Jackie Chandiru afunguka kutonufaika na Rehab

Jackie Chandiru afunguka kutonufaika na Rehab

Hitmaker wa “Gold Digger”, Msanii Jackie Chandiru amedai kwamba kituo cha matibabu ya watumiaji wa madawa, pombe na mihadarati haikuwahi kumsaidia kuondokana na uraibu wa dawa za kulevya. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni amesema hamkatishi tamaa mtu yeyote anayetamani kwenda Rehab ila kwa upande wake hali yake ya kiafya ilidorora zaidi alipokuwa chini ya uangalizi wa kituo hicho. Chandiru ametoa kauli hiyo alipoulizwa kutoa maoni yake kama King Saha atanufaika na uangalizi wa kituo cha matibabu ya watumiaji wa madawa za kulevya Utakumbukwa mapema wiki iliyopitwa msanii King Saha alikimbizwa hospitali baada ya kuugua ugonjwa unaodaiwa kusababishwa na uraibu wake wa kutumia mihadarati. Lakini habari njema kwa mashabiki zake ni kwamba madaktari walimruhusu kwenda nyumbani baada ya kupata nafuu.

Read More
 JACKIE CHANDIRU AFUNGUKA CHANZO CHA BLU3 KUVUNJIKA

JACKIE CHANDIRU AFUNGUKA CHANZO CHA BLU3 KUVUNJIKA

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Jackie Chandiru amefunguka sababu za kuvunjika kwa kundi la Blue 3. Katika mahojiano yake hivi karibuni Chandiru amesema ugomvi wa kila mara kati yake na Cindy Sanyu ndio chanzo cha kundi hilo kuvunjika, jambo ambalo liliwafanya wasanii wa kundi hilo kuchukua maamuzi ya kufanya muziki kama wasanii wa kujitegemea. Msanii huyo amesema iwapo wangetatua tofauti zao na Cindy mapema kundi la Blue 3 lingekuwa bado linaendelea harakati zake za kuwaburudisha mashabiki. Hata hivyo amesema hana chuki dhidi ya msanii mwenzake Cindy Sanyu huku akisisitiza kuwa anaamini kuna kipindi watakuja kufanya kazi pamoja kama kundi. Blue3 ni kundi la muziki kutoka uganda ambalo lilikuwa linaundwa na wasanii watatu ambao Jackie Chandiru, Cindy Sanyu na Lilian  Mbambazi. Kundi hilo lilianza muziki mwaka wa 2004 baada ya kushinda tuzo ya Coca Cola Popstars Mwaka 2003 na lilivunjika rasmi mwaka wa 2009 baada ya kufanya vizuri kwenye tasnia ya muziki Afrika Mashariki.

Read More
 JACKIE CHANDIRU ASUSIA UCHAGUZI WA UMA KISA CINDY SANYU

JACKIE CHANDIRU ASUSIA UCHAGUZI WA UMA KISA CINDY SANYU

Mwanamuziki Jackie Chandiru amefichua kuwa kuna uwezekano hatoshiriki katika uchaguzi ujao wa Chama cha Wanamuziki nchini Uganda (UMA) licha ya member wa zamani wa kundi la Blue3, Cindy Sanyu kugombea urais katika chama hicho. Chandiru anasema anamuunga mkono Cindy lakini amehamua kukaa mbali na uchaguzi huo kutokana na manyanyaso aliyokumbana nayo alipokuwa chini ya kundi la Blue 3 ambalo lilikuwa linaongozwa na Cindy Sanyu. “Shuleni kuna mtu nilimuunga mkono lakini alipokua kiongozi wa darasa alianza kunionea. Sipendi kupiga kura kwa sababu watu hufanya kinyume na kile wanachoahaidi,” amesema kwa mafumbo kwenye moja ya mahojiano yake nchini Uganda. Chandiru, hata hivyo, amesema Cindy ana sifa zote za kuwaongoza wanamuziki  nchini Uganda kupitia chama hicho ila hatopiga kura. Ujumbe huo umetafsiri na walimwengu kuwa msanii huyo bado ana machungu na Cindy ambaye walikuwa wanaunda kundi la Blue 3 ambalo lilifanya vizuri kwenye muziki nchini Uganda kati ya mwaka wa 2003 na 2008.

Read More
 JACKIE CHANDIRU: WAGANDA WANA ROHO CHAFU,WALINITUSI HADI NIKAHAMIA KENYA

JACKIE CHANDIRU: WAGANDA WANA ROHO CHAFU,WALINITUSI HADI NIKAHAMIA KENYA

Aliyekuwa msanii wa kundi la Blue 3 kutoka Uganda Jackie Chandiru amefunguka juu ya changamoto alizokutana nazo wakati alikuwa ameathirika na uraibu wa dawa za kulevya. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni, Chandiru amesema Waganda hawakumpa muda wa kupona kutoka kwa uraibu wa mihadarati kwani kila mara walikuwa wanamkosoa badala ya kumpa msaada. Hitmaker huyo wa “Gold Digger amesema kipindi picha zake zilifuja mtandaoni akiwa hali mbaya, alipokea matusi ya kila aina kutoka kwa Waganda jambo ambalo anadai lilimlazimu kutimkia nchini Kenya. “Waganda hawakunipa nafasi ya kupona, walipoona picha zangu nikiwa katika hali ya kutisha, walinitusi, na hali yangu ikawa mbaya zaidi. Ndio maana nimekaa muda mwingi nchini Kenya,” alisema. Chandiru hata hivyo anasema ataendelea kuishukuru familia yake na marafiki ambao walifanya kila wawezalo kumuona akifurahia maisha tena.

Read More