Morocco na Misri Karibu na Tiketi ya Kombe la Dunia

Morocco na Misri Karibu na Tiketi ya Kombe la Dunia

Morocco na Misri zina nafasi kubwa ya kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia mwaka 2026, kufuatia mwenendo wao mzuri katika mechi za kufuzu zinazoendelea barani Afrika. Mashindano haya ya kufuzu, yaliyoanza mwezi Novemba 2023, yanatarajiwa kukamilika mwezi ujao, huku raundi nne muhimu zikiwa zimebaki. Katika mfumo wa kufuzu wa Afrika, ni washindi wa makundi tisa pekee watakaopata nafasi ya moja kwa moja ya kushiriki fainali hizo zitakazofanyika Marekani, Canada na Mexico. Timu nyingine nne bora zitakazomaliza katika nafasi ya pili zitapata nafasi ya pili kupitia mchujo wa mabara unaotarajiwa kuchezwa Novemba mwaka huu. Misri na Morocco, ambazo zimekuwa na kampeni imara hadi sasa, huenda zikajikatia tiketi zao moja kwa moja kabla ya raundi ya mwisho, iwapo zitapata ushindi katika mechi zao za wiki hii. Ushindi huo utazifanya ziendelee kuongoza makundi yao kwa tofauti ya alama isiyoweza kufikiwa na wapinzani wao katika mechi zilizobaki. Timu nyingine kama Cape Verde, Comoro na Sudan bado zina nafasi ya kufuzu, japo zinahitaji ushindi katika mechi zao zilizosalia. Kwa upande mwingine, Nigeria, ambayo ni moja ya mataifa yaliyotarajiwa kufanya vizuri, inakumbwa na presha kubwa na huenda ikaondolewa mapema ikiwa haitarejea kwenye mstari wa ushindi.

Read More
 Morocco Yaizamisha Madagascar 3-2, Yatwaa Ubingwa wa CHAN

Morocco Yaizamisha Madagascar 3-2, Yatwaa Ubingwa wa CHAN

Timu ya taifa ya Morocco (Atlas Lions) imeandika historia tena katika anga la soka barani Afrika baada ya kutwaa taji lake la tatu la Mashindano ya Soka kwa Wachezaji wa Ndani ya Afrika (CHAN), kwa kuichapa Madagascar kwa mabao 3-2 katika fainali ya kusisimua iliyopigwa katika Uwanja wa Kimataifa wa Kasarani, Nairobi. Morocco, ambao waliwahi kutwaa taji hili mwaka 2018 na 2020, walionyesha kiwango cha juu licha ya upinzani mkali kutoka kwa Madagascar waliocheza kwa ari kubwa wakitafuta taji lao la kwanza. Nyota wa mchezo huo alikuwa mshambulizi mahiri Oussama Lamlaoui, ambaye alitikisa nyavu mara mbili, ikiwa ni pamoja na bao maridadi alilofunga kutoka umbali wa yadi 40. Bao hilo la kipekee liliibua shangwe uwanjani na kumfanya kumaliza mashindano akiwa mfungaji bora kwa jumla ya mabao sita. Ushindi huo haukuwa tu fahari kwa Morocco bali pia ulijumuisha zawadi nono ya pesa taslimu, shilingi milioni 453, ilhali washindi wa pili, Madagascar, waliyoonyesha kandanda safi, waliondoka na kitita cha shilingi milioni 155. Fainali hiyo ya kuvutia ilihudhuriwa na viongozi wa juu wa soka na serikali, akiwemo Rais wa Kenya William Ruto, Rais wa Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA) Gianni Infantino, na Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) Patrice Motsepe. Uwepo wao uliongeza hadhi ya tukio hilo na kudhihirisha maendeleo ya soka barani Afrika.

Read More
 Morocco na Madagascar Wafuzu Fainali za CHAN

Morocco na Madagascar Wafuzu Fainali za CHAN

Timu za taifa za Morocco na Madagascar zitarudi jijini Nairobi kucheza fainali za mashindano ya Afrika kwa wachezaji wa nyumbani (CHAN), baada ya kushinda mechi zao za nusu fainali dhidi ya Senegal na Sudan mtawalia. Morocco ilibandua mabingwa watetezi Senegal kwa mikwaju ya penati baada ya mchezo kumalizika kwa sare ya bao 1-1 katika muda wa kawaida na ziada. Katika raundi ya penati, Morocco ilifunga mikwaju mitano, huku Senegal ikitumia mitatu pekee, hivyo kuipa Morocco tiketi ya kuingia fainali. Madagascar ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Sudan katika dakika ya 116, ikiwafunga Sudan na kujiweka nafasi ya kucheza fainali dhidi ya Morocco. Sudan itacheza mechi ya kuwania nafasi ya tatu dhidi ya Senegal. Fainali baina ya Morocco na Madagascar itachezwa Jumamosi uwanjani Kasarani jijini Nairobi, baada ya mechi ya kuwania nafasi ya tatu kati ya Sudan na Senegal itakayofanyika uwanjani Mandela nchini Uganda.

