Wyre, Nameless na Jua Cali kutengeneza bendi ya muziki

Wyre, Nameless na Jua Cali kutengeneza bendi ya muziki

Msanii mkongwe nchini, Wyre amedokeza mpango wa kuunda bendi ya muziki itakayojumuisha wasanii wa kizazi kipya pamoja na wa zamani. Kupitia ukurasa wake wa Twitter, amepost video akitoa tangazo hilo ambapo amesema wameungana na kutengeneza timu ya malejendari wa muziki. “Kuna nini jamani. Kwa kawaida sifanyi hivi. Imekuwa zaidi ya miaka 20 katika kufanya jambo hili la muziki na nadhani ni kuhusu wakati huu ambao umefika…. Unajua kila kitu kinafikia hatua hiyo ya kufika mwisho. “Kwa hivyo nimeamua.. Tumeamua kuwa tunaunda bendi ya wasanii wa kitambo,” Msanii huyo aliweka wazi hilo huku akihamishia kamera kwa wasanii wengine ambao ni Nameless na Jua Calie pamoja na Kenzo.

Read More
 Nameless awajibu kisomo wanaomshinikiza kupata mtoto wa kiume

Nameless awajibu kisomo wanaomshinikiza kupata mtoto wa kiume

Msanii nyota nchini Nameless amewajibu walimwengu wanaomshinikiza kuzaa mtoto wa kiume kama njia ya kudhihirisha uanaume wake katika jamii. Akimjibu shabiki mmoja aliyemtaka aweke mkakati wa kumpata mtoto wa kiume na mke wake Wahu kwenye mtandao wa Facebook, Nameless amesema anajivunia kuwa baba ya watoto wa kike na lengo lake kwa sasa ni kuwalea mabinti zake kwenye mazingira yatakayowapa fursa ya kuishi na watu vizuri. Hitmaker huyo wa “Teamo” amewataka mashabiki kuacha kasumba ya kufuata mila zilizopitwa na wakati na badala yake wakumbatie utandawazi kama njia mojawapo ya kuendana na nyakati zilizopo. “Tafuta kijana boss…..Your legacy…..We Africans”, Shabiki aliandika kwenye mtandao wa Facebook ambapo Nameless alishuka kwenye uwanja wa comment na kuandika “”Saa zingine tunajiangusha na traditions that are outdated. Let’s evolve buana” Ikumbukwe Nameless na Wahu ambao wamekuwa kwenye ndoa tangu mwaka 2005, kwa pamoja wamebarikiwa kuwapata mabinti watatu ambao ni Tumiso, Nyakio na Shiru ambaye alizaliwa juzi kati.

Read More
 Wahu na Nameless wapata mtoto wa kike

Wahu na Nameless wapata mtoto wa kike

Lejendari wa muziki nchini  Nameless  amethibitisha kuwa mke wake Wahu amejifungua mtoto wa kike. Nameless ameeleza furaha yake kupitia mitandao yake ya kijamii kwa Wahu kujifungua salama, akimshukuru Mungu pamoja na mashabiki zake ambao wamekuwa mstari wa mbele kuwaombea dua kwa kusema kuwa mke yupo tayari kwa majukumu ya kumlea mtoto wao Aidha amesema mtoto huyo wa kike ambaye amepewa jina la kumuenzi dada yake mkubwa kulingana na tamaduni za jamii ya Kikuyu, anaitwa Shiru. Ni hatua ambayo imepokelewa kwa furaha na mastaa wenzake kutoka Kenya ambao walitupia comment zao kwenye posti yake wakimtakia heri pamoja na mke wake Wahu. Huyu anakuwa mtoto wa tatu kwa Nameless na Wahu Kagwi ambao wametimiza miaka 17 wakiwa mume na mke ikizingatiwa tayari katika ndoa yao wamebahatika kupata watoto wawili, wote wakiwa wakike.

Read More
 Wahu na Nameless waweka wazi jinsia ya mtoto wao

Wahu na Nameless waweka wazi jinsia ya mtoto wao

Staa wa muziki nchini Wahu ameweka wazi jinsia ya mtoto wake wa tatu ambaye atazaliwa hivi karibuni. Kupitia ukurasa wake wa Instagram amechapisha video ya hafla ya utambulisho wa jinsia ya mtoto wao na kusindikiza na maneno yanayosomeka “BabaGalz Chairman honored, excited and ready for Duty! Ujumbe huo umetafsiri moja kwa moja na watumiaji wa mitandao ya kijamii kuwa Wahu na mume wake Nameless wanatarajia kumpata mtoto wa kike. Hata hivyo mashabiki na mastaa mbali mbali wamewapongeza wawili hao kwa hatua hiyo wakati huu wapo mbioni kumkaribisha mwanafamilia mwingine. Utakumbuka juzi kati taarifa zilisambaa mtandaoni zikidai kuwa huenda Wahu alijifungua kwa siri kutokana na jumbe alizokuwa anachapisha kwenye mtandao wake wa Instagram.

