Ziza Bafana Akanusha Taarifa za Ugomvi na Kalifah Aganaga

Ziza Bafana Akanusha Taarifa za Ugomvi na Kalifah Aganaga

Msanii wa muziki wa dancehall kutoka Uganda, Ziza Bafana, amefunguka kuhusu uhusiano wake na mwanamuziki mwenzake Kalifah Aganaga, akisema kwamba amekuwa sehemu muhimu ya mafanikio ya Aganaga katika tasnia ya muziki. Akizungumza katika mahojiano na Sanyuka Television, Ziza Bafana alikanusha madai kuwa alimshambulia Kalifah kwa maneno au kumdharau, akieleza kuwa alieleweka vibaya. Alisisitiza kuwa hana chuki yoyote dhidi ya Aganaga na hata hawezi kumkosea heshima. “Nilieleweka vibaya kwa sababu mimi binafsi sina ubaya wowote na Kalifah Aganaga. Sina nia mbaya kabisa. Kalifah ni kama ndugu yangu, na mimi ni mmoja wa watu waliomsaidia katika kujenga kazi yake ya muziki. Siwezi kumdharau,” alisema Bafana. Ziza Bafana na Kalifah Aganaga wote ni wasanii wakongwe kwenye muziki wa Uganda na wamewahi kushirikiana kwenye majukwaa mbalimbali. Kauli ya Bafana imekuja wakati ambapo mashabiki wamekuwa wakizungumzia uwezekano wa mgogoro kati yao, hali ambayo sasa inaonekana kufutwa na maelezo hayo ya amani. Mashabiki wamepokea taarifa hiyo kwa hisia tofauti, baadhi wakimtaka Bafana na Aganaga kurejea studio pamoja kama zamani, huku wengine wakisisitiza umuhimu wa umoja miongoni mwa wasanii wa Uganda.

Read More
 Kalifah Aganaga akerwa na kitendo cha Catharine Kusasira kujidhalalisha mbele ya umma

Kalifah Aganaga akerwa na kitendo cha Catharine Kusasira kujidhalalisha mbele ya umma

Mwanamuziki wa dancehall kutoka nchini Uganda Kalifah Aganaga amesikitishwa na kitendo cha Catherine Kusasira kuangua kilio hadharani kwenye mahojiano yake hivi karibuni kutokana na ugumu wa maisha. Kwenye mahojiano na Spark TV, Aganaga amesema ni aibu kwa mwanamuziki huyo mkongwe kujidhalalisha mbele ya umma kama mtoto ikizingatiwa kuwa alitumia vibaya mshahara aliokuwa analipwa na serikali kipindi anahudumu kama mshauri wa rais Yoweri Museveni. Kauli ya aganaga inakuja mara baada ya catherine kusasira kunukuliwa akieleza masaibu kuwa tangu atemwe kama mshairi wa rais mwaka wa 2021 amekuwa akipitia kipindi kigumu kiuchumi kiasi cha madalali kupiga mnada mjengo wake wa kifahari na gari yake aina Land cruiser V8 kwa ajili ya kukamilisha madeni anayodaiwa.

Read More
 KALIFAH AGANAGA AMCHANA PRODYUZA DADDY ANDRE,ADAI HANA VIGEZO VYA KUWA KIONGOZI

KALIFAH AGANAGA AMCHANA PRODYUZA DADDY ANDRE,ADAI HANA VIGEZO VYA KUWA KIONGOZI

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Kalifah Aganagah amemtolea uvivu prodyuza Daddy Andrea kwa kusema kwamba hana vigezo vya kuwa naibu wa rais wa muungano wa wasanii nchini chini humo. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Aganaga anadai Daddy Andre alishindwa kudhibiti mahusiano yake ya kimapenzi, hivyo sio mtu wa kuaminika kwenye masuala ya kuongoza wasanii wa uganda kupitia muungano wao. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Kiboko” ametoa kauli hiyo ikiwa ni miezi kadhaa imepita tangu Daddy Andre avunje uhusiano wake na Nina Roz baada ya prodyuza huyo kujitambulisha kwa wazazi wa Nina Roz kama mume wake. Kalifah Aganaga na Daddy Andre wanatarajiwa kichuana vikali kwenye kinyanganyiro cha unaibu wa rais wa muungano wa wasanii nchini Uganda katika uchaguzi utakaofanyika mwezi Mei mwaka huu.

