Karen Nyamu afunguka baada ya kuzua tafrani nchini Dubai

Karen Nyamu afunguka baada ya kuzua tafrani nchini Dubai

Baby Mama wa mwanamuziki wa Mugithi Samidoh Muchoki, Karen Nyamu amezungumzia kuhusu video iliyosambaa mtandaoni akiwa anasindikizwa na walinzi nje ya ukumbi wa tamasha la Samidoh huko Qatar. Akizungumza moja kwa moja kwenye mtandao wa Instagram, Karen Nyamu amesema hakuwa na habari kuwa alihitaji leseni ya kuonekana jukwaani. Katika utetezi wake, amesema hakufanya kosa lolote kwenda jukwaani kwani alikuwa akifurahia tu burudani kama mashabiki wengine. Seneta huyo mteule ameongeza kuwa chini ya shinikizo ya kilevi, hivyo maazimio yake ya 2023 ni kuacha kunywa pombe kabisa. “Pombe inanifanya nisahau njia, Nimeacha Pombe.” Kwenye instagram live, shabiki mmoja alimshauri aache kufuata Samidoh ambapo alijibu kwamba anahitaji maombi ili kukomesha mzaha maishani mwake. Karen Nyamu pia aliwataka mashabiki wake wasiwe na wasiwasi naye. “Niko na Kila kitu kitu sina ni haya.” Akijibu moja ya shabiki yake, aliongeza kuwa hana mpango wa kuachana na Samidoh kwa sababu ya malezi ya watoto wao wawili kwa pamoja. “Simuachi, lazima Tulee watoto.”

Read More
 Karen Nyamu azua purukushani kwenye tamasha la Samidoh Dubai

Karen Nyamu azua purukushani kwenye tamasha la Samidoh Dubai

Seneta mteule  Karen Nyamu amejipata katika hali ya aibu baada ya kujaribu kujiunga na baba wa mtoto wake Samidoh Muchoki jukwaani alipokuwa akitumbuiza nchini Dubai. Kwenye video inayosambaa sana katika mitandao ya kijamii, Karen Nyamu ameonekana akivamia jukwaa ambalo Samidoh alikuwa akitoa burudani kwa mashabiki katika jaribio la kujiunga na mwanamuziki huyo wa Mugithi. Samidoh hata hivyo hakumpa muda wa kuzua purukushani ambapo walinzi wake walimsindikiza Karen Nyamu nje. Katika video hiyo, Samidoh alisimama akiwatazama maafisa wa usalama wakimsindikiza mama ya mtoto wake nje. Kisha akamkumbatia mkewe Edday Nderitu kwa upendo huku wakipiga picha na mashabiki. Siku chache zilizopita, Samidoh na mkewe walisafiri nchini Dubai kwa ajili ya hafla ya sherehe ambapo alitarajiwa kutumbuiza pamoja na wanamuziki wengine. Mama ya mtoto wake Karen Nyamu pia alijikatia tiketi ya ndege kujiunga nao kwenye sherehe hiyo ya mwisho wa juma. Mashabiki wengi walikasirishwa na hatua ya Karen kuhujumu safari ya Samidoh-Edday kwa kusema kwamba alimkosea heshima mke mkuu wa mwanamuziki huyo.

Read More