Mke wa Mkubwa Fella, ambaye ndiye meneja wa wasanii wa Bongo Fleva, amefunguka kuhusu hali ya afya ya mume wake akidai kuwa kwa sasa ametelekezwa na wasanii wengi aliowahi kuwasaidia.
Kupitia ukurasa wake Instagram, mke huyo kwa jina Sweet Fella, amesema amekuwa karibu na mume wake akimhudumia, akisisitiza kuwa jukumu hilo ni ibada kwake kama mke. Ameeleza kuwa licha ya mchango mkubwa alioutoa Mkubwa Fella katika kukuza na kusimamia vipaji mbalimbali, hakuna msanii aliyejitokeza kuulizia hali yake ya sasa.
Aidha, ametoa shukrani kwa marafiki na wanafamilia wanaoendelea kusimama nao katika kipindi hiki kigumu, akisema msaada wao ni wa thamani kubwa na Mungu atawalipa kwa wema wao.
Hata hivyo, ameongeza kuwa anaendelea kumuombea mume wake apone haraka na kusisitiza kuwa Mkubwa Fella atazungumza mwenyewe kuhusu hali yake mara tu atakapopata nafuu kiafya.