Morocco Kuvaana na Zambia Leo Katika Mechi Muhimu ya Kundi A – CHAN
Washindi mara mbili wa taji la Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), Morocco, watakuwa na lengo la kurejea kwenye njia ya ushindi leo jioni watakapomenyana na Zambia katika mechi ya Kundi A itakayopigwa kwenye uwanja wa Nyayo, Nairobi. Atlas Lions walizindua kampeni yao kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Angola, lakini wakapoteza mchezo wa pili kwa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Kenya siku ya Jumapili. Kwa upande mwingine, Zambia bado inawinda ushindi wake wa kwanza, baada ya kupoteza mechi zake zote mbili dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Angola. Morocco, ambao wamelenga kufuzu kwa hatua ya robo fainali, wanahitaji ushindi ili kuweka hai matumaini yao ya kuendelea kushiriki mashindano haya. Nayo Zambia, ambayo inaburuza mkia bila alama yoyote, inahitaji ushindi ili kuhuisha matumaini ya kusalia katika michuano hiyo. Katika mechi nyingine ya kundi hilo hilo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo itachuana na Angola katika uwanja wa Kasarani kuanzia saa mbili usiku. Mchuano huu pia ni wa muhimu katika kuamua hatma ya timu zitakazofuzu kwa hatua inayofuata. Baada ya raundi tatu za michuano ya Kundi A, Kenya inaongoza kwa alama saba, ikifuatiwa na Angola yenye pointi nne. DRC iko nafasi ya tatu kwa pointi tatu, Morocco ya nne, huku Zambia ikiwa mkiani bila pointi yoyote.
Read More