Dyana Cods Aomba Radhi kwa Mashabiki Wake Kufuatia Kauli Zake Kuhusu Rais William Ruto

Dyana Cods Aomba Radhi kwa Mashabiki Wake Kufuatia Kauli Zake Kuhusu Rais William Ruto

Msanii wa muziki wa rap nchini Kenya, Dyana Cods, ameomba msamaha hadharani kwa mashabiki wake kufuatia kauli zake za awali ambapo alionekana kuunga mkono Rais William Ruto. Taarifa hiyo ya msamaha iliitoa jukwaani kupitia video inayosambaa kwa kasi mitandaoni, ambapo Dyana alionekana akipiga magoti kwa hisia kubwa baada ya kumaliza kutumbuiza. Katika tukio hilo lililogusa hisia za wengi, Dyana alionesha majuto usoni mwake huku akiwatupia mashabiki wake maneno ya upendo na shukrani kwa kuwa upande wake licha ya makosa aliyoyafanya. Alisisitiza kuwa anawaweka mashabiki wake mbele kuliko kiongozi yeyote wa kisiasa, na kwamba anajali sana hisia zao. Msamaha huu unajiri baada ya hitmaker huyo wa ngoma ya “Set It” kushutumiwa mitandaoni kwa kauli zake za awali alizotoa akiwakosoa Wakenya kwa kumkosoa Rais Ruto kwa kushindwa kutekeleza ahadi aliyoitoa kwa wananchi. Kauli hiyo ilizua hisia kali, huku wengi wakimtuhumu kwa kujaribu kuhalalisha hali ngumu ya maisha nchini. Baadaye, Dyana alijitetea akisema alikuwa anatania. Tukio hili limeibua maoni tofauti mitandaoni, huku mashabiki wengine wakimsifu kwa ujasiri wa kukiri makosa yake, huku wengine wakimtaka awe makini zaidi na kauli zake hasa zinapohusisha masuala ya kisiasa yanayogusa hisia za wananchi wengi.

Read More
 Dyana Cods Atangaza Ujio wa Albamu Yake Mpya “Ghetto Story”

Dyana Cods Atangaza Ujio wa Albamu Yake Mpya “Ghetto Story”

Hitmaker wa ngoma ya “Set It”, Msanii Dyana Cods, ametangaza ujio wa albamu yake ya nne kwa jina Ghetto Story, hatua iliyowaacha mashabiki wake na hamu kubwa ya kusikia kazi hiyo mpya. Kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, Dyana alipakia mfululizo wa picha za kisanii na kusindikiza kwa maneno mafupi yenye uzito yaliyosomeka “#GhettoStory 4th album coming soon.” Ingawa mrembo huyo hakuweka wazi tarehe rasmi ya kuachia albamu hiyo, ujumbe huo umeibua mjadala na matarajio makubwa kutoka kwa mashabiki na wadau wa muziki, wengi wakitarajia kazi iliyojaa maudhui ya maisha halisi na uhalisia wa mitaani kama jina la albamu linavyoashiria. Albamu hii inatarajiwa kuwa mwendelezo wa mafanikio ya Dyana Cods katika muziki wa Kenya, huku wengi wakisubiri kuona ushirikiano mpya, ujumbe mzito, na ladha mpya ya kipekee inayotambulika kwa mtindo wake. Ikumbukwe kwamba Dyana Cods tayari ameachia albamu tatu tangu aanze safari yake ya muziki, ambazo ni THANK ME LATER (2022), River Lake Nilote (2023), na Rong Manners (2024).

