Mrembo wa Kenya Akataa Ndoa na Kuzaa Watoto

Mrembo wa Kenya Akataa Ndoa na Kuzaa Watoto

Socialite mwenye utata nchini Kenya, Lydia Wanjiru, amefunguka na kuweka wazi msimamo wake kuhusu maisha ya ndoa na uzazi, akisema wazi kuwa amechagua kuishi maisha bila kuolewa wala kuzaa watoto. Kupitia Instastory yake, Lydia amesema uamuzi huo ni wa hiari yake binafsi na umetokana na kutaka kuishi maisha yanayompa amani, uhuru na fursa ya kujijenga yeye mwenyewe bila shinikizo la kijamii. Mrembo huyo, ameeleza kuwa jamii imekuwa ikiweka matarajio makubwa kwa wanawake kuhusu ndoa na uzazi, jambo ambalo kwake halina nafasi. Amesisitiza kuwa kutokuwa na ndoa au watoto hakumaanishi kushindwa maishani, bali ni chaguo halali kama lilivyo kwa wale wanaochagua kuoa au kuzaa. Hii si mara ya kwanza kwa mrembo huyo kugonga vichwa vya habari. Mwishoni mwa mwaka jana, Lydia Wanjiru alizua gumzo mtandaoni baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuongeza makalio, kitendo ambacho kiliripotiwa kumwacha na madhara makubwa kiafya. Kutokana na hali hiyo, alilazimika kuomba msaada kutoka kwa Wakenya ili kugharamia matibabu na kurejea katika hali ya kawaida.

Read More
 Mrembo wa Kenya Asema Hajakaa Chini kwa Wiki 5 Baada ya Kufanyiwa Upasuaji wa Kuongeza Makalio BBL

Mrembo wa Kenya Asema Hajakaa Chini kwa Wiki 5 Baada ya Kufanyiwa Upasuaji wa Kuongeza Makalio BBL

Mwanamitindo na mshawishi wa mitandao ya kijamii nchini Kenya, Lydia Wanjiru, amefichua kuwa hajakaa chini kwa zaidi ya wiki tano kufuatia upasuaji wa kuongeza makalio (BBL) alioufanyiwa hivi karibuni. Kupitia maelezo yake kwenye Instastory, Lydia amesema kuwa madaktari walimshauri kuepuka kukaa chini ili kutoleta madhara kwenye eneo lililotibiwa, hatua ambayo ni muhimu katika kipindi cha kwanza cha kupona. Mrembo huyo mwenye utata, amefafanua kuwa anaendelea kufuata maagizo hayo kwa uangalifu hadi atakapofikisha wiki sita, muda ambao ataruhusiwa kukaa kawaida bila kuhatarisha matokeo ya upasuaji wake. Hata hivyo amewashukuru mashabiki wake kwa ushirikiano na uvumilivu, akisema kuwa safari ya kupona imekuwa yenye changamoto lakini ana imani itakuwa na matokeo mazuri mara itakapokamilika.

Read More
 Lydia Wanjiru Akanusha Tetesi za Kurudiana na Ex Wake Frank Dosoo

Lydia Wanjiru Akanusha Tetesi za Kurudiana na Ex Wake Frank Dosoo

Mrembo maarufu mtandaoni nchini Kenya, Lydia Wanjiru, amekanusha uvumi unaosambaa mtandaoni ukidai kuwa amerudiana na mpenzi wake wa zamani, Frank Dosoo. Kupitia InstaStory yake, Lydia ameonekana kukanusha madai hayo kwa maneno makali, akisema kuwa anafurahia gossip kama wengine, lakini inapozidi mipaka inakuwa kero hasa pale ambapo watu wanatunga hadithi bila ushahidi. Amesisitiza kuwa katika ulimwengu wa sasa ambapo kesi za kisheria ni jambo la kawaida, ni muhimu watu kuzingatia ukweli na kuwa na ushahidi kabla ya kusambaza taarifa. Mrembo huyo ameongeza kuwa madai ya kuonekana Kisumu akiwa na mtu fulani katika klabu moja ya usiku ni ya uongo, akibainisha kuwa hakuna hata picha au video inayoonyesha tukio hilo. Kauli hiyo imezima tetesi zilizokuwa zikienea mitandaoni kwamba wawili hao wamefufua tena mahusiano yao, huku mashabiki wake wakimsifia kwa jinsi alivyochukua hatua ya kuweka wazi ukweli na kuepuka drama za mtandaoni.

Read More
 Lydia Wanjiru Asema Kuishi na Mwanaume Maisha Yote ni Kifungo

Lydia Wanjiru Asema Kuishi na Mwanaume Maisha Yote ni Kifungo

Digital creator Lydia Wanjiru amejitokeza na mtazamo wa kipekee kuhusu maisha ya wanandoa, akisema kuwa kuishi na mwanaume chini ya paa moja ni sawa na hukumu ya maisha. Alisisitiza kwamba haiingii akilini kuona wanandoa wote wakirudi nyumbani kwa nyumba moja kila siku, kuanzia Januari hadi Desemba, bila hata nafasi ya kubadilisha mazingira. Wanjiru aliongeza kuwa wazo hilo kwake linaonekana la kuchosha na lenye kubana uhuru wa mtu binafsi, hasa kwa kizazi cha sasa kinachothamini sana nafasi ya binafsi na uhuru wa kufanya mambo kwa wakati unaotaka. Kauli yake imezua maoni mseto kutoka kwa wafuasi wake. Wapo waliomuunga mkono wakisisitiza kwamba ndoa kwa kweli si rahisi na changamoto zake mara nyingi hufichwa, huku wengine wakimkosoa wakidai mtazamo wake unaonyesha kutokuelewa maana ya upendo na uvumilivu katika maisha ya ndoa. Mjadala huo umeendelea kuchochea hisia kali mtandaoni, ambapo baadhi ya watu wameliona wazo la Wanjiru kama taswira ya kizazi kipya kinachoona ndoa kama mzigo, huku wengine wakisisitiza kwamba maisha ya kila siku chini ya paa moja ni fursa ya kujenga uhusiano wa kudumu.

Read More