EKO DYDDA AWAPA SOMO VIJANA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA AGOSTI 9

EKO DYDDA AWAPA SOMO VIJANA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA AGOSTI 9

Wakati joto la uchaguzi mkuu likizidi kupanda katika maeneo mengi nchini,mwanamuziki aliyegeukia siasa Eko Dydda amewataka vijana kuwa makini na viongozi wanaotoa rushwa, kwa ajili ya kuwashawishi kuchagua upya kwenye uchaguzi wa Agosti 9. Katika mahojiano na mpasho Eko Dydda ametoa changamoto kwa vijana kuwa na dhamira ya dhati kuwakataa wagombea watakaojaribu kuiendekeza rushwa wakati huu wa kampeini kwani ni njia ya kuwapofusha macho na matokeo yake ni taifa kupata viongozi wasiofaa. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Vidole” amekiri kwamba upungufu wa uadilifu miongoni mwa watu wengi nchini unatokana na tatizo la rushwa ambalo pia ni miongoni mwa changamoto kubwa dhidi ya amani, utulivu na mshikamano. Hata hivyo amewahimiza wakenya kutowachagua viongozi kwa misingi ya vyama vya kisiasa na badala yake kuwachagua viongozi wenye maono ya maendeleo na watakaojali maslahi yao. Utakumbuka Eko Dydda anawania wadhfa wa uwakilishi wadi ya Mathare kaskazini kwenye uchaguzi mkuu ujao kama mgombea uhuru.

Read More
 EKO DYDDA ATANGAZA KUWANIA WADHFA WA UWAKILISHI WADI MATHARE KASKAZINI KWENYE UCHAGUZI MKUU 2022

EKO DYDDA ATANGAZA KUWANIA WADHFA WA UWAKILISHI WADI MATHARE KASKAZINI KWENYE UCHAGUZI MKUU 2022

Mwanamuziki wa nyimbo za injili nchini Eko Dydda ametia nia ya kugombea uwakilishi wadi ya Mathare Kaskazini kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2022. Kupitia ukurasa wake wa instagram  hitmaker huyo wa “Niko na Reason” amesema kuwa amesukumwa kugombea kiti cha uwakilishi wadi wa eneo hilo kutokana na kero ambazo vijana wamekutana nazo kwenye suala la kusaka ajira. Aidha amesema ni muda wa vijana kuwania nyadhafi za uongozi  kwani viongozi waliochaguliwa wamefeli kutekeleza ahadi walizozitoa kwa wananchi. Hata hivyo ametoa changamoto kwa vijana kujisajili kama wapiga kura ili waweze kuleta mabadiliko katika maeneo ambayo wanatoka kwa kuwachagua viongozi wawajibikaji kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Eko dydda ni moja kati ya wasanii ambao wamekuwa wakishinikiza kumaliza ukabili miongoni mwa wakenya kwani mwaka wa 2015 aliacha kutumia jina la ukoo wake na akaanza kutumia Eko Dydda kama jina lake rasmi.

Read More