KANYE WEST ANUNUA MJENGO KARIBU NA NYUMBA YA KIM KARDASHIAN

KANYE WEST ANUNUA MJENGO KARIBU NA NYUMBA YA KIM KARDASHIAN

Staa wa muziki wa Hiphop kutoka nchini Marekani Kanye West ni kama amekubali yaishe kuhusu sakata la talaka na Kim Kardashian, ameona hawezi kumrudisha na sasa ameamua kumsogelea karibu ili apate nafasi ya kushirikiana naye kwenye malezi ya watoto wao. Tovuti ya Daily Mail imeripoti kwamba Kanye West amenunua nyumba yenye thamani ya dolla millioni 4.5 ambayo ni takribani shillingi millioni 508 kwa pesa za Kenya iliyopo kando ya mtaa ambao anaishi Kim Kardashian na watoto wake. Nyumba hiyo ipo kwenye eneo la mita za mraba 3,650 ikiwa na vyumba 5 vya kulala. Kanye West na Kim Kardashian ni wazazi wa watoto wanne ambao ni; North, Saint, Chicago, na Psalm, kwasasa hawako pamoja huku sakata la talaka likienda mahakamani. Hata hivyo tayari Kim Kardashian yupo kwenye mahusiano mapya na mchekeshaji Pete Davidson, uhusiano uliowekwa wazi hivi karibuni.

Read More
 KIM KARDASHIAN ASHINDA KIPENGELE CHA UMILIKI WA NYUMBA KWENYE SHAURI LA TALAKA

KIM KARDASHIAN ASHINDA KIPENGELE CHA UMILIKI WA NYUMBA KWENYE SHAURI LA TALAKA

Mahakama ya mjini Los angeles nchini marekani imempatia ushindi Kim Kardashian wa umiliki wa nyumba kwenye shauri la talaka linaloendelea dhidi yaKkanye West. Kim ameshinda kipengele hicho na sasa ni mmiliki wa nyumba ambayo walianzia maisha na Kanye West na kuanzisha familia pamoja. Jumba hilo lenye thamani ya shilling billion 6.7  lipo mjini Hidden Hills California, mwaka wa 2014 walilinunua pamoja kwa shilling billioni 2.6 kisha baadaye mwaka wa 2020 Kanye West aliikarabati. Hii imekuja kufuatia mustakabali wa watoto wao ambao wamezoea kuishi mahali hapo. Taarifa hii imekuja ikiwa ni siku chache tangu kanye west aiweke kwenye mnada moja ya ranchi zake zilizopo huko Wyoming nchini kwa shilling billioni 1.2. Mwezi uliopita  Kanye West pia aliripotiwa kununua jumba la kifahari kwenye fukwe za malibu huko marekani kwa shilling billioni 6.3.

Read More