Huddah Monroe Ashukuru Wakili Aliyemsaidia Kurekebisha Meno Yake

Huddah Monroe Ashukuru Wakili Aliyemsaidia Kurekebisha Meno Yake

Mrembo maarufu katika mitandao ya kijamii, Huddah Monroe, ameonyesha shukrani zake kwa wakili mmoja wa Kenya aliyemsaidia kurejesha tabasamu lake kwa kumsaidia kifedha. Kupitia Instastory, Huddah amefichua kuwa wakili huyo alimpatia shilingi milioni 2, fedha zilizotumika kurekebisha meno yake yaliyokuwa yameharibika baada ya kuhusika kwenye ajali akiwa bado msichana mdogo. Akizungumza kuhusu safari yake ya maisha, Huddah amesema alikulia katika mazingira ya umaskini, hali iliyowafanya wazazi wake kushindwa kumhudumia kwa matibabu ya meno. Upungufu huo ulimfanya kukumbwa na changamoto kubwa shuleni, ambapo wenzake walimchekelea kwa kukosa meno ya juu (front teeth).. Kwa sasa, Huddah anasema msaada huo umempa nguvu mpya na kuondoa majeraha ya kisaikolojia aliyobeba kwa miaka mingi. Amepongeza wakili huyo kwa moyo wa kujitolea na kuonyesha kuwa msaada wa kijamii unaweza kubadilisha maisha ya mtu kwa kiwango kikubwa.

Read More
 Huddah Monroe Afunguka Namna Marehemu Silas Jirongo Alivyombadilisha Maisha Yake

Huddah Monroe Afunguka Namna Marehemu Silas Jirongo Alivyombadilisha Maisha Yake

Socialite kutoka Kenya Huddah Monroe amefunguka kwa hisia kali kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge nchini humo, marehemu Cyrus Jirongo, akieleza namna alivyomsaidia kifedha kwa kiasi kikubwa na kumtoa kwenye hali ngumu ya maisha. Kupitia ujumbe wake wa rambirambi aliouchapisha mitandaoni, Huddah amesema msaada wa Jirongo ulikuwa wa kipekee na wa kubadilisha maisha, akisisitiza kuwa ni mmoja wa watu wachache waliomsaidia bila masharti. Katika ujumbe huo, Huddah amesema kuwa mara nyingi kumekuwepo na dhana kwamba watu wa jamii ya Waluhya hawatoi pesa, lakini kwa upande wake Jirongo alimthibitishia kinyume chake kwa vitendo. Huddah amesema msaada alioupata kutoka kwa Jirongo ulimtoa kabisa kwenye lindi la umaskini, hatua ambayo ilimfungulia ukurasa mpya wa maisha na mafanikio aliyofikia leo. Kifo cha Cyrus Jirongo kimetokea mapema jana baada ya kuhusika katika ajali mbaya ya barabarani kwenye barabara kuu ya Nakuru–Nairobi, tukio lililoshtua taifa la Kenya na kuacha majonzi makubwa kwa familia, marafiki na watu waliowahi kuguswa na ukarimu wake.

Read More
 Socialite Huddah Monroe Asema Hataki Watoto Maishani Mwake  

Socialite Huddah Monroe Asema Hataki Watoto Maishani Mwake  

Socialite na mfanyabiashara maarufu nchini Kenya, Huddah Monroe, amezua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kueleza wazi msimamo wake kuhusu suala la kupata watoto. Kupitia InstaStory, Huddah amesema hakuna kitu chochote duniani kinachoweza kumshawishi kujifungua au kuzaa mtoto. Amesisitiza kuwa uamuzi huo ni wa binafsi na haupaswi kuingiliwa na mtu yeyote. Huddah ameweka wazi kuwa hana shida na watu wengine wanaochagua kupata watoto wengi, akisema kila mtu ana haki ya kuishi maisha anayoyachagua bila kuhukumiwa. Hata hivyo, Huddah Monroe amesisitiza kuwa anaishi maisha yake kwa masharti yake mwenyewe na hataki kushinikizwa kufuata matarajio ya jamii kuhusu uzazi.