Read More
 KALIFAH AGANAGA ATILIA SHAKA MFUMO WA UCHAGUZI UTAKAOTUMIWA NA MUUNGANO WA WANAMUZIKI NCHINI UGANDA

KALIFAH AGANAGA ATILIA SHAKA MFUMO WA UCHAGUZI UTAKAOTUMIWA NA MUUNGANO WA WANAMUZIKI NCHINI UGANDA

Mwanamuziki wa dancehall kutoka nchini Uganda Kalifah Aganaga ametoa wito kwa muungano wa wasanii nchini humo kutofanya uchaguzi wa kuwachagua viongozi wapya kwa njia ya mtandao. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Kiboko” amesema wasanii wengi nchini humo hasa chipukizi wamefulia kiuchumi, hivyo hawana uwezo wa kununua vifurushi vya kupigia kura mtandaoni. Utakumbuka Kalifah Aganaga ametia nia ya kugombea wadhfa wa unaibu rais katika muungano wa wasanii nchini uganda kwenye uchaguzi wa kuwachagua viongozi wapya wa muungano huo utakaofanywa hivi karibuni.

Read More
 KALIFAH AGANAGA ATIA NIA YA KUWANIA UNAIBU WA RAIS KWENYE MUUNGANO WA WANAMUZIKI UGANDA

KALIFAH AGANAGA ATIA NIA YA KUWANIA UNAIBU WA RAIS KWENYE MUUNGANO WA WANAMUZIKI UGANDA

Msanii na prodyuza wa muziki nchini Uganda Kalifah Aganaga ametia nia ya kugombea  wadhifu wa unaibu wa rais katika muungano wa wanamuziki nchihi humo kwenye uchaguzi  wa mwaka huu Kupitia mitandao yake ya kijamii Aganaga amesema ana vigezo vyote vya kuwa naibu wa rais wa muungano huo ikizingatiwa kuwa ana uelewa mpana wa changamoto zinazowakumba wanamuziki nchini uganda. Hata hivyo ametoa wito kwa wanachama wa UMA kuunga mkono azma yake ya kuwa naibu wa rais wa muungano huo huku akiwataka wampe kura zao, uchaguzi wa kuwachagua viongozi wapya utakapowadia.

Read More
 KALIFAH AGANAGA AWACHANA MAPROMOTA WA MUZIKI UGANDA KISA KUWAPENDELEA WASANII WA NIGERIA

KALIFAH AGANAGA AWACHANA MAPROMOTA WA MUZIKI UGANDA KISA KUWAPENDELEA WASANII WA NIGERIA

Mwanamuziki wa Dancehall kutoka nchini Uganda Kalifah Aganaga amedai kwamba mapromota wa muziki nchini humo hawana nia njema ya kuupeleka muziki wa Uganda kimataifa. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Aganaga amesema mapromota wengi nchini Uganda hawataki kuwapa wasanii wa ndani kipau mbele kwenye matamasha yao ya muziki na badala yake wamekuwa wakiwazingatia sana wasanii wa Nigeria, jambo ambalo amedai sio sahihi kwani wasanii wa ndani wana ushawishi mkubwa kuliko wa nje. Bosi huyo wa lebo ya muziki ya “Bad Character Records” ameenda mbali zaidi na kusema kwamba mapromota wa muziki nchini Uganda hawajawahi watakia mema wasanii wa muziki nchini humo ikizingatiwa kuwa wengi wao ni wanafiki. Utakumbuka katika siku za hivi karibuni wasanii wa Nigeria wamekuwa wakitumbuiza sana kwenye shows mbali mbali nchini Uganda tangu Rais Yoweri Museveni afungue uchumi wa nchi hiyo ambapo tayari tumewaona wasanii kama Ruger na Chike wakifanya shows zao huku wasanii kama Tiwa Savage,FireBoy na Burna Boy wakitarajiwa pia kutumbuiza kwenye shows zao.

