Keyshia Cole Amwaga Hisia Baada ya Kuvunjika kwa Penzi Lake na Hunxho

Keyshia Cole Amwaga Hisia Baada ya Kuvunjika kwa Penzi Lake na Hunxho

Malkia wa R&B, Keyshia Cole, amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu kuachana kwake na rapa Hunxho katika mahojiano mapya kwenye kipindi cha The Breakfast Club. Msanii huyo mashuhuri alizungumza kwa uwazi kuhusu hali yake ya sasa ya kimapenzi na kueleza kuwa bado hajapona kabisa baada ya kuvunjika kwa uhusiano huo. Alifafanua kuwa kwa sasa yuko single na kwamba hali hiyo si ngumu hata kidogo kwake. Hata hivyo, alikiri bado hajawa tayari kuanza mahusiano mapya, ingawa anapokea pongezi na ishara za kuvutiwa kutoka kwa wanaume wengine. “Niko single , siyo hali ngumu hata kidogo… ni kweli kabisa niko single,” alisema Cole kwa kujiamini. Keyshia alisema kuwa moja ya sababu zinazomfanya ajisikie bado hajawa tayari kuendelea mbele ni kwamba bado ana tattoo inayomkumbusha kuhusu Hunxho, jambo linaloonesha kuwa hisia bado zipo. “Sijaamua kurudi kwenye dunia ya mahusiano bado [lakini] napokea pongezi… lakini je, niko tayari kuendelea? Hapana. Bado nina tattoo hii hapa kwa hiyo siwezi… sijui,” aliongeza kwa hisia. Kauli zake zimewagusa mashabiki wake ambao wamekuwa wakimpongeza kwa uaminifu na uwazi wake. Ingawa uhusiano wake na Hunxho umeisha, bado anaonekana kuugulia kimya kimya. Mashabiki wanaendelea kumuunga mkono na kumtakia afueni ya haraka na mafanikio katika maisha yake ya baadaye

Read More
 LEO KATIKA HISTORIA OKTOBA 14, ALIZALIWA MWANAMUZIKI KUTOKA MAREKANI KEYSHIA COLE.

LEO KATIKA HISTORIA OKTOBA 14, ALIZALIWA MWANAMUZIKI KUTOKA MAREKANI KEYSHIA COLE.

Siku kama ya leo oktoba 15 mwaka wa 1981 alizaliwa staa wa muziki wa RnB kutoka marekani Keyshia Cole. Jina lake halisi ni Keyshia Myeshia Johson na alizaliwa huko Oakland Carlifonia nchini Marekani ambako alianza kujifunza kuimba ambapo marafiki zake walimtambulisha kwa rap mkongwe nchini marekani MC Hammer akiwa na miaka 12 tu na kutaka kuimba naye. Keyshia baadae alijenga urafiki na 2 Pac ambaye alimwambia atamsaidia kwenye kumjenga kimuziki lakini kwa bahati mbaya hakufanikiwa kufanya kazi na rapa huyo ambaye alikuja akafariki baada kupigwa risasi. Akiwa na miaka 18 Keyshia Cole alihamia mjini Los Angeles  na kuanza kufanya kazi na wasanii kama D’Wayne Wiggings  wa  Tony Toni Tone na Messy Marv. Mwaka 2002, alitambulishwa kama msaani wa lebo ya muziki ya A&M Records A&R Ron baada ya boss wa lebel hio kusikia wimbo wake wa “Love” ukiwa bado hujakamilika ila ulivyokamilika ulikuwa wimbo wa kwanza wa Keyshia Cole kuuza kopi milioni 1 nchini Marekani. Mwaka wa 2005 Keyshia Cole aliachia album yake ya kwanza iitwayo The Way It Is  album ambayo ilifanikiwa kufikia viwango vya mauzo ya gold na platinum kwa kuuza zaidi ya nakala milllioni 1.6. Baada ya kuachana lebo ya muziki ya A& M record alijiunga na lebo ya Geffen Records ambayo ilisimamia kazi zote za album yake ya pili   iliyotoka mwaka 2007 inayokwenda kwa jina la Just Like You. Album hiyo ilifanikiwa kupata mapokezi mazuri nchini marekani kwani ilifanikiwa kushika namba 2 kwenye chati ya Billboard 200 lakini pia iliweza kufikia viwango vya mauzo ya platinum kwa kuuza zaidi ya nakala milllioni 1.7 nchini marekani pekee. Mpaka sasa KeyshiaCcole ameshafanya jumla ya album saba za muziki, single 17, soundtrack album 6, na ameshirikishwa na wengine kwenye album 18 za muziki.

Read More