Davido Atoa Sababu za Kutoshiriki Tamasha la London

Davido Atoa Sababu za Kutoshiriki Tamasha la London

Msanii maarufu wa muziki wa Afrobeats kutoka Nigeria, Davido, ametangaza kujiondoa rasmi katika tamasha kubwa la muziki lililopangwa kufanyika katika uwanja wa Tottenham Hotspur jijini London, ambalo lilitarajiwa kufanyika Julai 2025. Tamasha hilo lilikuwa linamjumuisha pamoja na wakali wa muziki kutoka Marekani, 50 Cent na Mary J. Blige. Kupitia taarifa aliyoitoa kwenye mitandao ya kijamii, Davido alieleza kuwa licha ya tamasha hilo kupata uungwaji mkono mkubwa kutoka kwa mashabiki pamoja na mafanikio katika mauzo ya tiketi, kulikuwepo na matatizo ya msingi katika maandalizi na uendeshaji wa tukio hilo Katika maelezo yake, Davido alionyesha kutoridhishwa na mchakato mzima wa maandalizi na kuonyesha kuwa uamuzi huu umetolewa baada ya mazungumzo yaliyoshindikana kati ya pande mbili, jambo lililomfanya asisitize kutoshiriki kwenye tamasha hilo. Uamuzi huo umewashtua mashabiki wengi waliokuwa na matarajio makubwa ya kumuona msanii huyo akitumbuiza sambamba na majina makubwa ya muziki wa kimataifa. Hadi sasa, waandaaji wa tamasha hilo hawajatoa tamko lolote rasmi kuhusu kujiondoa kwa Davido au hatua watakazochukua baada ya mabadiliko hayo.

Read More
 Chris Brown Aachiliwa kwa Dhamana ya Dola Milioni 6.7 London

Chris Brown Aachiliwa kwa Dhamana ya Dola Milioni 6.7 London

Msanii mashuhuri wa R&B kutoka Marekani, Chris Brown, ameachiwa kwa dhamana ya dola milioni 6.7 (takriban Shilingi bilioni 1) na mahakama mjini London baada ya kufunguliwa mashtaka ya kushambulia mtu bila sababu katika kilabu usiku mnamo mwaka 2023. Chris Brown mwenye umri wa miaka 36, ambaye ameshawahi kushinda tuzo ya Grammy, bado hajaombwa kutoa ombi la kukiri au kukataa shtaka hilo. Hata hivyo, masharti ya dhamana yake yanamruhusu kuanza ziara yake ya kimataifa mwezi ujao kama ilivyopangwa awali. Msanii huyo alikamatwa wiki iliyopita na baadaye kushtakiwa kwa kosa la kujeruhi kwa makusudi, kufuatia tukio ambalo inadaiwa alimshambulia mtayarishaji wa muziki kwa chupa ya kileo aina ya tequila. Jaji Tony Baumgartner alisema kuwa Brown anaruhusiwa kuendelea na ziara yake, ikijumuisha maonesho kadhaa nchini Uingereza, lakini lazima alipe dhamana hiyo ili kuhakikisha atahudhuria kesi yake mahakamani. Tukio hilo limezua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki na wanamuziki wenzake, huku wengi wakisubiri kwa hamu kuona hatima ya kesi hiyo inayomkabili mmoja wa wasanii wenye ushawishi mkubwa duniani.

Read More