Read More
 Msanii Dyana Cods Afunguka Baada ya Lawama za Kuunga Mkono Serikali

Msanii Dyana Cods Afunguka Baada ya Lawama za Kuunga Mkono Serikali

Mwanamuziki wa Kenya na mwimbaji wa wimbo maarufu “Set It”, Dyana Cods, ameomba msamaha kwa mashabiki wake kufuatia malalamiko yaliyotokana na kauli zake zilizotafsiriwa kuwa za kuiunga mkono serikali. Katika ujumbe alioutoa kupitia mitandao ya kijamii, Dyana alieleza kuwa kauli zake zilikuwa za kejeli (sarcastic) na hazikupaswa kuchukuliwa kwa uzito kama wengi walivyofanya. Alisema hakuwa na nia ya kuonyesha uungwaji mkono kwa hatua zozote za serikali zinazokera wananchi. “Ninaomba radhi kwa yeyote aliyekasirishwa na kile nilichosema. Hiyo haikuwa kauli ya kweli bali ni kejeli tu, watu hawakuelewa muktadha,” alisema Dyana katika taarifa yake. Kauli hiyo inakuja wakati ambapo wananchi wengi wamekuwa wakitoa hisia kali dhidi ya baadhi ya viongozi na sera za serikali, hasa kupitia mitandao ya kijamii. Kwa hivyo, mashabiki walichukulia kauli ya Dyana kwa uzito mkubwa, wakihisi ameipuuza hali halisi ya maisha yanayowakabili Wakenya. Baadhi ya mashabiki walimtaka afafanue msimamo wake, huku wengine wakimtaka kuwa makini na maudhui anayochapisha, hasa kwa kuwa ana ushawishi mkubwa kwa vijana. Hata hivyo, baada ya kutoa ufafanuzi huo, mashabiki wengine walionekana kumwelewa na kupongeza hatua yake ya kukiri na kujieleza kwa uwazi, wakisema kila mtu anaweza kueleweka vibaya mitandaoni. Dyana Cods, ambaye amepata umaarufu mkubwa kupitia vibao vyake vya Arbantone, amesisitiza kuwa anaelewa machungu ya wananchi na hana nia ya kudhihaki hali ya maisha au kuunga mkono dhuluma ya kisera.

Read More
 Dyana Cods Awasha Moto Mitandaoni Baada ya Kutuma Ksh 90,000 kwa Mpenzi Wake

Dyana Cods Awasha Moto Mitandaoni Baada ya Kutuma Ksh 90,000 kwa Mpenzi Wake

Mwanamuziki kutoka nchini Kenya anayevuma na kibao chake “Set It”, Dyana Cods, ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kuchapisha picha ya skrini inayoonyesha kwamba alimtumia mpenzi wake Ksh 90,000 kama ishara ya upendo. Kupitia Insta Story yake, Dyana alitoa ujumbe wenye nguvu kwa wanawake, akisisitiza kuwa mapenzi ni ya pande zote, na kwamba wanaume pia wanastahili kutunzwa na kupendwa kwa vitendo.  “Si lazima kila wakati iwe wanaume ndio wanatoa. Wapeni pia. Mkiwapenda, wapeni. Wakijituma, waletee zawadi. Wakinyamaza, shika simu uliza kama wako sawa.” Ujumbe huu umezua mjadala mkubwa kuhusu nafasi ya wanawake katika mahusiano ya kisasa, hasa katika jamii ambayo mara nyingi huwatarajia wanaume kuwa watoa zawadi na msaada wa kifedha. Wengi walimsifu kwa kuonyesha mfano wa mapenzi yanayoegemea usawa na kujali kwa pande zote mbili. Hata hivyo, baadhi ya mashabiki walihoji ujumbe wake kwa kuzingatia hali ya maisha ya watu wa kawaida:  “Sisi wengine hatuna hata ya kulipia Wi-Fi, alafu wewe unatuma elfu tisini,” aliandika mtumiaji mmoja wa X (zamani Twitter). Lakini kuna waliotetea msimamo wake, wakisema ni wakati wanawake waache kusubiri kupokea tu na waanze kuchangia pia pale wanapopenda. Mbali na kuwa mwanamuziki mwenye kipaji, Dyana Cods amejipatia umaarufu kupitia mitandao ya kijamii kwa mtindo wake wa maisha wa kipekee, misimamo ya moja kwa moja kuhusu mapenzi, na kujiamini kisanaa. Wimbo wake Set It ulichangia pakubwa kumtambulisha katika muziki wa Kenya, na sasa anaendelea kujijenga kama sauti ya kizazi kipya cha wasanii wanaoelezea maisha yao kwa uhuru – iwe ni kupitia muziki au mitandao.

Read More