Jay Melody Amtishia Mtu Aliyemvunjia Heshima: Siku Moja Utaishia Jela!”

Jay Melody Amtishia Mtu Aliyemvunjia Heshima: Siku Moja Utaishia Jela!”

Msanii wa Bongo Fleva, Jay Melody, ameacha mashabiki wake wakibaki na maswali baada ya kuandika ujumbe wa mafumbo kwenye Insta Story yake, hatua iliyozua mjadala mkubwa mitandaoni. Katika ujumbe huo, Jay Melody ameandika kwa mtindo wa onyo akimtahadharisha mtu ambaye hakumtaja moja kwa moja kwamba endapo ataendelea na tabia zake za usela anaweza kujikuta matatani na hata jela. Hitmaker huyo wa Mtoto ameongeza kuwa mtu huyo mara kwa mara huonekana akileta miyeyusho na kushindwa kuaminika, hali inayomfanya aonekane kama chizi machoni pa watu. Jay Melody pia amesisitiza kwamba siku moja mtu huyo ataingia katika matatizo makubwa na kuishia kujuta kwa matendo yake. Ujumbe huo uliachwa bila maelezo zaidi, jambo lililoacha mashabiki wake wakijiuliza kama msanii huyo alikuwa anamwandikia mtu maalum au alikuwa akizungumza kwa ujumla kuhusu maisha na tabia za baadhi ya watu. Mashabiki kadhaa mitandaoni wameonyesha hisia tofauti, wengine wakichukulia kama ujumbe wa mafundisho, huku wengine wakihisi huenda ni dongo lililotumwa kwa mtu maarufu.

Read More
 Msanii wa Bongo Fleva Jay Melody atangaza kukamilisha albamu yake mpya

Msanii wa Bongo Fleva Jay Melody atangaza kukamilisha albamu yake mpya

Msanii wa Bongo Fleva, Jay Melody, ametangaza kukamilisha albamu yake mpya, ikiwa ni taktibani mwaka mmoja tangu alipoachia albamu yake ya kwanza Therapy Aprili 26, mwaka 2024. Kupitia InstaStory kwenye mtandao wa Instagram, Jay Melody aliwafahamisha mashabiki wake kuwa albamu hiyo mpya ipo tayari, huku akiwaahidi nyimbo kuanza kusikika muda wowote kuanzia sasa. Hii inazidisha matarajio miongoni kwa mashabiki wake waliounga mkono kazi zake tangu mwanzo. Bado hajataja jina la albamu hiyo mpya wala orodha kamili ya nyimbo, lakini matarajio ni makubwa ikizingatiwa mafanikio ya Therapy ambayo ilijumuisha nyimbo zilizotamba kwenye chati mbalimbali. Mashabiki wanasubiri kwa hamu kusikia ladha mpya kutoka kwa hitmaker huyu wa Sawa.

Read More
 Jay Melody aukataa wimbo wake

Jay Melody aukataa wimbo wake

Mwanamuziki wa Bongofleva Jay Melody ambaye hivi karibuni ameachia wimbo wake wa miondoko ya Amapiano “Acha Wivu “ameamua kufuta post zote kwenye ukurasa wake wa Instagram zinazohusiana na wimbo huo. Mpaka sasa haijafamika sababu za Jay Melody kufuta post za wimbo huo japo stori za chini ya kapeti zinadai kuwa ni kutokana na wimbo huo kutopata mapokezi mazuri ukilinganisha na nyimbo za nyuma alizoziachia Mpaka sasa wimbo huo umesikikizwa na watu 59,000 kupitia mtandao wa YouTube

Read More
 JAY MELODY AWEKA HISTORIA NA WIMBO WAKE “NAKUPENDA”

JAY MELODY AWEKA HISTORIA NA WIMBO WAKE “NAKUPENDA”

Staa wa muziki wa Bongofleva Jay melody anazidi kufanya vizuri kupitia mauzo ya mtandaoni na wimbo wake “Nakupenda” ambayo tayari ina takriban wiki tatu tangu itoke rasmi. Habari njema kwa mashabiki wa Jay Melody, ni kwamba ngoma yake “Nakupenda”, imefanikiwa kufikisha jumla ya streams Milioni 10 ndani ya digital platforms zote ambazo wimbo huo umepandishwa. Wimbo huo ambao bado hauna video, na kwenye Shazam unakamata nafasi ya 2 kwenye kipengele cha Afrobeats na ya 82 Worldwide. Itakumbukwa, “Nakupenda” ni wimbo wa tatu kwa Jay Melody kuachia mwaka huu, baada ya “Sugar” pamoja na Remix yake.

