazingatiwa wasanii wa nje ambao watamtoza kiasi kikubwa cha pesa.

Read More
 DR. OFWENEKE AKANUSHA KUWA KWENYE UGOMVI NA AKOTHEE

DR. OFWENEKE AKANUSHA KUWA KWENYE UGOMVI NA AKOTHEE

Mchekeshaji Dr. Ofweneke amekanusha kuwa kwenye bifu na Akothee baada ya kumtaka mwimbaji huyo amlipe shilllingi millioni 1.4 ili awe mshereheshaji(MC) kwenye hafla ya harusi yake. Kwenye mahojiano na Mpasho Ofweneke amesema hana ugomvi na mwanamama huyo wa watoto 5 kama namna watu wanavyohoji kwenye mitandao ya kijamii kwani ni marafiki wakubwa. Mchekeshaji huyo amesema ana imani kuwa Akothee ana uwezo mkubwa wa kumlipa pesa hizo kwani bado wapo kwenye mchakato wa kukamilisha mazungumzo kati yao.

Read More