Mahakama yatupilia mbali kesi iliyowasilishwa na Luba Events dhidi ya msanii Eddy Kenzo

Mahakama yatupilia mbali kesi iliyowasilishwa na Luba Events dhidi ya msanii Eddy Kenzo

Mwimbaji kutoka nchini Uganda Eddy Kenzo ana kila sababu ya kutabasamu baada ya mahakama kutupilia mbali kesi iliyowasilishwa na  Luba Events kumzuia kutumbuiza jijini Kampala. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Kenzo amewataarifu mashabiki zake kuwa ameruhusiwa tena kutumbuiza jijini Kampala kufuatia kesi ya Luba Events kukosa ushahidi wa kutosha mahakamani. Kenzo ambaye kwa sasa yupo nchini Marekani kwa ajili ya tuzo za Grammy aliwakilishwa mahakamani na mawakili wake Kabega Musa, pamoja na Faisal Balikurungi. Mnamo Novemba, Eddy Kenzo alipigwa marufuku kutumbuiza jijini Kampala baada ya promota Moses Lubuulwa wa Luba Events kumburuza mahakamani kwa kukiuka mkataba wa kuandaa tamasha la “Eddy Kenzo Festival” lililomalizika hivi karibuni. Luba alieleza kuwa Eddy Kenzo alimsaliti aliposhindwa kumhuisha kwenye mandalizi ya tamasha hilo licha ya kumlipa fedha za kufanya ziara za “Eddy Kenzo Festival” katika maeneo mbalimbali nchini Uganda ikiwemo Masaka, Bundibujo na maeneo mengine. Hata hivyo alifichua kwamba alipata hasara ya kiasi cha Kshs, million 27 alipoandaa Tamasha la Eddy Kenzo mwaka 2020 ambalo halikufanyika kwa sababu ya Covid 19.

Read More
 Eddy Kenzo ashtakiwa na Promota kwa kukiuka mkataba wa kufanya tamasha la muziki

Eddy Kenzo ashtakiwa na Promota kwa kukiuka mkataba wa kufanya tamasha la muziki

Mwanamuziki Eddy Kenzo ameburuzwa mahakamani kwa kufanya tamasha la muziki wikiendi iliyopita bila kumhusisha promota muziki nchini humo Luba Events. Kwa mujibu wa nyaraka za mahakama, Luba amewasilisha kesi mahakamani kumzuia msanii huyo haziweze kufanya matamasha ya muziki nchi Uganda hadi pale uamuzi wa kesi yake itakapotolewa. Promota huyo amedai kuwa alisaini mkataba wa kufanya onesho la muziki na Eddy Kenzo mwaka 2020 ambapo alienda mbali zaidi na kumlipa Ksh 3.9 millioni lakini wakati janga la Corona lilizuka walilazimika kuahirisha onesho lao. Luba amesema licha ya kumuandika Eddy Kenzo barua ya kumuonya asifanye tamasha hilo la muziki bila kumshirikisha, msanii huyo alikwenda kinyume na agizo lake na kufanya tamsha hilo mwenyewe. Hata hivyo amedai kuwa jaribio la kutatua sakata lake na Eddy Kenzo halikuzaa matunda, jambo ambalo lilimlazimu kumfungulia kesi mahakamani. Ikumbukwe Luba Events alikuwa miongoni mwa mapromota wa muziki waliofidiwa na serikali ya Uganda kwa hasara waliyopata wakati wa janga la Corona baada ya matamasha ya muziki kusitishwa ghafla.

Read More