VDJ Jones akanusha kuwakandamiza wasanii wa Jeshi Jinga

VDJ Jones akanusha kuwakandamiza wasanii wa Jeshi Jinga

Bosi wa lebo ya muziki ya Superstar Entertainment VDJ Jones amefunguka kuhusu madai ya kuvunja kundi la muziki wa Gengtone Jeshi Jinga. Kwenye mahojiano na Nicholas Kioko amesema madai ya kuinyanyasa kundi hilo kifedha hayana ukweli wowote huku akisema kuwa wasanii wa Jeshi Jinga wenyewe walishindwa kuachia muziki muzuri licha ya kutumia nguvu nyingi kuwatoa kisanaa. VDJ Jones amesema hajutii suala la kusitisha mkataba wa kufanya kazi na wasanii wa kundi hilo kwani walifeli kurudisha shillingi milioni mbili alizowekeza kwenye muziki wao. Sanjari na hilo amemkingia kifua mchekeshaji Eric Omondi kwa kusema kuwa mchekeshaji huyo anaiwazia mazuri tasnia ya muziki nchini Kenya ila wasanii wamefeli kumuunga mkono kwenye harakati za kuleta mabadiliko. Hata hivyo amewataka wasanii wa Kenya waache masuala ya kujihusisha sana na matukio yasiyokuwa na tija kwenye mitandao ya kijamii badala yake waachie nyimbo kali kama namna ambavyo wasanii wa Nigeria na Tanzania wanavyofanya.

Read More
 WASANII WA JESHI JINGA WAMVUA NGUO KRG THE DON KWA KUKOSOA LUGHA YAO YA SHENG

WASANII WA JESHI JINGA WAMVUA NGUO KRG THE DON KWA KUKOSOA LUGHA YAO YA SHENG

Wasanii wa Jeshi Jinga wamemtolea uvivu KRG The Don kwa madai ya kukosoa lugha yao ya Sheng ambayo walibuni hivi majuzi. Katika mahojiano yao hivi karibuni wasanii hao wamemtaka KRG The Don aache kuwaingilia wakiwa kwenye harakati  zao za kuja na lugha mpya itakayowaunganisha watu duniani kwani msanii huyo anatumia suala hilo kutafuta kiki. Aidha wamesema sheng yao mpya inakidhi vigezo vyote vya kuwa lugha rasmi kwani wamekuwa wakiifanyia kazi lugha hiyo kwa muda mrefu ambapo wamekanusha madai ya kutumia mihadarati kwa kusema kwamba madai hayo hayana msingi wowote kwa sababu wao ni watu wanajiheshimu sana. Wasanii hao wameenda mbali na kuwachana baadhi ya wasanii ambao wameanza kutumia lugha hiyo kwa shughuli zao za kisanaa kwa kuwataka waheishimu kama lugha zingine badala ya  kutoa nyimbo ambazo hazina mashiko kwenye jamii. Hata hivyo Jeshi Jinga wamedokeza ujio wa album yao mpya ambayo tayari wameanza kufanyia kazi huku wakiwataka mashabiki wakae mkao wa kula kupokea ngoma yao mpya itakayotoka  hivi karibuni.

Read More