Otile Brown Aumizwa na Habari za Ndoa ya Nabayet, Aandika Ujumbe wa Hisia Kali

Otile Brown Aumizwa na Habari za Ndoa ya Nabayet, Aandika Ujumbe wa Hisia Kali

Mwanamuziki wa Bongo R&B kutoka Kenya, Otile Brown, ameibua hisia mtandaoni baada ya kuonyesha maumivu na mshangao kufuatia habari za aliyekuwa mpenzi wake, Nabayet kutoka Ethiopia, kufunga ndoa. Kupitia Insta Story yake, Otile alionekana kushindwa kuficha hisia zake, hasa kwa kuwa alimtaja Nabayet katika wimbo wake mpya unaotarajiwa kuachiwa. Ameandika:  “How does she go & get married after mentioning her on my new song dropping tomorrow… now I feel dueh…”,  Otile aliandika hisia nyingi Maneno hayo yameibua hisia mseto mitandaoni, huku mashabiki wake wakimfariji na wengine wakihisi kwamba bado ana hisia kwa mrembo huyo. Uhusiano wa Otile Brown na Nabayet ulikuwa wa muda mrefu na wa hadharani, uliovutia mashabiki wengi kutoka Afrika Mashariki na Ethiopia. Wawili hao walionekana kuwa na mahusiano yenye upendo mkubwa kabla ya kuachana kimya kimya miaka michache iliyopita. Kabla ya habari za ndoa ya Nabayet, Otile alikuwa ameonekana kuendelea na maisha, lakini ujumbe huu mpya unaonyesha pengine bado kuna hisia zilizobaki. Mashabiki sasa wanasubiri kwa hamu wimbo mpya wa Otile Brown ili kusikia alivyomzungumzia Nabayet, huku wengi wakijiuliza kama hii itaathiri maudhui au hisia za kazi hiyo.

Read More
 Nabayet, Mpenzi wa Zamani wa Otile Brown, Afunga Ndoa Kwenye Harusi ya Kifahari Ethiopia

Nabayet, Mpenzi wa Zamani wa Otile Brown, Afunga Ndoa Kwenye Harusi ya Kifahari Ethiopia

Mwanamitindo maarufu kutoka Ethiopia,Nabayet, ambaye aliwahi kuwa mpenzi wa msanii nyota wa Kenya Otile Brown, ameaga rasmi maisha ya u-single baada ya kufunga ndoa kwenye harusi ya kifahari iliyofanyika nchini mwake mwishoni mwa wiki. Harusi hiyo, iliyohudhuriwa na familia, marafiki wa karibu na watu mashuhuri kutoka sekta ya mitindo na burudani, ilifanyika katika hoteli ya kifahari jijini Addis Ababa. Nabayet alionekana mrembo kupindukia akiwa amevalia gauni jeupe la harusi lililobuniwa na mbunifu maarufu wa mitindo wa Ethiopia. Video na picha za tukio hilo zimeenea kwenye mitandao ya kijamii, huku mashabiki wakimpongeza kwa hatua hiyo mpya katika maisha yake. Ingawa hakufichua jina la mchumba wake, mashabiki walionekana kushangilia penzi jipya la mrembo huyo ambaye amekuwa akipunguza sana kuweka maisha yake ya kimapenzi hadharani. Nabayet aliingia kwenye uhusiano wa kimapenzi na Otile Brown mwaka 2019, na wawili hao walivutia mashabiki wengi kwa mahusiano yao ya kuvutia yaliyokuwa yakisambazwa kupitia mitandao ya kijamii. Hata hivyo, uhusiano huo uliisha baada ya muda kutokana na tofauti zao za kimtazamo. Otile Brown bado hajatoa kauli rasmi kuhusu harusi hiyo ya mpenzi wake wa zamani. Mashabiki wa Nabayet wameendelea kumpongeza kwa hatua hiyo kubwa, wakimtakia heri katika maisha mapya ya ndoa.

Read More