Read More
 Huddah Monroe Azua Tetesi za Mahusiano na  Rapa Rick Ross

Huddah Monroe Azua Tetesi za Mahusiano na Rapa Rick Ross

Rapper wa Marekani Rick Ross ameibua gumzo jipya la tetesi za kimapenzi na sosholaiti wa Kenya Huddah Monroe baada ya kutuma ujumbe wa faragha uliodhihirisha ukaribu wao. Huddah, kupitia ukurasa wake wa Instagram, ameshare screenshot ya mazungumzo yao na kuandika ujumbe ulioashiria kujisalimisha kwake kwa mapenzi ya msanii huyo. Katika maelezo yake, Huddah amesisitiza kuwa yuko tayari kumfuata Rick Ross kwa chochote anachotaka, akimtaja kuwa ndiye mwenye mamlaka na uongozi katika mawasiliano yao. Maneno aliyoyaweka yalionesha wazi namna anavyomuona msanii huyo kama mtu muhimu kwake na namna anavyompa kipaumbele katika maisha yake ya kimtandao. Hatua hiyo imewafanya wengi kuamini kuwa wawili hao huenda wako katika hatua za mwanzo za uhusiano. Mashabiki mitandaoni wamekuwa na maoni mseto, baadhi wakisema wawili hao wamekuwa na ukaribu kwa muda mrefu, huku wengine wakidai huenda ni maandalizi ya promo au mradi mpya utakaowahusisha.

Read More
 Huddah Monroe Akosoa Kampuni za Ulinzi Kenya

Huddah Monroe Akosoa Kampuni za Ulinzi Kenya

Mjasiriamali na mshawishi wa mitandaoni, Huddah Monroe, ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kukosoa kampuni za ulinzi nchini Kenya kwa kuendelea kuwapa wanawake, wakiwemo single mothers, zamu za usiku. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Huddah ametaja kuwa ni jambo lisilo la kawaida kwa wanawake kupewa zamu za usiku wakati wanahitajika zaidi nyumbani kwa ajili ya watoto wao. Huddah amesema kuwa watoto, hasa wa umri mdogo, wanahitaji uwepo na uangalizi wa mama zao wakati wa usiku kwa sababu ndiyo muda ambao wengi wanapata usalama wa kihisia, mwongozo na utulivu. Ameongeza kuwa kampuni zinazotoa ratiba hizo hazizingatii changamoto za single mothers, ambao mara nyingi hawana mtu wa kubadilishana majukumu nao nyumbani. Mrembo huyo hata hivyo ametoa changamoto kwa kampuni za ulinzi nchini Kenya kuunda mwongozo utakaowaruhusu wanawake kupata mapumziko wakati wa usiku, kwani ratiba za kazi za usiku huathiri ustawi wa familia.

Read More
 Huddah Monroe Awakashif Wanaume wa Kenya kwa Kukosa Heshima Kwa Wanawake

Huddah Monroe Awakashif Wanaume wa Kenya kwa Kukosa Heshima Kwa Wanawake

Mjasiriamali na socialite maarufu, Huddah Monroe, ameibua mjadala mtandaoni baada ya kutoa matamshi makali akiwakosoa baadhi ya wanaume wa Kenya kwa kile alichokiita tabia ya kuwadhalilisha na kutowaheshimu wanawake. Kupitia ujumbe aliouchapisha mtandaoni, Huddah amesema hataki tena kuzungumza au kujihusisha na wanaume wa “millennials”, akiwataja kama kizazi kisichoheshimu wanawake na kinachopenda kutumia maneno ya dharau. Amesema kuwa kulingana na uzoefu wake, wanaume wa kizazi hicho mara nyingi hukosa adabu wanapowasiliana na wanawake. Huddah ameongeza kuwa anaona afadhali kuzungumza na kizazi kipya cha Gen Z, akisema kuwa angalau wao wanaonyesha viwango vya juu vya heshima na ustaarabu linapokuja suala la kuwasiliana na wanawake. Kauli hiyo imekuja muda mfupi baada ya Huddah kufunguka kupitia Insta story yake kuhusu tukio alilodai lilimtokea katika moja ya hoteli ya kifahari jijini Nairobi, ambapo mwanaume alimfuata kwa njia aliyoiita isiyo na heshima, na kujaribu kumtongoza bila staha.

