Mke wa Mkubwa Fella Awajibu Waliomsema Vibaya Mume Wake

Mke wa Mkubwa Fella Awajibu Waliomsema Vibaya Mume Wake

Mke wa Mkubwa Fella amejibu vikali watu waliomsema vibaya mume wake wakati alipokuwa akipitia kipindi kigumu cha kiafya. Kupitia instastory yake, mwanamama huyo amechapisha video inayoonyesha yeye na Mkubwa Fella wakifurahia kinywaji, huku hali ya Mkubwa Fella ikionekana kuimarika na kuwa nzuri. Katika video hiyo, wawili hao wameonekana wakiwa na furaha na tabasamu, ishara iliyowafanya wengi kudhani kuwa afya ya Mkubwa Fella inaendelea kuimarika siku hadi siku. Hatua hiyo imetafsiriwa na wengi kama ujumbe mzito kwa wale waliokuwa wakimsema vibaya Mkubwa Fella na hata kumdhihaki kipindi alipokuwa akiomba msaada wa kifedha kutokana na ugonjwa uliomkumba. Ikumbukwe kuwa, baada ya Mke wa Mkubwa Fella kujitokeza hadharani kuomba msaada, baadhi ya watu mitandaoni walimchamba vikali, huku wengine wakifika hatua ya kumtakia mume wake kifo, jambo lililozua hasira na masikitiko makubwa miongoni mwa Watanzania.

Read More
 Mke wa Mkubwa Fella Atishia Kuanika Siri Nzito

Mke wa Mkubwa Fella Atishia Kuanika Siri Nzito

Mke wa meneja maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Mkubwa Fella, amezua gumzo kubwa mitandaoni baada ya kutoa kauli kali zinazolenga watu anaodai wameanza kumchokonoa na kumshambulia kwa maneno. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Sweet Fella amefunguka kwa hasira akisema amekuwa akivumilia kwa muda licha ya kushambuliwa mara kwa mara. Amesema kuwa alifichua jambo dogo tu na watu wameendelea kumsema kwa zaidi ya wiki moja, akionya kuwa endapo atazungumza tena kwa mara ya pili, basi mambo makubwa yatawekwa wazi na mjadala huo utadumu kwa muda mrefu. Katika ujumbe wake, amewataka wakosoaji waache kujistukia na wasikilize kwa makini anachokizungumza, akisisitiza kuwa baadhi yao hawataki kusikia ukweli kwa kujifanya masikio yao ni mazito. Kauli ya Sweet Fella imekuja baada ya baadhi ya watu kumkosoa wakidai alitumia vibaya mchango uliotolewa na Diamond Platnumz kwa kula bata Dubai na kumtelekeza mgonjwa, hatua ambayo ilimpelekea hitmaker huyo wa Sasampa kusitisha msaada wa matibabu.

Read More
 Mke wa Mkubwa Fella Asema Wasanii Wamemkibia Mume wake Baada ya Kuugua

Mke wa Mkubwa Fella Asema Wasanii Wamemkibia Mume wake Baada ya Kuugua

Mke wa Mkubwa Fella, ambaye ndiye meneja wa wasanii wa Bongo Fleva, amefunguka kuhusu hali ya afya ya mume wake akidai kuwa kwa sasa ametelekezwa na wasanii wengi aliowahi kuwasaidia. Kupitia ukurasa wake Instagram, mke huyo kwa jina Sweet Fella, amesema amekuwa karibu na mume wake akimhudumia, akisisitiza kuwa jukumu hilo ni ibada kwake kama mke. Ameeleza kuwa licha ya mchango mkubwa alioutoa Mkubwa Fella katika kukuza na kusimamia vipaji mbalimbali, hakuna msanii aliyejitokeza kuulizia hali yake ya sasa. Aidha, ametoa shukrani kwa marafiki na wanafamilia wanaoendelea kusimama nao katika kipindi hiki kigumu, akisema msaada wao ni wa thamani kubwa na Mungu atawalipa kwa wema wao. Hata hivyo, ameongeza kuwa anaendelea kumuombea mume wake apone haraka na kusisitiza kuwa Mkubwa Fella atazungumza mwenyewe kuhusu hali yake mara tu atakapopata nafuu kiafya.

Read More