Lauren Pisciotta Aibuka na Madai Mapya Dhidi ya Kanye West

Lauren Pisciotta Aibuka na Madai Mapya Dhidi ya Kanye West

Aliyekuwa Msaidizi wa rapa Kanye West, Lauren Pisciotta ameibuka tena na tuhuma nzito za unyanyasaji dhidi ya rapa huyo na safari hii amedai kuwa Kanye alimfanyia mambo mengi mazito kuliko hata yale aliyowahi kuyaeleza mwaka jana. Katika malalamiko mapya Pisciotta anadai Kanye alimfanyia mambo mengi mabaya, ikiwemo shambulio la ngono, unyanyasaji wa kijinsia, uviziaji na mengine mengi pamoja na tukio la kumbusu mdomoni kwa lazima na kumuuliza jinsi sehemu zake za siri zilivyo wakati wakiwa hotelini kwenye safari ya kikazi huko San Francisco. Itakumbukwa kuwa mwaka jana mwadada huyo aliibuka kwa mara ya kwanza kumshtaki Kanye West kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na kumsimamisha kazi kinyume cha sheria ingawa msanii huyo aliyapuuza na kuyakejeli madai hayo kupitia mitandao ya kijamii.

Read More