KAROLE KASITA AKANUSHA KUWA NA UJA UZITO WA FFEFE BUSI

KAROLE KASITA AKANUSHA KUWA NA UJA UZITO WA FFEFE BUSI

Siku kadhaa zilizopita video iliokuwa ikionesha uja uzito wa msanii Karole Kasita ilivuja na kusambaa mtandaoni. Walimwengu kwenye mitandao ya kijamii walianza kuhusisha uja uzito huo na rapa Ffefe Busi ambaye walimtaja kama mhusika mkuu kutokana na ukaribu wake na mrembo huyo. Sasa Karole Kasita ameibuka na kukanusha madai yao kwenye mahojiano yake mapya kwa kusema kwamba hajawahi kuwa na mahusiano yeyote ya kimapenzi na Ffefe Busi kwani ni mshikaji wake wa karibu. Hitmaker huyo wa “You” amesema anayehusika na uja uzito wake ni mtu anayemheshimu, hivyo hatoweka wazi maelezo ya uja uzito wake kwa umma kwani hapendi kuanika mambo yake ya faragha hadharani.

Read More
 KAROLE KASITA APINGA HATUA YA SERIKALI KUPIGA MARUFUKU WASANII KUTUMBUIZA MASHULENI

KAROLE KASITA APINGA HATUA YA SERIKALI KUPIGA MARUFUKU WASANII KUTUMBUIZA MASHULENI

Msanii Karole Kasita amekosoa hatua ya wizara ya elimu nchini Uganda kuwapiga maarufuku wasanii kutumbuiza kwenye shule za umma kutokana na wao kuvalia mavazi yao yanayokwenda kinyume na maadili ya jamii. Karole Kasita amesema wizara ya elimu nchini Uganda inapaswa ije na njia nyingine kushughulikia swala la wasaniii kuvalia vizuri wakiwa jukwaani kwani inahujumu kazi za wasanii ikizingatiwa wengi wao wanategemea muziki kupata riziki. Wasanii wengine ambao wameonekana kutoridhishwa na kitendo cha Wizara ya Elimu kusitisha maonesho mashuleni kutokana na wasanii kutovali mavazi yenye staha ni pamoja na Pia Ponds na Rickman Manrick. Utakumbuka mapema wiki hii wizara ya elimu nchini Uganda ilisitisha maonesho ya muziki mashuleni hadi pale watakapotoa mweelekeo wa namna  wasanii wanapaswa kuvalia wakiwa kwenye majukwaa ya shule.

Read More
 KAROLE KASITA WAZOZANA NA MENEJA WAKE JORAM KISA PESA

KAROLE KASITA WAZOZANA NA MENEJA WAKE JORAM KISA PESA

Karole Kasita alianza kuimba akiwa shule ya upili ya St. Joseph Naggalama ambapo alirekodi wimbo wake wa kwanza uitwao  “Bounce it” kwa ushirikiano na msanii Nutty Neithan mwaka wa  2015 akiwa chuo kikuu. Lakini baada alijuunga na bendi ya muziki ya S &  S kabla ya kuanza muziki wake kama msanii wa kujitegemea mwaka wa 2018. Karole ambaye anajulikana kwa uwezo wake mkubwa wa kutoa burudani ya nguvu akiwa jukwaani ameweka alama kwenye tasnia ya muziki nchini uganda kama moja kati ya wasanii wa kike wanaofanya vizuri. Ufanisi huo umetokana na mchango wa Meneja Joram ambaye amekuwa akisimamia muziki wake kwa muda lakini taarifa mpya ni kuwa mrembo hafanyi kazi tena na meneja wake huyo. Chanzo cha karibu na karole kasita kinasema msanii huyo na meneja wake waliingia kwenye ugomvi kutoka na mzozo wa fedha jambo lilomlazimu mrembo huyo kujiondoa na kuanza kufanya muziki wake kivyake. “They are no longer working together. They fell out and it could be due to money,” the source revealed. Hata hivyo mpaka sasa Karole Kasita pamoja na aliyekuwa meneja wake wapo kimya juu ya suala hilo.

Read More
 KAROLE KASITA APUZILIA MBALI UCHAGUZI WA CHAMA CHA WASANII UGANDA

KAROLE KASITA APUZILIA MBALI UCHAGUZI WA CHAMA CHA WASANII UGANDA

Mwanamuziki kutoka Uganda Karole Kasita amedai kwamba hatoshiriki uchaguzi wa chama cha wanamuziki nchini humo ambao utafanyika mwezi huu. Katika mahojiano yake hivi karibuni Karole Kasita  amepuzilia mbali uchaguzi huo kwa kusema kwamba wagombea wa nyadhfa za uongozi katika chama hicho hawana ajenda za kuwasaidia wasainii wa uganda kwani wengi wao wanalenga kujinufaisha wenyewe. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Balance” amesema hatashiriki uchaguzi wa chama cha wasanii nchini uganda hadi pale chama hicho kitaanza kuangazia maslahi ya wasanii. “Sitapiga kura wala kushiriki katika masuala ya chama hadi watakapokuwa tayari kusaidia tasnia hiyo. Wengi wao wanatafuta pesa kutoka kwa serikali, hawaujali sisi,” alisema. Utakumbuka Cindy Sanyu na King Saha wanawania nafasi ya urais katika Chama cha Wanamuziki nchini Uganda (UMA).

Read More
 KAROLE KASITA ADAI HATAKI KUSIKIA HABARI YA HARUSI KWENYE MAISHA YAKE

KAROLE KASITA ADAI HATAKI KUSIKIA HABARI YA HARUSI KWENYE MAISHA YAKE

Msanii wa muziki wa dancehall kutoka nchini uganda Karole Kasita amefunguka na kudai kwamba hataki kabisa kufunga ndoa kwa njia ya harusi.   Karole kasita amesema hana imani tena na wanaume na hivyo haoni akimtambulisha mwanaume yeyote kwa wazazi wake hivi karibuni.   Hitmaker huyo wa Balance amesema anafadhalisha mahusiano yake yawe ya siri kwani kuna aibu kubwa uibuka wakati mwanamke anapoachwa baada ya harusi.   Kauli yake imekuja mara baada ya kuumizwa kwenye mahusiano yake ya zamani baada ya kuachwa na mchumba kipindi yupo chuo kikuu, hivyo hanawaogopa wanaume wote kwani wanaweza kumkimbia.            

Read More