Eve Mungai Aumizwa na Taarifa za Mrembo wa Ex Wake Trevor Kupata Uja Uzito

Eve Mungai Aumizwa na Taarifa za Mrembo wa Ex Wake Trevor Kupata Uja Uzito

Youtuber maarufu mtandaoni, Eve Mungai, ameonekana kuumizwa na taarifa za mpenzi wake wa zamani, Director Trevor, kuthibitisha kuwa anatarajia mtoto na mrembo wake wa sasa anayejulikana kama Kiki Love. Eve, kupitia mitandao yake, aliandika ujumbe ulioonekana kuashiria kwamba hana furaha kubwa na taarifa hiyo, akisema kuwa โ€œsio wa kwanza kupata uja uzito.โ€ Kauli hiyo imeibua tafsiri tofauti kwa mashabiki wake, wengi wakihisi kwamba inaweza kuwa ishara ya machungu au hisia za wivu kwa hatua ya maisha ya ex wake licha ya kujaribu kujionyesha mwenye nguvu mbele ya umma. Hii inajiri baada ya Trevor mwenyewe kuthibitisha habari za ujauzito wa mrembo wake kupitia mitandao ya kijamii, akishare picha na ujumbe wa furaha akitangaza kuwa yeye na Kiki wanatarajia mtoto wao wa kwanza. Alienda mbali zaidi na kuwataka wafuasi wake wampendekezee majina watakayompa mtoto wao.

Read More
 Eve Mungai Afunguka Kuhusu Mapambano ya Afya ya Akili

Eve Mungai Afunguka Kuhusu Mapambano ya Afya ya Akili

Mwanahabari wa kidijitali na mtayarishaji wa maudhui, Eve Mungai, amefunguka kuhusu maisha yake ya ndani kwa mara ya kwanza baada ya kipindi kigumu alichopitia mwaka huu. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Eve ameeleza kwamba kati ya mwezi Aprili na Juni, alipitia kipindi cha msongo wa mawazo (depression) kikali kilichomfanya kutumia muda mwingi kitandani, kushindwa kula ipasavyo, na kuhisi amelemewa na maisha. Mrembo huyo, amekiri kuwa maombi, msaada wa familia, marafiki wa karibu na utafutaji wa msaada kitaalamu vilimsaidia hatua kwa hatua kurejea kwenye hali ya kawaida na kupona. Akizungumzia maisha yake ya kibinafsi, Eve Mungai pia amethibitisha kwamba kwa sasa yupo single, na kufutilia mbali tetesi kuhusu maisha yake ya mahusiano. Kuhusu hatua yake ya kujiondoa kwenye mahojiano ya mastaa na podcast, Eve amesema baada ya miaka mitano ya kufanya kazi hiyo bila kupumzika, alihisi kuchoka kwa kuwa alikuwa akifukuza ndoto za watu wengine badala ya kuwekeza kwenye ndoto zake binafsi.

Read More
 Mwanablogu Eve Mungai Aapa Kuwaanika Wanaume Wanaomtumia Picha Chafu

Mwanablogu Eve Mungai Aapa Kuwaanika Wanaume Wanaomtumia Picha Chafu

Mwanablogu na mshawishi maarufu wa mitandao ya kijamii nchini Kenya, Eve Mungai, ameapa kuchukua hatua kali dhidi ya wanaume walio katika ndoa wanaomtumia picha zisizofaa kupitia jumbe za moja kwa moja (DMs) kwenye mitandao yake ya kijamii. Kupitia chapisho kali kwenye Instagram Stories, Eve alionyesha kuchoshwa na tabia ya baadhi ya wanaume waliooa kumtumia maudhui ya matusi na picha za ngono, akisema kuwa wakati umefika wa kuanika majina yao hadharani. โ€œWanaume waliooa, mna wake zenu halafu bado mnanitumia picha za ajabu kwenye DM? Msidhani mtatulia! Saa imefika ya kuwaanika,โ€ aliandika Eve kwa hasira. Eve Mungai, ambaye amejijengea jina kwa maudhui ya kijamii na mahojiano ya kuvutia na watu mashuhuri, aliongeza kuwa vitendo hivyo si tu vya kukosa heshima bali pia vinadhalilisha wake wa wanaume hao. Alisema kuwa wanawake wengi hawajui wanachoendelea nyuma ya pazia, na kama njia ya kupambana na tabia hizo, ataanza kuwataja wahusika kwa majina. Kauli yake imezua mjadala mkali mitandaoni, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa kusimama kidete kupinga udhalilishaji wa kingono, huku wengine wakimtaka kuwa na subira na kushughulikia suala hilo kwa njia ya binafsi.

Read More