Read More
 KALIFAH AGANAGA MBIONI KUMALIZA BIFU YAKE NA MSANII BEBE COOL

KALIFAH AGANAGA MBIONI KUMALIZA BIFU YAKE NA MSANII BEBE COOL

Mwanamuziki wa dancehall kutoka nchini Uganda Kalifah Aganaga amemaliza tofauti zake na msanii Allan Hendrick ambaye ni kijana wa Bebe Cool kwa kufanya wimbo wa pamoja. Katika mahojiano yake ya hivi karibuni Aganaga amesema amechukua hatua ya kumaliza ugomvi uliokuwepo kati yake na familia msanii Bebe Cool kama njia kuwaomba msamaha watu wote aliowakosoa kwenye career yake ya muziki. Hitmaker huyo wa “Kiboko” anaamini uhusiano wake na Allan Hendrick utamsaidia pakubwa kumfikia Bebe Cool ambaye kwa muda mrefu hajawakuwa na maelewano mzuri. Utakumbuka Aganaga wamekuwa kwenye bifu na Bebe Cool baada kumsuta vikali kwa hatua ya kumtekeleza kimuziki mwanae Allan Hendrick ambapo alienda mbali zaidi na kusema kuwa jambo lilomfanya mwanae huyo awe omba omba katika lebo ya muziki ya Gagamel kitendo kilichomkasirisha Bebe Cool.

Read More
 KALIFAH AGANAGA AMSHAURI PRODYUZA WA MUZIKI DADDY ANDRE AACHE KUIMBA

KALIFAH AGANAGA AMSHAURI PRODYUZA WA MUZIKI DADDY ANDRE AACHE KUIMBA

Mwanamuziki na mtunzi wa nyimbo kutoka nchini Uganda Khalifah Aganaga amemtaka Daddy Andre kuamua iwapo anataka kuwa mtayarishaji wa muziki au mwimbaji. Kulingana na Aganaga, ni vigumu msanii kufanikiwa kwenye nyanja mbili za utayarishaji wa muziki na uimbaji kwa wakati mmoja. Hitmaker huyo wa “Kiboko”  amesema ikiwa daddy andre ataendelea kuimba atapoteza biashara kama prodyuza ikizingatiwa kuwa wasanii watamkimbia kwa hofu ya kuibiwa ubunifu wao kwenye nyimbo zao. “Ikiwa ataendelea kuimba, atapoteza biashara yake kama prodyuza. Baadhi ya wanamuziki wakubwa na wenye vipaji watamkimbia wakihofia kuwa anaweza kuiba mawazo yao na kuyatumia kwa manufaa yake,” Aganaga alisema kwenye mahojiano. Hata hivyo ameenda mbali zaidi na kusema kuwa prodyuza anayeimba hawezi tenga muda kwa wasanii wanaotaka kufanya kazi nae kwani atajikita zaidi kwenye muziki. “Prodyuza anayeimba hawezi tenga muda kwa msanii mwingine. Producer atajikita zaidi kwenye muziki wake kuliko watu anaofanya nao kazi,” aliongeza. Mpaka sasa Daddy Andre hajazungumza chochote kuhusiana na vijembe vya Kalifah Aganaga. Daddy Andre ana nyimbo nyingi kwenye kabati la muziki wake ikiwemo; “Tugende Mu Church”, “I miss you” “Omwana wa Bandi”, “Hurt you” miongoni mwa zingine.

Read More
 KALIFAH AGANAGA ADAI MUSEVENI AMESHINDWA KUTIMIZA AHADI YA KUMFADHILI KIMASOMO

KALIFAH AGANAGA ADAI MUSEVENI AMESHINDWA KUTIMIZA AHADI YA KUMFADHILI KIMASOMO

Mwanamuziki kutoka nchini Uganda Kalifah Aganaga amefichua kuwa Rais Museveni ameshindwa kutimiza ahadi yake aliyotoa ya kumfadhili kusomea kozi ya uhandisi wa sauti nchini Marekani. Akiwa kwenye moja ya interview, Hitmaker huyo wa “Kiboko” amesema kwamba Museveni alikubali kumfadhili kimasomo nje ya nchi walipokutana katika Ikulu ya rais mwaka wa 2020 ila kwa watu wake wa karibu wamekuwa wakimpa ahadi za uongo. Kalifah Aganaga aliigura chama cha NUP na kutimukia NRM baada ya kushindwa kupata tiketi ya chama hicho ambayo ingemsaidia kuwania ubunge wa eneo la Rubaga Kusini.

Read More