Meja Kunta Atoa Msamaha kwa Jux na D Voice Baada ya Utata wa Wimbo

Meja Kunta Atoa Msamaha kwa Jux na D Voice Baada ya Utata wa Wimbo

Baada ya drama ya muda mitandaoni kuhusu umiliki wa wimbo “Ex Wa Nani”, msanii wa singeli Meja Kunta amevunja ukimya na kutoa maoni yake juu ya sakata hilo, ambalo limewahusisha wasanii Jux na D Voice. Akizungumza na Podcast ya Simulizi na Sauti, Meja Kunta alieleza kuwa hana muda wa kubishana na watu anaowaita “watoto wadogo,” akionyesha msimamo wake wa kutotaka kuendeleza mzozo huo. “Mimi ni mkubwa, sikutaka kubishana na watoto wadogo. Sitaki kupigizana kelele. D Voice anajua mwenyewe alichokifanya na tumeshaongea jana,” alisema Meja Kunta kwa utulivu. Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya Jux kuposti kipande cha wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii, hatua iliyozua maswali kutoka kwa mashabiki kuhusu uhalali wa wimbo huo, ambao awali ulitajwa kuwa ni mali ya Meja Kunta. Taarifa zinaeleza kuwa D Voice alimpa Jux wimbo huo bila ridhaa ya Meja, hali iliyochochea mvutano wa maneno. Hata hivyo, Meja Kunta ameonesha ukomavu kwa kufichua kuwa Jux na D Voice walimpigia simu kumuomba msamaha, jambo ambalo linaashiria kutamatika kwa mgogoro huo. Kwa sasa, mashabiki wanasubiri kuona hatma ya wimbo huo na iwapo utafanyiwa marekebisho ya umiliki au utaachiwa rasmi na mmoja wa wahusika waliotajwa.

Read More
 Jux aeleza sababu za mwili wake kupungua

Jux aeleza sababu za mwili wake kupungua

Msanii wa Bongofleva Juma Jux amefunguka kupungua sana kimwili baada ya mashabiki kuzungumza mengi juu ya muonekano wake. Jux amesema kuwa sababu kubwa ya yeye kukonda ni kukosa muda wa kupumzika, kula na kutofanya mazoezi kutokana na albam yeke aliyokuwa akiiandaa kwa mashabiki zake alikosa muda mzuri ndio maana amepungua. Msanii huyo amewahakikishia mashabiki zake kuwa, mwili wake siku si nyingi utarudi katika hali ya kawanda kwani, anatarajia kuanza tena kufanya mzaoezi ili aweze kurudisha mwili. Lakini pia amesema kuwa hashindani na msanii yoyote bali anafanya muziki kwa ajili ya nchi na mashabiki zake na ndio maana kwenye album yake itwayo King Of Heart hajashirikisha wasanii wakubwa.

Read More
 Album mpya ya Jux kutoka Novemba 25

Album mpya ya Jux kutoka Novemba 25

Msanii wa Muziki Bongo, Jux ametangaza albamu yake mpya, ‘King of Hearts’ yenye nyimbo 16 itatoka Novemba 25 mwaka. Hii inakuwa ni albamu ya pili ya Jux kuiachia katika safari yake ya muziki baada ya ile ‘The Love Album’ iliyoachiwa mwaka 2019. Miongoni mwa wasanii walioshirikishwa kwenye albamu hii mpya ni pamoja na Zuchu, Mbosso, Marioo na Patoranking kutokea nchini Nigeria. Ukiachana na Jux, wasanii wengine wanaotarajia kuachia albamu mwaka huu na Rosa Ree na Marioo.

