Morocco Kuvaana na Zambia Leo Katika Mechi Muhimu ya Kundi A – CHAN

Morocco Kuvaana na Zambia Leo Katika Mechi Muhimu ya Kundi A – CHAN

Washindi mara mbili wa taji la Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN), Morocco, watakuwa na lengo la kurejea kwenye njia ya ushindi leo jioni watakapomenyana na Zambia katika mechi ya Kundi A itakayopigwa kwenye uwanja wa Nyayo, Nairobi. Atlas Lions walizindua kampeni yao kwa ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Angola, lakini wakapoteza mchezo wa pili kwa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Kenya siku ya Jumapili. Kwa upande mwingine, Zambia bado inawinda ushindi wake wa kwanza, baada ya kupoteza mechi zake zote mbili dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Angola. Morocco, ambao wamelenga kufuzu kwa hatua ya robo fainali, wanahitaji ushindi ili kuweka hai matumaini yao ya kuendelea kushiriki mashindano haya. Nayo Zambia, ambayo inaburuza mkia bila alama yoyote, inahitaji ushindi ili kuhuisha matumaini ya kusalia katika michuano hiyo. Katika mechi nyingine ya kundi hilo hilo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo itachuana na Angola katika uwanja wa Kasarani kuanzia saa mbili usiku. Mchuano huu pia ni wa muhimu katika kuamua hatma ya timu zitakazofuzu kwa hatua inayofuata. Baada ya raundi tatu za michuano ya Kundi A, Kenya inaongoza kwa alama saba, ikifuatiwa na Angola yenye pointi nne. DRC iko nafasi ya tatu kwa pointi tatu, Morocco ya nne, huku Zambia ikiwa mkiani bila pointi yoyote.

Read More
 Kenya Yaanza Vyema Mashindano ya Dunia ya Wavu wa Ufukweni Nchini Morocco

Kenya Yaanza Vyema Mashindano ya Dunia ya Wavu wa Ufukweni Nchini Morocco

Timu ya taifa ya mpira wa wavu wa ufukweni ya wanaume imeanza kwa kishindo kampeni yake kwenye Mashindano ya Dunia ya Mpira wa Wavu wa Ufukweni yanayoendelea mjini Martiak, Morocco. Wachezaji wa Kenya, Brian Melly na Wilson Waibei, walionesha ubabe wao walipoibuka na ushindi wa seti mbili bila jibu dhidi ya wapinzani wao kutoka Burundi, Ishimwe na Ndayisaba, kwa alama 21-14 na 21-15 katika mechi ya kundi A. Hata hivyo, timu hiyo pia ilitoka sare na wenyeji Morocco katika mechi ya pili ya kundi hilo. Wachezaji wengine wa timu ya wanaume kutoka Kenya, Elphas Makuto na Jairus Kipkosgei, nao walitoa ushindani mkubwa kwa kutoka sare dhidi ya Ghana na Nigeria kwenye mechi zao za awali. Kwa upande wa wanawake, Kenya pia imetuma wakilishi wake kwenye mashindano hayo. Gaudencia Makokha na Sharlene Maywa wako katika kundi A pamoja na timu kutoka Nigeria na Burundi, ambapo wanatarajiwa kucheza mechi muhimu katika siku zijazo. Aidha, Mercy Iminza na Veronica Adhiambo watashuka uwanjani usiku wa leo kwenye kundi D wakikabiliwa na changamoto kutoka kwa timu za Nigeria na Mauritius. Mashindano haya ya dunia ni ya kiwango cha juu na yanatarajiwa kufikia kilele mwezi Novemba mwaka huu nchini Australia, ambako timu zitakazofanya vizuri zitajipatia nafasi ya kushiriki kwenye fainali hizo. Timu ya Kenya inaendelea kuonyesha dhamira ya kutwaa ushindi na kupeperusha vyema bendera ya taifa katika mchezo huu unaozidi kupata umaarufu barani Afrika na duniani kwa ujumla.

Read More
 Morocco yavuna billioni 3 Kombe la Dunia

Morocco yavuna billioni 3 Kombe la Dunia

Timu ya taifa ya Morocco imefanikiwa kuvuna jumla ya dola za Kimarekani milioni 25 sawa na Ksh. bilioni 3 baada ya kufanikiwa kumaliza nafasi ya nne kwenye michuano ya Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar. Croatia walioshinda nafasi ya tatu wamejishindia dola milioni 27 sawa na Ksh. bilioni 3.3, mshindi wa pili kati ya Ufaransa na Argentina leo atavuna dola milioni 30 sawa na Ksh. bilioni 3.7 huku bingwa wa michuano akivuna dola milioni 42 sawa na Ksh. bilioni 5.2

Read More
 Ufaransa yatinga Fainali Kombe la Dunia 2022

Ufaransa yatinga Fainali Kombe la Dunia 2022

Mabingwa watetezi wa michuano ya Kombe la Dunia timu ya taifa ya Ufaransa imefanikiwa kutinga fainali ya michuano hiyo baada ya kuwazaba 2-0 Morocco Theo Hernandez wa ufaransa alipachika bao la kwanza katika dakika ya 5 ya mchezo huo huku mshambuliaji Randal Kolo Muani akipachika bao la pili na kufunga kitabu cha magoli katika dakika ya 79 ya mchezo na kufuta matumaini ya Morocco kucheza fainali ya kombe la dunia kwa mara ya kwanza. Morocco ambao ni wawakilishi pekee wa Bara la Afrika waliokuwa wamesalia kwenye michuano hiyo sasa wataisaka nafasi ya tatu kwa kuvaana na Croatia Ufaransa watajaribu kutetea taji lao mbele ya Argentina kwenye mchezo wa fainali siku ya Jumapili Desemba 18.

Read More
 Morocco yafuzu hatua ya mtoani Kombe la Dunia

Morocco yafuzu hatua ya mtoani Kombe la Dunia

Wawakilishi wengine wa Afrika kwenye michuano ya Kombe la Dunia inayoendelea Qatar, Timu ya Taifa ya Morocco imefanikiwa kufuzu hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo baada ya kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya Canada kwenye mchezo wa mwisho wa kundi F. Morocco imefuzu wakiwa vinara wa kundi hilo baada ya kufikisha alama 7 wakifuatiwa na Croatia na kuwaacha Ubelgiji na Canada wakiyapa mkono wa kwaheri mashindano hayo makubwa zaidi kwa mchezo wa kandanda ulimwenguni. Morocco inakuwa timu ya pili kutoka Afrika kutinga hatua ya 16 bora baada ya Senegal kutangulia mapema.

Read More