Read More
 JAY MELODY AFUNGUKA KUMTAKA KIMAPENZI PAULA

JAY MELODY AFUNGUKA KUMTAKA KIMAPENZI PAULA

Hit Maker wa Nakupenda, msanii Jay Melody amefunguka juu ya hisia zake kwa Paula Kajala. Hii imekuja baada ya kumpost Mrembo huyo kwenye Ukurasa wake wa Instagram na Kuifuta baada ya Muda. Akiwa kwenye kipindi cha Refresh cha Wasafi TV ametolea ufafanuzi mpaka kupost picha ya Mrembo huyo na baAdae kuifuta hakuwa na nia mbaya kwa Paula kwani alikuwa anamuonyesha upendo wa kawaida. “Mimi therealpaulahkajala Nampenda kama watu wengine ninavyowapenda naziona picha zake nzuri ndio maana nikaamua kumpost lakini nilichokiandika havihusiani na picha yake ndio maana nilitanguliza picha yangu. Hakuna ubaya katika hilo. “Hakuna mtu yoyote alienicheki lakini picha niliifuta baada ya kuona Coment zimekuwa Nyingi hadi wajomba zake nikaona sina haja ya kumtengenezea mtoto wa watu Mawazo nikaona ni bora niifute” Amesema Jay Melody.

Read More
 JAY MELODY AKIRI KUCHOSHWA NA SHUGHULI YA UANDISHI NYIMBO

JAY MELODY AKIRI KUCHOSHWA NA SHUGHULI YA UANDISHI NYIMBO

Msanii wa Bongofleva Jay Melody amesema hatokuja kumuandikia msanii mwenzake wimbo wowote kwa kuwa kipindi cha nyuma hakufaidi na chochote kwenye shughuli ya uandishi ya nyimbo. Katika mahojiano yake hivi karibuni Jay Melody amesema kwa sasa ameelekeza nguvu zake zote kwenye suala la kujiandikia nyimbo zake mwenyewe kama njia ya kutanua wigo wa muziki wake huwafikia watu wengi duniani. Lakini pia Hitmaker huyo wa “Sugar” amewataka mashabiki waache utimu kwenye muziki kwa kuwa inarudisha nyuma juhudi za wasanii kuupeleka muziki wa Bongofleva kimataifa. Kwa sasa Jay Melody anafanya vizuri na ngoma yake mpya inaitwa “Nakupande”.

Read More
 JAY MELODY MBIONI KUACHIA ALBUM YAKE MPYA

JAY MELODY MBIONI KUACHIA ALBUM YAKE MPYA

Msanii wa Bongofleva, Jay Melody amesema albamu yake mpya ambayo ipo mbioni kutoka itakuwa na ngoma 15. Akizungumza na kipindi cha The Switch ya Wasafi FM,hitmaker huyo wa ngoma ya “Sugar” amesema albamu hiyo aliipanga kuiachia mwaka jana lakini akasogeza mbele ili kujipanga vizuri. Mbali na hayo, Jay Melody amesema ataachia video ya wimbo wake wa ‘Sugar’ remix aliyomshirikisha Marioo hivi karibuni kwani tayari wamemaliza kushuti video ya wimbo huo. Utakumbuka Jay Melody anakuwa msanii mwingine kuweka wazi kutoa albamu mwaka huu baada ya Navy Kenzo, Harmonize, Ommy Dimpoz, Marioo, Maua Sama na Zuchu.

Read More