Jowy Landa Apinga Kauli ya Spice Diana Kuhusu Mafanikio Bila Kuwa na Hit songs

Jowy Landa Apinga Kauli ya Spice Diana Kuhusu Mafanikio Bila Kuwa na Hit songs

Mwanamuziki chipukizi kutoka Uganda, Jowy Landa, amejitokeza hadharani kupinga kauli ya Spice Diana kwamba mtu anaweza kufanikiwa katika muziki bila kuwa na nyimbo kali (hit songs). Kupitia mahojiano aliyofanya hivi karibuni na kituo cha redio, Jowy Landa alisema kuwa mafanikio ya kweli katika muziki hayawezi kupimwa kwa umaarufu wa mtu mtandaoni au mwonekano wa kisanaa pekee, bali kwa uwezo wa kutoa kazi zinazogusa mashabiki na kudumu kwenye chati. “Ni vigumu kusema umefanikiwa kama hauna hata wimbo mmoja ambao watu wanaweza kuuita hit. Mafanikio katika muziki yanatokana na impact unayoacha kwa wasikilizaji. Nyimbo kali huonyesha ubunifu na uwezo halisi wa msanii,” alisema Jowy. Kauli hiyo imeonekana kumlenga moja kwa moja Spice Diana, ambaye hivi majuzi alijinasibu kwamba amefanikiwa katika tasnia ya muziki licha ya kutoachia nyimbo nyingi zilizotamba. Mashabiki kwenye mitandao ya kijamii wamegawanyika, baadhi wakimuunga mkono Jowy kwa kusema kuwa muziki mzuri ndio unaojenga jina la msanii, huku wengine wakimtetea Spice Diana wakidai kuwa mafanikio ni pana zaidi na si lazima yaambatane na hit songs pekee.

Read More
 Jowy Landa Afunguka Baada ya Wasanii Kukwepa Mazishi ya Kaka Yake

Jowy Landa Afunguka Baada ya Wasanii Kukwepa Mazishi ya Kaka Yake

Msanii maarufu kutoka Uganda, Jowy Landa, amevunja ukimya na kueleza hisia zake kuhusu kutokuwepo kwa baadhi ya wasanii katika mazishi ya kaka yake, aliyefariki wiki iliyopita kufuatia majeraha aliyopata baada ya kushambuliwa na wahalifu jijini Kampala. Akizungumza kwenye mahojiano na kituo kimoja cha televisheni, Jowy alisema hakuwa na kinyongo na wale wasanii ambao hawakuhudhuria hafla hiyo, akieleza kuwa wengi wao walimfikia kwa njia binafsi kumpa pole. “Ilikuwa ni msiba, siyo tamasha. Walioweza kufika walifika, lakini wengine walinitumia jumbe za rambirambi. Kama msanii A Pass, alinipigia simu kunifariji. Wasanii huwa na ratiba nyingi, kwa hiyo sioni kuwa ni jambo kubwa sana,” alieleza Jowy. Aidha, alikanusha madai ya kuwepo kwa mgogoro baina yake na Nandor Love, akisisitiza kuwa bado ni marafiki wa karibu, japo kwa sasa kila mmoja anashughulika na majukumu tofauti. “Sijawahi kuwa na bifu na Nandor Love. Tumekuwa marafiki wa karibu sana, ila kwa sasa kila mmoja ana shughuli zake. Mimi nipo na Team No Sleep (TNS), naye yupo Ghost Empire, hivyo hatupatani mara kwa mara kama zamani,” aliongeza. Jowy Landa kwa sasa anaendelea na shughuli zake za muziki chini ya lebo ya TNS, huku akiendelea kupewa pole na mashabiki na wadau mbalimbali wa muziki kufuatia msiba huo mkubwa.

Read More
 Jowy Landa Atoa Majibu Mazito kwa Wakosoaji Wake

Jowy Landa Atoa Majibu Mazito kwa Wakosoaji Wake

Msanii wa muziki kutoka Uganda, Jowy Landa, ameibuka na kujibu ukosoaji anaoupata kutoka kwa baadhi ya mashabiki na wadau wa tasnia ya burudani, akisema kwamba hawamsumbui kwani anaamini wanachukizwa na mafanikio yake. Kwenye mahojiano na runinga moja nchini Uganda, Jowy alisema kwamba hafuatilii wala kubeba kwa uzito maoni ya wanaomsema vibaya.  “Mimi hukosolewa kwa sababu mimi ni bora. Watu huwa hawaendi kinyume na wasio na mvuto. Wanaonizungumzia ni kwa sababu wamekasirishwa na ukuaji wangu wa kimuziki,” alisema kwa msisitizo. Kauli hiyo imezua maoni mseto kutoka kwa mashabiki, hasa ikizingatiwa historia yake ya kutoa kauli kali dhidi ya wasanii wenzake. Mapema mwaka huu, alizua mjadala mkubwa baada ya kumkosoa vikali Spice Diana, akimtuhumu kuwa na kiwango duni cha sauti na kudai kwamba kazi zake hazina ubunifu wa kweli. Kauli hiyo iliwakasirisha baadhi ya mashabiki wa Spice Diana, lakini upande wa msanii huyo haukujibu hadharani, jambo lililowafanya wengi kusifu utulivu wa timu ya Spice katika kukabiliana na mivutano ya kisanii. Hata hivyo, Jowy sasa anaonekana kukerwa na ukosoaji wa watu dhidi yake, jambo ambalo limeibua maswali kutoka kwa baadhi ya wachambuzi wa burudani: Je, msanii anayependa kukosoa wenzake hastahili pia kukosolewa? Wadadisi wa masuala ya muziki wanasema hali kama hizi huibua mjadala kuhusu ukomavu wa wasanii, uwezo wa kujifunza kupitia maoni ya wengine, na uhusiano wa kweli kati ya ubunifu na ukosoaji wa wazi.

Read More
 Mwanamuziki wa Uganda Jowy Landa afunguka sababu za kutokuwa na mchumba

Mwanamuziki wa Uganda Jowy Landa afunguka sababu za kutokuwa na mchumba

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Jowy Landa amefunguka sababu za kutokuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi. Kwenye mahojiano yake hivi karibuni amesema anaogopa kuchumbiana na mwanaume akiwa anafanya muziki kwani atakuwa kizingiti kikubwa kwake kutunaua wigo kisanaa. “Wanaume huwa wanatudhulumu sana ila mimi sina mpenzi kwa sasa. Hawa wanaume wanaweza kukuharibia shughuli zako za kimuziki”, Alisema kwenye mahojiano na runinga moja. Jowy Landa amekuwa akihusushwa kutoka kimapenzi na meneja wake DJ Roja lakini amekuwa akipuzilia mbali madai hayo kwa kusema kuwa hayana ukweli wowote.

Read More