Read More
 HUDDAH: SIJAWAHI KUWA SINGLE MAISHANI MWANGU

HUDDAH: SIJAWAHI KUWA SINGLE MAISHANI MWANGU

Mrembo maarufu nchini na Afrika Mashariki kwa ujumla, Huddah Monroe anaendelea kufunguka tusioysajua kuhusu maisha yake. Kupitia instastory yake mrembo huyo amesema hajawahi kuwa single katika maisha yake yaani kwake kukaa bila mwanaume ni mwiko! “Jambo la kwanza siwezi kaa bila mwanamume, wanaume wameninunulia magari na manyumba sijawahi kuwa single maishani mwangu sijui huwa wanafanyaaje kuuwa mtu kama mimi,” amesema Huddah. Kauli yake inakuja siku chache baada ya kutusanua kwamba aliwahi kuolewa akiwa na umri wa miaka 19 na mwanamume ambaye hajamtaja jina lake. Hata hivyo, hawakupata watoto kwa sababu mwanaume wake alikuwa mraibu wa dawa za kulevya. “Nilikuwa kwenye ndoa (19), hatukuwa na mtoto na tukaachana kwa sababu mwanaume alikuwa mlevi wa dawa za kulevya! Sikuwa maarufu kwa hivyo sikuhitaji kuitangaza! So naongea kwa uzoefu. Si mzaha nyinyi nyote! Usiku mwema! Hiyo ndiyo siri yangu kubwa.” aliandika Insta Story. Utakumbuka Huddah Monroe anahusishwa kuwa na mahusiano na Staa wa Bongofleva, Jux baada ya hivi karibuni kuonekana pamoja hadi kutokea kwenye video ya mwimbaji huyo, Sikuachi.

Read More
 JUX AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA HUDDAH

JUX AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA HUDDAH

Mwanamuziki wa Bongofleva, Juma Jux amefunguka na kudai kwamba hana uhusiano wowote wa kimapenzi na mrembo Huddah kutoka nchini Kenya. Kwa kipindi kirefu kumekuwepo na tetesi za wawili kuwa pamoja ila sasa zimepamba moto baada ya Huddah kutokea kwenye video ya Jux, Simuachi. “Tufanye kwa ufupi ni rafiki yangu, nje ya vile ambavyo watu wanamjua, ni mtu ambaye anafikiria kitu ambacho kinaweza kutunufaisha wote wawili kila tunapokutana, kama umeona video kuna product zake kule,” Jux ameimbia The Switch ya Wasafi FM. Hata hivyo amekanusha kurudiana na aliyekuwa mpenzi wake, mrembo Jackie Cliff akisema hajawahi kuonana na mrembo huyo tangu atokea jela na kurejea nchini Tanzania kwani tayari ana mtu wake. “Niwe muwazi hatuna mawasiliano yoyote lakini mara ya kwanza kabisa wakati ametoka tulishawahi kuwasiliana, alinitumia tu meseji basi tukaongea” amesema juma_jux na kuongeza, “Kwa hiyo sasa hivi nadhani kitu kizuri ametoka ana uhuru wake kama kawaida hicho ndio kitu muhimu, mimi na maisha yangu, lakini kiukweli hatuna mahusiano yoyote.” Utakumbuka Jux amewahi kuwa na mahusiano na wanawake maarufu kama Jacqueline Wolper, Jackie Cliff na Vanessa Mdee.

Read More
 AMBER LULU: NAMTAMANI SANA JUX

AMBER LULU: NAMTAMANI SANA JUX

Msanii wa Bongofleva Amber Lulu amemtaja Juma Jux kuwa ndio mwanaume anayetamani kupata naye mtoto kwa sababu ana akili, yupo smart na atamuongoza vyema lakini pia amekuwa akimfuatilia msanii huyo kwa muda mrefu. Mrembo huyo ambaye anafanya poa na singo yake mpya iitwayo Nimeachika amesema amepanga kuzaa watoto 5 kila mmoja na baba yake sababu akizaa na baba mmoja kisha akafariki yeye ataishia kupata tabu na watoto. Ikumbukwe pia Amber Lulu kipindi cha nyuma alishaweka wazi kutamani kuwa kwenye mahusiano na Diamond Platnumz, lakini hata hivyo nafasi ya kuwa na Diamond inaonekana ni nyembamba sababu baada ya hitmaker huyo wa Naanzaje kuzaa watoto 4 na wanawake tofauti amekiri hivi karibuni kuwa kwa sasa kuwa kwenye mahusiano na wanawake sio kipaumbele chake bali nguvu amezielekeza kwenye kuzidi kufanya kazi ili kuendelea kufanikiwa kiuchumi.

Read More