Read More
 Morocco Kuvaana na Zambia Leo Katika Mechi Muhimu ya Kundi A – CHAN

Morocco Kuvaana na Zambia Leo Katika Mechi Muhimu ya Kundi A – CHAN

Washindi mara mbili wa taji la Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), Morocco, watakuwa na lengo la kurejea kwenye njia ya ushindi leo jioni watakapomenyana na Zambia katika mechi ya Kundi A itakayopigwa kwenye uwanja wa Nyayo, Nairobi. Atlas Lions walizindua kampeni yao kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Angola, lakini wakapoteza mchezo wa pili kwa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Kenya siku ya Jumapili. Kwa upande mwingine, Zambia bado inawinda ushindi wake wa kwanza, baada ya kupoteza mechi zake zote mbili dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Angola. Morocco, ambao wamelenga kufuzu kwa hatua ya robo fainali, wanahitaji ushindi ili kuweka hai matumaini yao ya kuendelea kushiriki mashindano haya. Nayo Zambia, ambayo inaburuza mkia bila alama yoyote, inahitaji ushindi ili kuhuisha matumaini ya kusalia katika michuano hiyo. Katika mechi nyingine ya kundi hilo hilo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo itachuana na Angola katika uwanja wa Kasarani kuanzia saa mbili usiku. Mchuano huu pia ni wa muhimu katika kuamua hatma ya timu zitakazofuzu kwa hatua inayofuata. Baada ya raundi tatu za michuano ya Kundi A, Kenya inaongoza kwa alama saba, ikifuatiwa na Angola yenye pointi nne. DRC iko nafasi ya tatu kwa pointi tatu, Morocco ya nne, huku Zambia ikiwa mkiani bila pointi yoyote.

Read More
 Kenya Yaanza Vyema Mashindano ya Dunia ya Wavu wa Ufukweni Nchini Morocco

Kenya Yaanza Vyema Mashindano ya Dunia ya Wavu wa Ufukweni Nchini Morocco

Timu ya taifa ya mpira wa wavu wa ufukweni ya wanaume imeanza kwa kishindo kampeni yake kwenye Mashindano ya Dunia ya Mpira wa Wavu wa Ufukweni yanayoendelea mjini Martiak, Morocco. Wachezaji wa Kenya, Brian Melly na Wilson Waibei, walionesha ubabe wao walipoibuka na ushindi wa seti mbili bila jibu dhidi ya wapinzani wao kutoka Burundi, Ishimwe na Ndayisaba, kwa alama 21-14 na 21-15 katika mechi ya kundi A. Hata hivyo, timu hiyo pia ilitoka sare na wenyeji Morocco katika mechi ya pili ya kundi hilo. Wachezaji wengine wa timu ya wanaume kutoka Kenya, Elphas Makuto na Jairus Kipkosgei, nao walitoa ushindani mkubwa kwa kutoka sare dhidi ya Ghana na Nigeria kwenye mechi zao za awali. Kwa upande wa wanawake, Kenya pia imetuma wakilishi wake kwenye mashindano hayo. Gaudencia Makokha na Sharlene Maywa wako katika kundi A pamoja na timu kutoka Nigeria na Burundi, ambapo wanatarajiwa kucheza mechi muhimu katika siku zijazo. Aidha, Mercy Iminza na Veronica Adhiambo watashuka uwanjani usiku wa leo kwenye kundi D wakikabiliwa na changamoto kutoka kwa timu za Nigeria na Mauritius. Mashindano haya ya dunia ni ya kiwango cha juu na yanatarajiwa kufikia kilele mwezi Novemba mwaka huu nchini Australia, ambako timu zitakazofanya vizuri zitajipatia nafasi ya kushiriki kwenye fainali hizo. Timu ya Kenya inaendelea kuonyesha dhamira ya kutwaa ushindi na kupeperusha vyema bendera ya taifa katika mchezo huu unaozidi kupata umaarufu barani Afrika na duniani kwa ujumla.

Read More
 Morocco yavuna billioni 3 Kombe la Dunia

Morocco yavuna billioni 3 Kombe la Dunia

Timu ya taifa ya Morocco imefanikiwa kuvuna jumla ya dola za Kimarekani milioni 25 sawa na Ksh. bilioni 3 baada ya kufanikiwa kumaliza nafasi ya nne kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar. Croatia walioshinda nafasi ya tatu wamejishindia dola milioni 27 sawa na Ksh. bilioni 3.3, mshindi wa pili kati ya Ufaransa na Argentina leo atavuna dola milioni 30 sawa na Ksh. bilioni 3.7 huku bingwa wa michuano akivuna dola milioni 42 sawa na Ksh. bilioni 5.2

Read More
 Ufaransa yatinga Fainali Kombe la Dunia 2022

Ufaransa yatinga Fainali Kombe la Dunia 2022

Mabingwa watetezi wa michuano ya Kombe la Dunia timu ya taifa ya Ufaransa imefanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo baada ya kuwazaba 2-0 Morocco Theo Hernandez wa ufaransa alipachika bao la kwanza katika dakika ya 5 ya mchezo huo huku mshambuliaji Randal Kolo Muani akipachika bao la pili na kufunga kitabu cha magoli katika dakika ya 79 ya mchezo na kufuta matumaini ya Morocco kucheza fainali ya kombe la dunia kwa mara ya kwanza. Morocco ambao ni wawakilishi pekee wa Bara la Afrika waliokuwa wamesalia kwenye michuano hiyo sasa wataisaka nafasi ya tatu kwa kuvaana na Croatia Ufaransa watajaribu kutetea taji lao mbele ya Argentina kwenye mchezo wa fainali siku ya Jumapili Desemba 18.

Read More
 Morocco yafuzu hatua ya mtoani Kombe la Dunia

Morocco yafuzu hatua ya mtoani Kombe la Dunia

Wawakilishi wengine wa Afrika kwenye michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea Qatar, Timu ya Taifa ya Morocco imefanikiwa kufuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo baada ya kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Canada kwenye mchezo wa mwisho wa kundi F. Morocco imefuzu wakiwa vinara wa kundi hilo baada ya kufikisha alama 7 wakifuatiwa na Croatia na kuwaacha Ubelgiji na Canada wakiyapa mkono wa kwaheri mashindano hayo makubwa zaidi kwa mchezo wa kandanda ulimwenguni. Morocco inakuwa timu ya pili kutoka Afrika kutinga hatua ya 16 bora baada ya Senegal kutangulia mapema.

Read More