Maandy Amlinganisha Willy Paul na Michael Jackson Baada ya Show Kali
Rapa wa kike kutoka nchini Kenya, Maandy, amezua mshangao na gumzo mtandaoni baada ya kumsifia msanii Willy Paul kufuatia tamasha lake alilohudhuria mwishoni mwa wiki. Kupitia mitandao ya kijamii, Maandy ameeleza kuwa amebaki na mshangao mkubwa kutokana na kiwango cha umahiri alichokiona jukwaani, akimfananisha Willy Paul na Michael Jackson kwa uwezo wake wa kuimba na kucheza kwa usahihi na nguvu kubwa. Maandy amesema kuwa Willy Paul amethibitisha kuwa ni mmoja wa wasanii wanaojituma zaidi nchini humo kwa kujenga maonesho ya kiwango cha juu kinachovutia mashabiki. Ameongeza kuwa ubora wa uchezaji wake, sauti thabiti na uwezo wa kumiliki jukwaa vinamtofautisha na wengi katika muziki wa Afrika Mashariki. Kauli hiyo imezua maoni mseto mtandaoni, baadhi ya mashabiki wakikubaliana na sifa hizo huku wengine wakidai kuwa kulinganisha msanii huyo na Michael Jackson ni hatua kubwa.
Read More