NACADA Yajibu Bien: “Sio Unafiki Bali Ni Hatua ya Kulinda Afya ya Umma”

NACADA Yajibu Bien: “Sio Unafiki Bali Ni Hatua ya Kulinda Afya ya Umma”

Mamlaka ya Kitaifa ya Kudhibiti Matumizi ya Dawa za Kulevya (NACADA) imejibu vikali matamshi ya msanii Bien wa kundi la Sauti Sol, aliyekosoa pendekezo la kuwapiga marufuku wasanii na watu mashuhuri kutangaza bidhaa za vileo. Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, NACADA imesisitiza kuwa hatua hiyo haifungamani na unafiki wa maadili wala juhudi za kukandamiza uhuru wa wasanii, bali inalenga kulinda afya ya umma hasa vijana, ambao ndio walio katika hatari zaidi ya kushawishika na ulevi kupitia ushawishi wa watu maarufu. Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya Bien kusema kuwa hatua hiyo ni unafiki na kwamba wasanii wana haki ya kujipatia kipato kupitia matangazo ya kibiashara. Hata hivyo, NACADA imetoa wito kwa wasanii kutumia ushawishi wao kuhamasisha maisha yenye afya na kutoa matumaini kwa jamii badala ya kushabikia bidhaa zinazoweza kuwa hatari kwa maisha ya wengi.

Read More
 Nviiri The Storyteller Aunga Mkono Marufuku ya Matangazo ya Pombe

Nviiri The Storyteller Aunga Mkono Marufuku ya Matangazo ya Pombe

Msanii Nviiri The Storyteller ameunga mkono pendekezo la Mamlaka ya Kudhibiti Matumizi ya Pombe na Dawa za Kulevya (NACADA) kuwapiga marufuku wasanii na watu maarufu kutangaza bidhaa za pombe. Kupitia ujumbe wake kwa umma, Nviiri amefichua kuwa aliwahi kushiriki kampeni ya matangazo ya pombe mtaani Kayole Jijini Nairobi, lakini baadaye alijutia uamuzi wake huo baada ya kugundua kuwa wakazi wa eneo hilo walihitaji zaidi chakula na fursa za maendeleo badala ya bidhaa za vileo. “Nilijihisi vibaya sana baadaye. Niliona wazi kuwa kile watu wale walihitaji si kileo, bali tumaini na njia za kujikwamua kimaisha,” alisema Nviiri. Msanii huyo ametoa wito kwa wasanii wenzake kuacha kufuata pesa kwa gharama ya maisha ya mashabiki wao, na badala yake kutumia ushawishi wao kwa njia inayojenga jamii. “Tuache kupotosha mashabiki wetu kwa matangazo yanayohatarisha afya na mustakabali wao. Tuna nguvu ya kushawishi na tuitumie kwa busara,” alisisitiza. Kauli ya Nviiri inakuja wakati NACADA ikisisitiza msimamo wake kuhusu athari za matangazo ya pombe yanayohusisha watu mashuhuri, ikisema kuwa yamechangia ongezeko la matumizi ya pombe miongoni mwa vijana.

Read More