Lava Lava Atangaza Ujio wa EP Mpya ‘Time’

Lava Lava Atangaza Ujio wa EP Mpya ‘Time’

Msanii nyota wa Bongofleva, Lava Lava, ametangaza rasmi ujio wa Extended Playlist (EP) yake mpya inayotarajiwa kuachiwa Ijumaa hii. Kazi hiyo mpya, inayokwenda kwa jina la Time, imebeba jumla ya nyimbo sita za moto, ikiwa na kolabo mbili za kuvutia kutoka kwa wasanii Yammi na Bill Nass. EP hii inakuwa kazi yake ya kwanza tangu ajiondoe kwenye lebo ya WCB, hatua inayoashiria mwanzo mpya katika safari yake ya muziki akiwa msanii huru. Lava Lava amesema anatarajia mashabiki wataipokea kwa hamasa, akieleza kuwa “Time” ni mradi uliojaa ubunifu, hisia na ujumbe wa maisha. Kwa mujibu wa taarifa, EP hiyo itapatikana kwenye majukwaa yote ya muziki mtandaoni kuanzia siku ya uzinduzi. Mashabiki wameshaanza kuonyesha shauku kubwa kupitia mitandao ya kijamii, wakisubiri kusikia ladha mpya kutoka kwa msanii huyo anayefahamika kwa sauti yake ya kipekee.

Read More
 Lava Lava Apata Ubalozi Wake wa Kwanza Tangu Kuondoka WCB

Lava Lava Apata Ubalozi Wake wa Kwanza Tangu Kuondoka WCB

Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Lava Lava, ametangaza rasmi mkataba wake wa kwanza wa ubalozi tangu alipoondoka kwenye lebo ya WCB Wasafi. Msanii huyo sasa ni balozi wa kampuni ya kuuza magari ya Khushi Motors Tanzania. Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi rasmi wa yard ya kampuni hiyo, Lava Lava alisema amefurahia kushirikiana na Khushi Motors, ambayo inalenga kuwasaidia Watanzania wengi kupata magari kwa bei nafuu na zinazolingana na hali ya maisha ya watu wa kawaida. “Khushi Motors ipo kwa ajili ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata gari analolitamani kwa bei inayomuwezesha,” alisema Lava Lava wakati wa tukio hilo, huku akionyesha furaha yake kwa hatua hiyo mpya kwenye maisha yake ya sanaa na biashara. Ubalozi huu unakuja kama ishara ya mwanzo mpya kwa Lava Lava baada ya kujitegemea nje ya WCB, na mashabiki wake wengi wamepongeza hatua hiyo, wakimtakia mafanikio zaidi ndani na nje ya muziki. Kwa sasa, Lava Lava anatarajiwa kushiriki katika kampeni mbalimbali za masoko za Khushi Motors, ikiwa ni pamoja na matukio ya mauzo, promosheni na kampeni za kidigitali kupitia mitandao ya kijamii.

Read More
 Lava Lava Aondoka Rasmi WCB Wasafi, Aanza Safari Mpya ya Muziki

Lava Lava Aondoka Rasmi WCB Wasafi, Aanza Safari Mpya ya Muziki

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Lava Lava, ameashiria rasmi kuanza ukurasa mpya katika maisha yake ya muziki kwa kuondoa machapisho yote kwenye ukurasa wake wa Instagram, hatua ambayo imewasha moto wa mijadala mitandaoni kuhusu hatima yake ya kisanii. Hatua hii imejiri saa chache tu baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa WCB Wasafi, Diamond Platnumz, kuthibitisha mbele ya waandishi wa habari kuwa Lava Lava ameondoka kwenye lebo hiyo rasmi bila kulazimika kulipa ada yoyote ya kuvunja mkataba. Zaidi ya hapo, Diamond alieleza kuwa wamempa Lava Lava kiasi cha pesa kama msaada ili kumuwezesha kuanzisha maisha ya kujitegemea katika tasnia ya muziki. “Tumeachana kwa amani, hakuna malipo yoyote aliyotakiwa kutoa, na kama familia, tumempa sapoti ya kifedha kuanza safari yake mpya,” alisema Diamond. Lava Lava, ambaye amekuwa chini ya lebo ya WCB kwa miaka kadhaa, amejijengea jina kwa nyimbo kadhaa zilizotamba kama Tuachane, Gundu, na Saula. Hatua ya kuondoka Wasafi inatafsiriwa na wengi kama ishara ya kutafuta uhuru zaidi wa kisanii na kusukuma mbele ndoto zake kwa mtazamo mpya. Mashabiki wake wameonyesha hisia mseto, wengine wakimsifu kwa ujasiri wa kuanza upya, huku wengine wakisubiri kwa hamu kuona mwelekeo mpya wa kazi yake ya muziki. Wakati huo huo, sekta ya burudani inasubiri kuona ikiwa Lava Lava ataibuka na label yake binafsi au ataungana na mtandao mwingine wa kimuziki. Kwa sasa, yote macho kwa Lava Lava, msanii anayechukua hatua ya mabadiliko kwa matumaini, heshima, na dira mpya.

Read More
 LAVA LAVA ATANGAZA UJIO MPYA,OKTOBA 23

LAVA LAVA ATANGAZA UJIO MPYA,OKTOBA 23

Msanii wa bongofleva kutoka WCB, Lava Lava ametangaza kuja na project mpya, Oktoba 23, mwaka wa 2021. Lava Lava ambaye hivi karibuni amefuta picha zake zote kwenye ukurasa wake wa Instagram, amechapicha ujumbe kuhashiria Oktoba 23, mwaka huu atakuwa na kitu. Ikumbukwe mwimbaji huyo ambaye mwaka huu ameachia  EP iitwayo ‘Promise’, tayari alitangaza kukamilika kwa albamu yake. Mwaka huu wasanii wa WCB kama Rayvanny na Mbosso wameweza kutoa albamu zao na zinazidi kufanya vizuri.

Read More