Socialite Liebe Kiki Awaonya Wasichana Wanaotaka Kujichubua: “Hakikisha Una Pesa ya Kutosha”

Socialite Liebe Kiki Awaonya Wasichana Wanaotaka Kujichubua: “Hakikisha Una Pesa ya Kutosha”

Socialite maarufu Liebe Kiki ametoa ushauri kwa wasichana wanaotamani kujichubua ngozi, akisema kuwa mchakato huo ni wa gharama kubwa na unahitaji maandalizi ya kifedha ya kutosha. Kupitia video iliyosambaa mitandaoni, Liebe Kiki alisema kwamba kujichubua si jambo la mchezo na ni lazima mtu awe na uwezo wa kifedha wa kuendeleza matunzo ya ngozi kwa muda mrefu, la sivyo atajikuta katika hali mbaya zaidi kiafya na kimuonekano. “Kujichubua ni gharama. Kama huna pesa za kutosha, tafadhali usianze. Itakupeleka pabaya zaidi kuliko ulivyokuwa,” alisema Kiki. Socialite huyo aliongeza kuwa wasichana wengi huingia kwenye safari ya kujichubua bila kuelewa kikamilifu kile kinachohitajika, na matokeo yake huishia kuwa na matatizo ya ngozi kama vipele, kuchomwa na kemikali, au mabadiliko mabaya ya rangi ya ngozi. Hii si mara ya kwanza kwa Kiki kutoa maoni kuhusu mitindo ya urembo. Amekuwa mstari wa mbele kuzungumzia upasuaji wa kuongeza makalio, maisha ya mitandaoni, na changamoto wanazopitia wanawake maarufu.

Read More
 Mwanamitindo Liebe Kiki Aachana na Bleaching, Ahamasisha Kujikubali

Mwanamitindo Liebe Kiki Aachana na Bleaching, Ahamasisha Kujikubali

Mwanamitindo na influencer maarufu, Liebe Kiki, amefunguka kuhusu safari yake ya kurejesha rangi yake halisi ya ngozi baada ya kutumia kwa muda mrefu bidhaa za kubadilisha rangi. Katika taarifa yake kupitia Instagram, Kiki alieleza kuwa yuko kwenye hatua za mwisho za kuondoa athari za bleaching na kufichua kuwa sababu kubwa iliyomsukuma kuanza mchakato huo ilikuwa ni majeraha ya kihisia aliyopitia akiwa mtoto. Kiki alisema kuwa alipitia changamoto nyingi za kiakili na kihemko ambazo zilisababisha kujitafuta kwa kina, hali iliyompelekea kufanya maamuzi ambayo baadaye aligundua yalikuwa ya kujeruhi nafsi yake. Aidha, alieleza kuwa ujasiri wa kueleza hadharani kuhusu mabadiliko ya ngozi ni sehemu ya safari yake ya kujikubali. Mashabiki wake wamepongeza hatua yake hiyo wakisema ni mfano wa kuigwa kwa vijana wengi wanaojikuta kwenye shinikizo la mabadiliko ya mwonekano kutokana na hali ya kijamii au familia. Ushuhuda wake umetajwa kuwa wa kuhamasisha watu wengi kuukubali uhalisia wao na kutafuta utilivu wa roho badala ya suluhisho za nje. Suala la kubadili rangi ya ngozi limeendelea kuibua mijadala mikali mtandaoni, hasa kuhusu athari zake kiafya na kiakili. Kwa hatua yake ya kujieleza kwa uwazi, Liebe Kiki sasa anachukuliwa kama sauti ya mabadiliko na mfano wa kuigwa katika kujikubali na kujipenda jinsi ulivyo.

Read More