Read More
 Huddah Aanikwa Mtandaoni kwa Kutorejesha Mkopo wa Milioni 6

Huddah Aanikwa Mtandaoni kwa Kutorejesha Mkopo wa Milioni 6

Mfanyabiashara anayejiita Madollar Mapesa, amezua gumzo baada ya kuweka wazi kwamba anamdai mrembo na mfanyabiashara, Huddah Monroe, shilingi milioni 6 za Kenya. Kupitia Instagram yake, mkopo huo ulitolewa kupitia meneja wake na ulitarajiwa kurejeshwa kwa wakati, lakini hadi sasa haujalipwa. Mapesa amesema kwamba mara nyingi huwa anawasaidia watu wengi kupata mikopo mikubwa kwa masharti nafuu kuliko benki au taasisi nyingine za kifedha, akisisitiza kuwa amewaokoa wengi dhidi ya kupoteza mali na biashara zao kwa sababu ya minada. Hata hivyo, amesema licha ya ukarimu huo, baadhi ya watu maarufu wamekuwa wakikosa kuheshimu makubaliano ya kurejesha mikopo kwa wakati. Madollar ameonya kuwa ana ushahidi wa kutosha kuthibitisha madai yake endapo Huddah atakanusha. Pia ametuma ujumbe kwa wadaiwa wengine anaowadai akiwataka kulipa kabla hajaanza kampeni za kuwataja majina hadharani. Taarifa hizi zimechochea mjadala mkubwa mitandaoni, ambapo baadhi ya mashabiki wanamtaka Huddah kujitokeza na kueleza ukweli, huku wengine wakipuuza madai ya Mapesa wakiyataja kama mbinu ya kutafuta umaarufu.

Read More
 Huddah Monroe Apandisha Bei ya Lunch Date Hadi KSh 150,000

Huddah Monroe Apandisha Bei ya Lunch Date Hadi KSh 150,000

Sosholaiti na mfanyabiashara maarufu wa Kenya, Huddah Monroe, ameibua mjadala mitandaoni baada ya kupandisha bei ya ofa yake ya lunch date kutoka KSh 50,000 hadi KSh 150,000. Hatua hiyo inadaiwa kuchochewa na uhitaji mkubwa kutoka kwa mashabiki wanaotaka kukutana naye. Kupitia tangazo lake, Huddah alisema mpango huo unalenga kutoa nafasi kwa mashabiki wake waliotamani muda mrefu kupata muda wa ana kwa ana naye. Aidha, alidai kuwa malipo hayo yamekuwa mengi kiasi cha kufanya akaunti yake ya M-Pesa kufurika. Awali, Huddah alikuwa ameeleza kuwa gharama ya lunch date ilikuwa KSh 50,000, lakini sasa imeongezwa mara tatu. Vilevile, aliongeza kuwa kwa mtu anayetaka kuwa rafiki wake wa karibu, atatakiwa kulipia kiasi cha KSh 1 milioni. Tangazo hilo limeendelea kuvutia hisia mseto, mashabiki wengine wakimpongeza kwa kuthamini muda wake, huku wengine wakipinga bei hizo wakiziona kama kupita kiasi.

