HARMONIZE AMVISHA PETE YA UCHUMBA KAJALA MASANJA

HARMONIZE AMVISHA PETE YA UCHUMBA KAJALA MASANJA

Msanii wa Bongofleva Harmonize amemvisha pete ya uchumba Mwigizaji Kajala Masanja ikiwa ni siku chache toka wawili hao warudiane baada ya penzi lao kuvunjika kipindi cha nyuma. Tukio hilo limefanyika Jumamosi Juni 25,mwaka 2022  katika hoteli ya Serena huku likihudhuriwa na watu wa karibu wa wasanii hao ukiwemo uongozi wa lebo ya Konde Gang. Wakati wa tukio hili Harmonize amekiri kwamba Kajala ni Mwanamke bora kwake na kuna wakati Kajala alimpa hifadhi kwenye nyumba yake wakati Harmonize akiwa hana nyumba. Harmonize na Kajala wamechumbiana ikiwa ni takribani mwaka mmoja tangu walipotengana baada ya mwanamuziki huyo kumfungulia mashtaka Kajala na binti yake Paula akiwatuhumu kuvujisha picha zake za utupu

Read More
 FRIDAH KAJALA ATAMBULISHWA KAMA MENEJA WA HARMONIZE

FRIDAH KAJALA ATAMBULISHWA KAMA MENEJA WA HARMONIZE

Ni Rasmi sasa mwanadada Fridah Kajala ni meneja wa Lebo ya Konde Music Worldwide. Kajala ameongezeka kwenye uongozi wa Konde music ikiwa ni tamanio la Harmonize ambaye ndiye CEO wa lebo hiyo, kumtaka asimamie biashara yake ya Muziki. Kajala ametangazwa rasmi na Choppa_ambaye ni mmoja wa mameneja wa Harmonize, kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika; “Allow Me To Welcome In Management Team New C.E.O And Manager Kajala Frida I’m Excited To Work With You Shem #kondegang4you“. Naye Harmonize alishusha comment kwenye posti hiyo yenye maneno yanayosomeka; “Big Team, Big Dream” huku Kajala akiachia emoji za moto na kuonyoosha mikono juu. Utakumbuka, Harmonize kabla hajarudiana na mpenzi wake Kajala, aliwahi kusema kwamba anatamani siku moja akirudiana na mrembo huyo, awe meneja wake.

Read More