Maandy Afunguka: Sitaki Mwanaume Mgonjwa Kila Mara!

Maandy Afunguka: Sitaki Mwanaume Mgonjwa Kila Mara!

Msanii maarufu wa muziki wa hip hop nchini Kenya, Maandy, amezua gumzo mitandaoni baada ya kufichua wazi msimamo wake kuhusu aina ya mahusiano anayoyapendelea. Akizungumza kupitia mahojiano ya hivi karibuni, Maandy alisema hapendi kujiingiza kwenye mahusiano yenye changamoto nyingi, hasa yale ambayo kila mara yanakuwa na matatizo ya kiafya. Alisisitiza kuwa hawezi kuwa na mwenzi ambaye mara kwa mara anakumbwa na maradhi, akieleza kuwa hali kama hiyo humvunjia nguvu na kuathiri utulivu wa uhusiano. “Kwa kweli sipendi mahusiano ya mashida. Kwanza, sipendi mtu anayeumwa kila mara,” alisema msanii huyo kwa msisitizo. Kauli hiyo imezua hisia mseto miongoni mwa mashabiki wake. Wapo waliomuunga mkono wakisema kila mtu ana haki ya kuweka vigezo anavyovipenda kabla ya kuingia kwenye uhusiano, na wengine wakimpongeza kwa uaminifu wake. Hata hivyo, sehemu ya wafuasi walionekana kutokubaliana naye, wakitafsiri maneno hayo kama ukosefu wa huruma kwa watu wanaopitia changamoto za kiafya. Maandy, anayejulikana kwa vibao vyake vya mitindo ya uhalisia na ujumbe wa moja kwa moja, mara nyingi hutumia muziki wake kuzungumzia masuala ya mapenzi, mitindo ya maisha, na changamoto za kijamii. Kauli yake ya hivi karibuni imeonesha kuwa hata katika maisha yake binafsi, anashikilia misimamo thabiti kuhusu kile anachokubali na kukikataa kwenye mapenzi.

Read More
 Maandy aachia rasmi EP yake mpya Baddies Need Love

Maandy aachia rasmi EP yake mpya Baddies Need Love

Mwanamuziki kutoka nchini Kenya, Maandy ameachia rasmi EP yake mpya iitwayo ‘Baddies Need Love’ EP hiyo yenye jumla ya ngoma tano za moto. ina kolabo tatu kutoka kwa wasanii kama Charisma, Okello Max, Watendawili, na Ywaya Tajiri. ‘Baddies Need Love EP’ ina ngoma kama Ficha, Decide, Si kawaida, Mnoma na Baddies Need Love yenye imebeba jina la EP. EP hiyo ambayo imetayarishwa na maprodyuza kama Metro, Suka Doba na Sirav, inapatikana kwenye majukwaa yote ya muziki (digital platforms). EP mpya ya Maandy inaashiria maendeleo makubwa katika safari yake ya usanii, ikichanganya mitindo mbalimbali ya muziki na sauti bunifu zinazodhihirisha ukuaji wake kama msanii.

Read More
 Maandy azima tetesi za kutoka kimapenzi na Breeder LW

Maandy azima tetesi za kutoka kimapenzi na Breeder LW

Rapa Maandy kwa mara nyingine amekanusha madai yote kwamba yeye na msanii Breeder LW ni wapenzi. Kupitia ukurasa wake wa Instagram akiwajibu mashabiki zake waliokuwa wakidhani kwamba wanachumbiana, Maandy amethibitisha kwamba madai hayo hayana ukweli wowote. Hitmaker huyo wa ‘Ni Wetu’ ameeleza kwa kina kwamba mwanamke aliyepiga picha na Breeder LW wakiwa kwenye mahaba mazito, siku moja baada ya kumbukizi ya kuzaliwa kwake sio yeye. Maandy amedai kwamba alipata taarifa ya kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na rapa huyo kupitia simu za marafiki zake, huku akiwataka mashabiki kuacha tabia ya kumhusisha kimapenzi na Breeder LW ikizingatiwa kuwa hakuna kitu kinaendelea kati yao.