Read More
 Huddah Atoa Vigezo vya Kukutana Naye, Asema Urafiki Ni Shillingi Milioni 1

Huddah Atoa Vigezo vya Kukutana Naye, Asema Urafiki Ni Shillingi Milioni 1

Sosholaiti wa Kenya, Huddah Monroe, ametangaza masharti mapya kwa mashabiki wanaotamani kukutana naye ana kwa ana. Kwa mujibu wa mpango huo, atatoza Sh50,000 kwa chakula cha mchana cha saa mbili, ambapo saa moja ya ziada imetengwa kwa ajili ya picha na mazungumzo ya kawaida. Hata hivyo, gharama ya chakula haitajumuishwa na mahali pa kukutana patachaguliwa na mhusika mwenyewe. Huddah ameliita zoezi hili “The Bachelorette,” akieleza kuwa ni nafasi ya kipekee kwa mashabiki kupata muda wake. Ameweka msimamo kuwa hawezi kutoa muda wake bure kwani anauchukulia kama wa thamani, na kwamba kuwa naye kunahitaji gharama. Mbali na chakula cha mchana, Huddah pia amedokeza uwezekano wa kushirikiana na mashabiki wake kwenye shughuli nyingine za burudani kama michezo, iwapo watakuwa tayari. Amesema nafasi za kuhudhuria zitafunguliwa rasmi kuanzia Jumanne wiki ijayo. Katika kujibu shabiki mmoja aliyeuliza kuhusu urafiki, Huddah amesisitiza kuwa hata kuwa rafiki naye ni gharama kubwa, akitaja kiwango cha Sh1 milioni kama ada ya urafiki, akisema muda wake binafsi ni wa thamani na haupatikani kirahisi.

Read More
 Colonel Mustafa Adai Kuwasaidia Huddah na Noti Flow Kufikia Umaarufu

Colonel Mustafa Adai Kuwasaidia Huddah na Noti Flow Kufikia Umaarufu

Msanii mkongwe wa muziki nchini Kenya,Colonel Mustafa, amezua gumzo mitandaoni baada ya kudai kuwa muda aliowahi kutumia na mastaa wa kike kama Huddah Monroe na Noti Flow uliwasaidia kupenya kwenye anga la umaarufu, wakati walipokuwa bado hawajatambulika sana katika tasnia ya burudani. Akizungumza kwenye podcast ya Alex Mwakideu Live, alisema kwamba mahusiano yake na wanawake hao yalimsaidia kuwapa mwanga wa mafanikio waliokuwa bado hawajaufikia kwa wakati huo. Kwa mujibu wa msanii huyo, jina lake lilihusishwa na mastaa hao kabla ya wao kung’aa, na hivyo mchango wake haupaswi kupuuzwa. Kauli hiyo imeibua hisia mseto mitandaoni. Wapo wanaoamini kuwa Mustafa alikuwa sehemu ya safari ya mafanikio ya Huddah na Noti Flow, huku wengine wakimtuhumu kwa kujitafutia kiki na kutumia majina ya watu maarufu kurudi kwenye ramani ya burudani. Hadi sasa, Huddah Monroe na Noti Flow hawajajibu madai hayo, lakini mashabiki wanazidi kufuatilia kwa makini endapo wahusika watajitokeza kuweka wazi upande wao wa simulizi hii. Mustafa, anayekumbukwa kwa kazi zake akiwa na kundi la Deux Vultures, anaonekana kurejea tena kwenye vyombo vya habari si kwa muziki, bali kwa matamshi yenye utata kuhusu mahusiano ya zamani.

