Lydia Jazmine amaliza tofauti zake na Prodyuza Bushingtone
Msanii kutoka nchini Uganda Lydia Jazmine ameweka kando tofauti zake na prodyuza Bushingtone baada ya kuwa na ugomvi wa muda mrefu. Kulingana na taarifa za ndani, Wawili hao wameonekana wakiwa studio wakiandaa kazi mpya pamoja. “Wameelewana na tayari wako studio wanafanya kazi pamoja katika project kadhaa,” chanzo kimoja kimefichua. Jitihada za vyombo vya habari nchini Uganda kubaini ukweli wa taarifa hiyo hazikuzaa matunda ila ni jambo la kusubiriwa kutoka kwa duo zilikuwa bure kwa wakati wa vyombo vya habari. Utakumbuka mwaka 2010, Lydia Jazmine alitoka kimuziki kwa msaada wa Producer Bushingtone. Wawili hao walifanya kazi pamoja kwa muda hadi pale Lydia alipolamba dili nono la kutumbuiza katika mashindano ya Coke Studio nchini Kenya. Lakini wawili hao walikuja wakachanganya mapenzi na kazi kiasi cha kukosana vibaya, hivyo Lydia Jazmine akasajiliwa na mameneja kama R. Kampala, Ronnie Mulindwa na Mpaka Records ya Ykee Benda.
Read More