Fetty Wap Aachiwa Huru Baada ya Miaka 3 Gerezani
Rapa wa Marekani Fetty Wap ameachiwa huru baada ya kutumikia zaidi ya miaka mitatu gerezani, hatua ambayo imepokelewa kwa hisia mseto miongoni mwa mashabiki wake na wadau wa muziki duniani. Kwa mujibu wa majarida mbali mbali nchini Marekani, Fetty Wap, ameachiwa mapema leo kutoka gerezani alikokuwa akitumikia kifungo cha miaka sita kwa kosa la kuhusika katika mtandao wa usambazaji wa dawa za kulevya. Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Fetty Wap ameonyesha shukrani za dhati kwa familia, marafiki na mashabiki waliomsimamia kwa maombi na upendo wakati wote akiwa gerezani. Aidha, ameahidi kutumia uzoefu wake kama funzo na kujikita katika kusaidia jamii, hususan watoto na vijana walioko katika mazingira magumu. Ameonyesha nia ya kuunga mkono miradi ya elimu, teknolojia na huduma za afya kama njia ya kurudisha mkono kwa jamii. Fetty Wap kwa sasa yupo chini ya uangalizi mkali wa kisheria (home confinement) hadi Novemba 2026, ambapo atalazimika kufuata masharti kadhaa ikiwemo kutohusishwa na dawa za kulevya, kuripoti mienendo yake kwa mamlaka husika na kudhibiti shughuli zake za kifedha.
Read More