Eko Dydda Atetea Gospel ya Kisasa kwa Kuwapuuza Wakosoaji

Eko Dydda Atetea Gospel ya Kisasa kwa Kuwapuuza Wakosoaji

Msanii wa muziki wa injili kutoka Kenya, Eko Dydda, amewatolea uvivu wanaoendelea kukosoa mtindo wake mpya wa muziki wa Injili, akisisitiza kuwa hatabadilisha msimamo wake wala imani yake kwa sababu ya maneno ya watu. Kupitia ujumbe wake uliosambaa mitandaoni, Eko Dydda amewataka wanaobeza muziki wake kupeleka lawama zao kwingine, akisema wazi kuwa hafanyi muziki kuwaridhisha wanadamu bali anamtumikia Mungu. Msanii huyo ameeleza kuwa kila kizazi kina njia yake ya kumtukuza Mungu, na kwamba muziki wake unalenga kuwafikia vijana wa kizazi cha sasa kwa lugha na sauti wanazoelewa. Amesisitiza kuwa mtindo hauondoi ujumbe, bali ni njia tu ya kuufikisha kwa hadhira pana zaidi. Eko Dydda amekuwa akitambulika kwa kuvaa mavazi ya kisasa, kutumia meno ya grills na kuwasilisha ujumbe wake kwa vijana kupitia lugha ya mtaani ya sheng. Mtindo ambao umeibua hisia mseto miongoni mw watu wanaodai kwamba msanii huyo huenda amepoteza mwelekeo kwa kuiga mitindo ya wasanii wa kidunia.

Read More
 EKO DYDDA AWAPA SOMO VIJANA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA AGOSTI 9

EKO DYDDA AWAPA SOMO VIJANA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA AGOSTI 9

Wakati joto la uchaguzi mkuu likizidi kupanda katika maeneo mengi nchini,mwanamuziki aliyegeukia siasa Eko Dydda amewataka vijana kuwa makini na viongozi wanaotoa rushwa, kwa ajili ya kuwashawishi kuchagua upya kwenye uchaguzi wa Agosti 9. Katika mahojiano na mpasho Eko Dydda ametoa changamoto kwa vijana kuwa na dhamira ya dhati kuwakataa wagombea watakaojaribu kuiendekeza rushwa wakati huu wa kampeini kwani ni njia ya kuwapofusha macho na matokeo yake ni taifa kupata viongozi wasiofaa. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Vidole” amekiri kwamba upungufu wa uadilifu miongoni mwa watu wengi nchini unatokana na tatizo la rushwa ambalo pia ni miongoni mwa changamoto kubwa dhidi ya amani, utulivu na mshikamano. Hata hivyo amewahimiza wakenya kutowachagua viongozi kwa misingi ya vyama vya kisiasa na badala yake kuwachagua viongozi wenye maono ya maendeleo na watakaojali maslahi yao. Utakumbuka Eko Dydda anawania wadhfa wa uwakilishi wadi ya Mathare kaskazini kwenye uchaguzi mkuu ujao kama mgombea uhuru.

Read More
 EKO DYDDA ATANGAZA KUWANIA WADHFA WA UWAKILISHI WADI MATHARE KASKAZINI KWENYE UCHAGUZI MKUU 2022

EKO DYDDA ATANGAZA KUWANIA WADHFA WA UWAKILISHI WADI MATHARE KASKAZINI KWENYE UCHAGUZI MKUU 2022

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini Eko Dydda ametia nia ya kugombea uwakilishi wadi ya Mathare Kaskazini kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022. Kupitia ukurasa wake wa instagram  hitmaker huyo wa “Niko na Reason” amesema kuwa amesukumwa kugombea kiti cha uwakilishi wadi wa eneo hilo kutokana na kero ambazo vijana wamekutana nazo kwenye suala la kusaka ajira. Aidha amesema ni muda wa vijana kuwania nyadhafi za uongozi  kwani viongozi waliochaguliwa wamefeli kutekeleza ahadi walizozitoa kwa wananchi. Hata hivyo ametoa changamoto kwa vijana kujisajili kama wapiga kura ili waweze kuleta mabadiliko katika maeneo ambayo wanatoka kwa kuwachagua viongozi wawajibikaji kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Eko dydda ni moja kati ya wasanii ambao wamekuwa wakishinikiza kumaliza ukabili miongoni mwa wakenya kwani mwaka wa 2015 aliacha kutumia jina la ukoo wake na akaanza kutumia Eko Dydda kama jina lake rasmi.

Read More