Manchester City Kumnasa Kiungo Chipukizi wa Norway kwa Shilingi Bilioni 2

Manchester City Kumnasa Kiungo Chipukizi wa Norway kwa Shilingi Bilioni 2

Klabu ya Manchester City ipo katika hatua za mwisho kukamilisha usajili wa kiungo wa kati kutoka Norway, Sverre Halseth Nypan, kwa ada ya uhamisho inayokadiriwa kuwa Euro milioni 15, sawa na takribani Shilingi bilioni 2.1 za Kenya. Nypan, ambaye ana umri wa miaka 18, anatokea katika klabu ya Rosenborg BK ya Norway, ambako amecheza tangu mwaka 2022. Katika kipindi hicho, amehusika kwenye michezo 62 na kufunga mabao 14, akionyesha kiwango cha juu licha ya umri wake mdogo. Kinda huyo anatajwa kuwa mmoja wa vipaji bora zaidi barani Ulaya kwa sasa, na uwezo wake wa kusoma mchezo, kupiga pasi za mwisho, na kudhibiti kasi ya mchezo umevutia macho ya kocha Pep Guardiola. Manchester City wanapanga kumuingiza kijana huyo katika mpango wa muda mrefu wa kukuza vipaji, huku uwezekano wa kumtoa kwa mkopo ili kupata uzoefu wa ligi kubwa ukiwa bado wazi. Ingawa hakuna tangazo rasmi lililotolewa, taarifa kutoka kwa vyanzo vya karibu na klabu zote mbili zinaeleza kuwa mazungumzo yako katika hatua za mwisho, na usajili huo unaweza kutangazwa rasmi wakati wowote.

Read More
 Crystal Palace Yaandika Historia kwa Kuitandika Manchester City na Kutwaa Kombe la FA

Crystal Palace Yaandika Historia kwa Kuitandika Manchester City na Kutwaa Kombe la FA

Katika moja ya matukio ya kushangaza zaidi kwenye historia ya soka ya Uingereza, Crystal Palace waliibuka mabingwa wa Kombe la FA kwa mara ya kwanza tangu klabu hiyo ianzishwe zaidi ya miaka 120 iliyopita, baada ya kuichapa Manchester City bao 1-0 katika Uwanja wa Wembley mbele ya maelfu ya mashabiki. Mchezo huo uligubikwa na kasi, presha na kiwango cha hali ya juu, lakini lilikuwa ni goli la mapema la Eberechi Eze katika dakika ya 16 lililoamua hatima ya mechi. Eze alimalizia kwa ustadi mkubwa pasi ya chini kutoka kwa Daniel Muñoz, baada ya kushirikiana kwa kasi na Mateta katika mfululizo wa pasi safi kwenye eneo la hatari la City. Licha ya City kumiliki mpira kwa zaidi ya asilimia sabini na saba, hawakuweza kuvunja ukuta imara wa Palace, huku kipa Dean Henderson akicheza kwa kiwango cha juu na kuokoa mashambulizi kadhaa hatari  ikiwemo penalti ya Omar Marmoush na shuti kali la Jeremy Doku. Kocha wa Palace, Oliver Glasner, ambaye alichukua timu katikati ya msimu, sasa ameweka jina lake kwenye vitabu vya historia kwa kuwa kocha wa kwanza kutoka Austria kutwaa Kombe la FA. Akizungumza baada ya mchezo, Glasner alisema:  “Tulihitaji kuwa wakamilifu leo, na kwa kweli wachezaji walionyesha umoja, nidhamu na moyo mkubwa. Huu ni ushindi wa kila mmoja wetu.” Kwa Manchester City ya Pep Guardiola, kipigo hicho kimehitimisha msimu bila kutwaa taji lolote jambo ambalo halijawahi kutokea tangu msimu wa 2016/17. Licha ya kufanya mashambulizi 23, ukosefu wa ufanisi na umakini katika nafasi muhimu uliwagharimu. Guardiola alikiri kuwa walikosa makali: “Tulimiliki mpira, lakini hatukufanya maamuzi mazuri katika eneo la mwisho. Palace walijipanga vyema, hongera kwao.” Kwa ushindi huu, Crystal Palace wamejihakikishia tiketi ya moja kwa moja ya kushiriki Ligi ya Europa msimu ujao hatua kubwa kwa klabu ambayo wengi walidharau uwezo wake msimu huu. Mashabiki waliokuwa Wembley walisherehekea kwa hamasa kubwa, huku wakishuhudia timu yao ikiandika historia

Read More
 Arsenal yaibamiza Manchester City magoli 5-1 huku Man United ikikubali kichapo Old Trafford

Arsenal yaibamiza Manchester City magoli 5-1 huku Man United ikikubali kichapo Old Trafford

Klabu ya Arsenal iliibamiza Manchester city kipigo cha magoli matano kwa moja kwenye mechi ya ligi nchini England iliyochezwa leo ugani Emirates. Magoli ya Arsenal yalifungwa na Martin Odergard, Thomas Partey, Myles Lewis Skelly, Kai Havertz na Ethan Nwaneri dakika ya 2, 56, 62, 76 na 90+3 huku Earling Haaland akifungia Manchester city bao pekee la kufutia machozi dakika ya 55. Kwa matokeo hayo Arsenal anashikilia nafasi ya pili kwa pointi 50 nyuma ya vinara Liverpool ambao wana pointi 56 kwenye msimamo wa ligi kuu England. Manchester city iko katika nafasi ya nne na pointi ya 41. Kwengineko Manchester United imekubali kichapo cha mabao 2-0 kutoka kwa Crystal Palace katika dimbani la Old Trafford. Mabao ya mawili ya Jean Mateta dakika ya 64 na 89 yalitosha kabisa kuharibu wikiendi ya vijana wa Ruben Amorin, Manchester United iko nafasi ya 13 ikiwa na alama 29 baada ya michezo 24 kwenye Ligi Kuu ya Uingereza EPL Kwenye matokeo mengine iliyochezwa hii leo, Totenham Hotspurs akiwa ugenini dhidi ya Brentford alipata ushindi wa magoli mawili bila jibu. Magoli ya Spurs yalifungwa na Vitaly Janelt ambaye alijifunga dakika ya 29 na Paper  Matar Sarr dakika ya 87. Kwa matokeo hayo, Spurs anashikilia nafasi 14 ya na pointi 27 nyuma ya Brentford ambao wanashikilia nafasi 11 ya na pointi 31 kwenye msimamo wa ligi kuu nchini England.

Read More