Eddie Butita Avunja Kiapo Cha Kutovalia Pyjama Inayofanana na Mpenzi Wake

Eddie Butita Avunja Kiapo Cha Kutovalia Pyjama Inayofanana na Mpenzi Wake

Mchekeshaji kutoka Kenya Eddie Butita amejipata njia panda baada ya kushiriki picha pamoja na mpenzi wake Cele Terer wakiwa wamevalia Pyjamas mfanano ikiwa ni miaka miwili imepita tangu akashifu vikali kitendo hicho kama ushamba uliopitiza. Kupitia Instagram, Butita alichapisha misururu ya picha maridadi kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa na mpenzi wake Cele, wakiwa wamepiga pozi za kimahaba kando ya mti wa Krismasi uliopambwa. Wawili hao walionekana wakiwa na furaha tele, huku wote wakiwa wamevalia pyjamas za Krismasi zenye muundo mmoja. Furaha hiyo ya Butita ilidumu kwa muda mfupi kabla ya walimwengu wenye kumbukumbu kali kufufua kauli yake ya Disemba 25, mwaka 2025. Katika video hiyo iliyosambazwa sana, Butita alikiri mbele ya mashabiki wake kuwa hatowahi kamwe kuvalia mavazi yanayofanana na mpenzi wake kisha akapost mitandaoni. Butita alisema kitendo hicho ni ushamba ambapo alienda mbali zaidi akawataka mashabiki wamweka kwa maombi ili asije kuvunja kiapo chake na kukufuru alichokitamka. Kufufuka kwa video hiyo imeashiria wazi kwamba mchekeshaji huyo hatimaye amezidiwa na nguvu ya mahaba, na hivyo kujisalimisha kwenye mahitaji ya mpenzi wake Celest Terer. Wengi wamechukulia hili kama uthibitisho wa msemo kwamba mapenzi hayana kiapo, na kwamba hata watu wenye msimamo mkali wanaweza kubadilika wanapokuwa kwenye uhusiano.

Read More
 Eddie Butita Aonekana Hadharani na Mpenzi Mpya Celeste Katika Uzinduzi wa Albamu ya Okello Max

Eddie Butita Aonekana Hadharani na Mpenzi Mpya Celeste Katika Uzinduzi wa Albamu ya Okello Max

Mchekeshaji na mtayarishaji maarufu kutoka Kenya, Eddie Butita, ameibua gumzo mitandaoni baada ya kuonekana kwa mara ya kwanza hadharani akiwa karibu na mpenzi wake mpya, Celeste, katika hafla ya uzinduzi wa albamu ya msanii Okello Max iliyofanyika usiku wa jana katika ukumbi wa Mass House, jijini Nairobi. Butita na Celeste walionekana wakiwa pamoja kwa karibu muda wote wa hafla hiyo, wakionyesha ishara wazi za mapenzi. Walionekana wakicheka, kushikana mikono na kufurahia burudani kwa pamoja huku wakipigwa picha na waandishi wa habari na mashabiki waliokuwepo ukumbini. Picha na video za wawili hao zimesambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii, na kuibua mjadala miongoni mwa mashabiki ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakijiuliza kuhusu maisha ya mahusiano ya Butita. Hii ni kutokana na ukweli kwamba hajawahi kuthibitisha wazi uhusiano na Celeste, licha ya tetesi ambazo zimekuwepo kwa muda. Hafla hiyo ya burudani, iliyohudhuriwa na wasanii wakubwa na wadau mbalimbali wa tasnia ya muziki, iliendelea kuwa ya kipekee huku Butita na Celeste wakionekana kuwa na wakati mzuri pamoja, jambo lililothibitisha kuwa huenda wawili hao sasa wako tayari kuonyesha uhusiano wao hadharani. Wakati mashabiki wakisubiri kauli rasmi kutoka kwa Butita au Celeste, tukio hilo limeashiria mwanzo mpya katika maisha ya kimapenzi ya Butita, na wengi wamepongeza hatua hiyo mpya wakisema inafurahisha kuwaona wakifurahia maisha pamoja. Kwa sasa, Butita na Celeste wameingia rasmi kwenye orodha ya wanandoa wapya maarufu katika jiji la Nairobi, na mashabiki wanaendelea kufuatilia kwa karibu kila hatua ya safari yao ya mapenzi.

Read More