Read More
 Msanii Maandy awachana Ma-Dejaay wa Kenya kwa uzembe

Msanii Maandy awachana Ma-Dejaay wa Kenya kwa uzembe

Msanii wa kike nchini Maandy amewatolea uvivu madejaay wa Kenya kwa kuwa na uzembe kwenye utendaji kazi wao wa kucheza nyimbo za wasaniii wa humu nchini. Kupitia instastory yake amesema madejaay wamekuwa kizingiti wa kupeleka muziki Kenya kimataifa licha ya mchekeshaji Eric Omondi kujitoa mhanga kupigania tasnia ya muziki nchini kwa kushinikiza asilimia 75 za nyimbo za Kenya zipigwe kwenye vyombo vya habari. Hitmaker huyo wa “We ni Wetu” amesema licha ya wasanii kuachia nyimbo mpya kila kuchao bila kupoa madejaay wamekuwa wakicheza nyimbo za zamani kwenye Playlists zao kiasi cha kupitwa na vituo vya radio ambavyo vimekuwa mstari wa mbele kucheza nyimbo mpya za wasanii tofauti na madj ambao wamekuwa wakilaza damu kwenye kazi zao. Hata hivyo amemalizia kwa kusema kuwa madeejay watano ndio anawaheshimu kwa utendaji kazi wao nchini huku akiwataja wengine waliosalia kama mzigo kwenye kiwanda cha muziki kwa kuwa hawana uzalendo wa kushabikia muziki wa Kenya. “I want to free Kenyan DJ’s from the same playlist so much great new music has been released over the past year !! Mko lazy sana sanaaa!!! I only like 5 DJ’s ,hao wengine apana!!! You are the biggest disconnect. Do better. Even radio bumps new music immediately its out.” Ameandika.

Read More
 MAANDY AWAJIBU WANAODAI ANATOKA KIMAPENZI NA MAPRODYUZA

MAANDY AWAJIBU WANAODAI ANATOKA KIMAPENZI NA MAPRODYUZA

Msanii wa kike nchini Maandy amewajibu wanaodai kuwa mafanikio yake kimuziki yametokana na yeye kutoka kimapenzi na maprodyuza wa muziki. Kupitia ukurasa wake wa Instagram hitmaker huyo wa ngoma ya “By The Way” ameonakana kukasirishwa na wanaomema vibaya kwa kusema kwamba tuhuma hizo hazina ukweli wowote bali zimeibuliwa na watesi wake ambao wanalenga kumuharibia jina. Mrembo huyo ameenda mbali zaidi na kusema kwamba kama kweli  angekuwa anajiuza kimwili kwa maprodyuza angeshapeleka muziki wake kimataifa kitambo. “Huko clock app Wanasema Nagawa mbaya . If I was to use my body to get ahead , ningekua Grammies nikipigania space na Beyoncé ,si hapa ungwaro 😮‍💨😮‍💨 To the producers I’ve worked with kindly mark register hapa tuone mko wangapi 😂😂😂😂”, Aliandika Instagram. Hii si mara ya kwanza kwa Maandy kuzushiwa taarifa za aina hii kwani kipindi cha nyuma alidaiwa kutoka kimapenzi na rapa Breeder LW, madai ambayo aliyakanusha vikali.

Read More
 MAANDY AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA MEJJA

MAANDY AKANUSHA KUTOKA KIMAPENZI NA MEJJA

Female rapper kutoka Kenya, Maandy amepuzilia mbali uvumi wa muda mrefu kuwa anatoka kimapenzi na Mejja. Akipiga stori na Podcast ya Nicholas Kioko kwenye mtandao wa youtube, Maandy amekanusha madai hayo kwa kusema kwamba uhusiano wake na msanii huyo ni wa kirafiki tu na kwa sasa anafurahia maisha yake akiwa hana mpenzi yaani single! Hitmaker huyo ngoma ya “By The Way” amesema licha ya kusumbuliwa na wanaume wengi, kwa sasa hataki kukurupuka kuingia kwenye mahusiano ya kimapenzi kutokana na yeye kujikita zaidi katika muziki wake. Uvumi wa Maandy kutoka kimapenzi na Mejja ulianza miezi kadhaa iliyopita baada ya wawili hao kuonekana wakiwa pamoja studio waki-vibe na mdundo wa singo yao mpya. Kwa sasa Maandy anafanya vizuri na wimbo wake uitwao Ka Unaweza aliomshirikisha Mejja, wimbo ambao una zaidi ya Views laki 2 youtube ndani kipindi cha siku 2 tangu kuachiwa kwake.

Read More