Jackie Chandiru afunguka kutonufaika na Rehab
Hitmaker wa “Gold Digger”, Msanii Jackie Chandiru amedai kwamba kituo cha matibabu ya watumiaji wa madawa, pombe na mihadarati haikuwahi kumsaidia kuondokana na uraibu wa dawa za kulevya. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni amesema hamkatishi tamaa mtu yeyote anayetamani kwenda Rehab ila kwa upande wake hali yake ya kiafya ilidorora zaidi alipokuwa chini ya uangalizi wa kituo hicho. Chandiru ametoa kauli hiyo alipoulizwa kutoa maoni yake kama King Saha atanufaika na uangalizi wa kituo cha matibabu ya watumiaji wa madawa za kulevya Utakumbukwa mapema wiki iliyopitwa msanii King Saha alikimbizwa hospitali baada ya kuugua ugonjwa unaodaiwa kusababishwa na uraibu wake wa kutumia mihadarati. Lakini habari njema kwa mashabiki zake ni kwamba madaktari walimruhusu kwenda nyumbani baada ya kupata nafuu.
Read More