Wilbroda Atoa Wito kwa Rais Ruto Asikie Kilio cha Wananchi

Wilbroda Atoa Wito kwa Rais Ruto Asikie Kilio cha Wananchi

Mwigizaji maarufu wa Kenya, Wilbroda, ameibua hisia kali mtandaoni baada ya kueleza kwa uchungu hali ngumu ambayo wananchi wanapitia chini ya utawala wa sasa, huku akimpelekea Rais William Ruto ujumbe wa moja kwa moja akimtaka asikilize kilio cha wananchi. Kupitia video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Wilbroda alieleza kuwa bado kuna muda wa miaka miwili na nusu kabla ya uchaguzi mwingine, na angetamani sana kuona Rais akisikia sauti ya wananchi na kurekebisha baadhi ya mambo ambayo, kwa mtazamo wake, yameathiri maisha ya wananchi wa kawaida. “Ningependa sana askize ground, this guy still has two and a half years, I wish he would listen to the people and reverse a lot of things that have happened in this country. People are going through so much,” alisema Wilbroda kwa hisia kali. Kauli yake imeibua maoni tofauti kutoka kwa Wakenya mtandaoni, wengi wakimuunga mkono na wengine wakimtaka azingatie usawa katika uchambuzi wake. Lakini ujumbe wake umeeleweka wazi: maisha yamekuwa magumu kwa mwananchi wa kawaida, na kuna haja ya serikali kuchukua hatua kurekebisha hali hiyo. Wilbroda, anayefahamika kwa ucheshi na uigizaji wa kuvutia, amekuwa sauti ya watu wengi mitandaoni, na kwa mara hii, ameamua kutumia umaarufu wake kuangazia masuala ya kijamii yanayoathiri mamilioni ya Wakenya.

Read More