Read More
 Huddah Monroe Ataka Roboti Badala ya Watu, Alalamikia Uzembe Kazini

Huddah Monroe Ataka Roboti Badala ya Watu, Alalamikia Uzembe Kazini

Mjasiriamali na mwanasosholaiti maarufu wa Kenya, Huddah Monroe, ameibua mjadala mkali mitandaoni baada ya kulalamikia wafanyakazi wake kwa kile alichokitaja kama kukosa akili ya kawaida (common sense) katika kushughulikia mambo madogo kazini. Katika ujumbe wake uliojaa malalamiko na kejeli kupitia InstaStory, Huddah alieleza kukerwa na kile alichokiita uzembe na ukosefu wa ufanisi, kutoka kwa wafanyakazi wa ngazi ya juu hadi chini. Alisisitiza kuwa hana tatizo na kazi kubwa, bali ni mambo madogo kama usafi na uangalifu wa mazingira ambayo yanamvunja moyo zaidi. “Nina timu nzima, lakini hakuna anayefikiria kuondoa maua yaliyoanza kuoza mezani. Nitafungua duka la kwanza la roboti Kenya!, Nahitaji clone (nakala yangu) kwa sababu timu yangu haiwezi hata kushughulikia mambo madogo,” aliandika Huddah, akionyesha wazi kutoridhika na utendaji wa kikosi chake cha sasa. Kauli hiyo imezua hisia mseto kutoka kwa mashabiki na wafuasi wake, baadhi wakimuunga mkono kwa kutaka nidhamu kazini, huku wengine wakimkosoa kwa lugha ya ukali dhidi ya wafanyakazi wake. Wapo pia waliodokeza kuwa kauli yake inaonyesha shinikizo kubwa analokumbana nalo katika kuendesha biashara. Huddah, anayejulikana kwa ujasiriamali wake na uwazi katika mitandao ya kijamii, amekuwa mstari wa mbele kukuza bidhaa za urembo chini ya chapa ya Huddah Cosmetics, na pia hujulikana kwa mtindo wake wa maisha wa kifahari. Hadi sasa, hajatoa taarifa nyingine kufuatia malalamiko hayo, lakini ujumbe wake umeonyesha wazi kuwa anataka mabadiliko ya haraka katika timu yake – au roboti wachukue usukani.

Read More
 Huddah Monroe: Wanaume wa Gen Z Hawana Ujasiri wa Kuwatongoza Wanawake

Huddah Monroe: Wanaume wa Gen Z Hawana Ujasiri wa Kuwatongoza Wanawake

Mfanyabiashara na mwanasosholaiti maarufu kutoka Kenya, Huddah Monroe, amezua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kutoa kauli yenye utata kuhusu wanaume wa kizazi cha Gen Z. Kupitia mitandao ya kijamii, Huddah alisema kuwa wanaume wa kizazi hiki wamekosa ujasiri wa kutangamana na wanawake na kuanzisha mazungumzo, tofauti kabisa na enzi za Millennials. Huddah alieleza kushangazwa na tabia ya wanaume wa kizazi cha Gen Z ambao, kwa mtazamo wake, huonekana kuogopa au kutojihusisha moja kwa moja na wanawake katika mazingira ya kijamii.  “Navaa ninja yangu na kwenda sehemu za kijamii kwa ajili ya utafiti wangu tu, maana sina ninayemtaka huko. Lakini wanaume hawakaribii wanawake,” aliandika Huddah. Huddah aliendelea kueleza kuwa hali hiyo imemfanya awahurumie wanaume wa kizazi hiki kwa sababu mawasiliano ya ana kwa ana yamepungua sana. Kwa maoni yake, kizazi cha sasa kinaonekana kuwa na uwoga au labda kimezidiwa na matumizi ya mitandao ya kijamii, kiasi cha kushindwa kuwa na ujasiri wa kawaida wa kuanzisha mazungumzo. “Millennials walikuwa na game. Gen Z wanaonekana kama wamekata tamaa. Wengine wakijaribu, mazungumzo yao hayana ladha wala mvuto,” aliongeza. Kauli hii imechochea maoni mbalimbali, huku baadhi ya mashabiki wakimpongeza kwa kusema anasema ukweli mchungu. Wengine wamehusisha hali hiyo na mabadiliko ya kijamii, hofu ya kukataliwa, au ongezeko la mtazamo hasi dhidi ya wanaume wanaowakaribia wanawake bila mwaliko. Huddah, ambaye ana sauti kubwa mitandaoni kuhusu masuala ya kijamii, anasema hali hii inaweza kuwa ishara ya matatizo makubwa zaidi katika namna watu wa kizazi kipya wanavyojenga mahusiano.

Read More