Smady: ‘Beat za Kenya Hazivutii Mashabiki, Tunalazimika Kwenda Jamaica!’
Mwanachama wa kundi la muziki la Mbogi Genje, Smady, amefunguka kuhusu sababu inayowafanya wasanii wengi wa Kenya kupendelea kutumia beat za mtindo wa dancehall kutoka Jamaica katika nyimbo zao. Akipiga stori na Kasa Boss, Smady amesema hali hiyo inachangiwa na changamoto zinazowakabili baadhi ya maproducer nchini humo katika kutengeneza beat zenye ubora wa juu. Kwa mujibu wa Smady, wasanii wengi hulazimika kutafuta beat kutoka nje au kutumia midundo iliyoathiriwa na dancehall ya Jamaica kwa sababu inakuwa tayari ina ubora na mvuto unaoweza kuvutia mashabiki. Msanii huyo amesema kuwa sekta ya muziki nchini Kenya bado ina nafasi kubwa ya kuboresha upande wa utayarishaji wa muziki, hasa katika ubunifu na ubora wa beat.
Read More