KENRAZY AACHIA RASMI SON OF GOD ALBUM
Mkali wa muziki nchini Kenrazy ameachia rasmi album yake mpya inayokwenda kwa jina la Son of God. Son of God album imebeba jumla ya mikwaju 20 ya moto huku ikiwa na kolabo 7 pekee. Kenrazy amewashirikisha wasanii mbali mbali wa humu nchini kama Bigpin, Kaya,Visita, Sosuun, Civa Ramah K na Young haze. Album ya “Son of God” ni album ya tatu kwa mtu mzima kenrazy baada ya Ti-chi ya mwaka wa 2008 na Get it Right from Kenrazy ya mwaka wa 2011. Hata hivyo Album hiyo inapatikana ‘Exclusive’ kupitia mitandao yote ya kukisikiliza na kuuza muziki duniani kama vile youtube, na Spotify
Read More