Read More
 ROBERT ALAI APINGA MSWADA WA NAMELESS KUTAKA BARABARA MOJA NAIROBI KUPEWA JINA LA E-SIR

ROBERT ALAI APINGA MSWADA WA NAMELESS KUTAKA BARABARA MOJA NAIROBI KUPEWA JINA LA E-SIR

Mwanablogu aliyegeukia siasa nchini Robert Alai amekosoa pendekezo la Nameless kutaka barabara moja jijini Nairobi lipewa jina la marehemu E-sir kama njia moja ya kutambua mchango wake katika tasnia ya muziki nchini. Kulingana na Alai pendekezo la Nameless limepitwa na wakati na ingekuwa vyema kituo cha kukuza vipaji vya wasanii ingebuniwa na kisha kupewa jina la msanii huyo aliyeachana alama kwenye muziki wa kizazi kipya. Utakumbuka Gavana Nairobi Johnstone Sakaja tayari aliunga mkono pendekezo hilo ila akataka taratibu za kisheria kufuata kabla ya ombi hilo kufanikishwa. Nameless anaendeleza harakati za kurai wakenya kutia saini mswaada wa kushinikiza barabara moja jijini Nairobi maeneo ya South C kupewa jina la msanii E-Sir kabla hajaidhinishwa.

Read More
 WAHU NA NAMELESS WASHEREKEA MIAKA 17 YA NDOA

WAHU NA NAMELESS WASHEREKEA MIAKA 17 YA NDOA

Wanamuziki David Mathenge maarufu kama Nameless na Wahu Kagwi wametimiza miaka 17 ya ndoa na miaka 25 tangu wayaanze mahusiano yao. Wawili hao ambao walianza mahusiano yao mwaka 1997 walifanikiwa kufunga ndoa mwaka 2005 na katika ndoa yao wamebahatika kupata watoto wawili, wote wakiwa wakike. Leo, Septemba 10 ni anniversary yao, ambapo wametimiza miaka 12 wakiwa mke na mume. Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nameless ambaye ndiye mume wa Wahu ameandika haya.. “Happy Anniversary Babe! 17 years today since we said ” I DO!” and 25 years since our first date! And you still the ONE ! Just alittle heavier !! Thank you for taking this journey of life with me! ” Ndoa ya wanamuziki hao imedumu muda mrefu kinyume na matarajio ya wengi kutokana na jinsi watu maarufu wamekuwa wakiacha ndoa zao ulimwenguni kote. Utakumbuka kwa sasa Nameless na Wahu wanatarajia kupata mtoto wao wa tatu hivi karibuni.

Read More
 PENZI LA JULIANA KANYAMOZI LAMKOSESHA USINGIZI NAMELESS

PENZI LA JULIANA KANYAMOZI LAMKOSESHA USINGIZI NAMELESS

Msanii mkongwe nchini Nameless ameshindwa kuficha mapenzi yake kwa msanii wa kike nchini Uganda Juliana Kanyamozi. Katika mahojiano yake hivi karibuni Nameless amesema asingekuwa ameoa  angemchumbia mwanamuziki huyo kwa kuwa ni mrembo, ana kipaji cha kipekee lakini pia ni mchapa kazi. Hitmaker huyo wa ngoma “Deep” ameenda mbali zaidi na kusema kwamba wamekuwa marafiki kwa kipindi kirefu kwenye shughuli zao za kimuziki. Hata hivyo watumiaji kwenye mitandao ya kijamii wameonekana kushangaza na kauli ya rapa huyo wengi wakihoji huenda  Nameless ana kazi ya pamoja na Juliana Kanyamozi hivyo anatengeneza mazingira ya kuzungumuziwa kabla ya ujio wa ngoma yao mpya. Nameless amesema hayo alipokuwa nchini uganda ambako alikuwa ameenda kwa ajili ya kutumbuiza kwenye onesho la Comedy Store. Utakumbuka Nameless alifunga ndoa na msanii mwenzake Wahu mwaka wa 2005 na wabarikiwa na watoto wawili ambao ni Tumiso na Nyakio. Ndoa ya wanamuziki hao imedumu muda mrefu kinyume na matarajio ya wengi kutokana na jinsi watu maarufu wamekuwa wakiacha ndoa zao ulimwenguni kote.

Read More
 NAMELESS NA WAHU WANATARAJIA MTOTO WA TATU

NAMELESS NA WAHU WANATARAJIA MTOTO WA TATU

Wanamuziki David Mathenge maarufu kama Nameless na Wahu Kagwi wametangaza kwamba wanatarajia mtoto wao wa tatu. Wawili hao walitoa tangazo hilo kupitia video ambayo waliichapisha kwenye mitandao ya kijamii. Tumiso ndiye kifungua mimba wa wanamuziki hao ambao walifunga ndoa mwaka 2005 na wa pili ni Nyakio. Ndoa ya wanamuziki hao imedumu muda mrefu kinyume na matarajio ya wengi kutokana na jinsi watu maarufu wamekuwa wakiacha ndoa zao ulimwenguni kote. Utakumbuka kwa sasa Wahu na Nameless wanafanya vizuri na wimbo wao mpya uitwao Deep, wimbo ambao ni wa sita kutoka kwenye album yao ijayo iitwayo MZ. Tayari wameachia nyimbo kama This Love Ya Wahu, This Love Ya Nameless, Te Amo, Feeling na Back it Up.

Read More
 NAMELESS AWAONYA VIJANA DHIDI YAKUTUMIWA NA WANASIASA TAIFA LINAPOJIANDAA KWA UCHAGUZI MKUU

NAMELESS AWAONYA VIJANA DHIDI YAKUTUMIWA NA WANASIASA TAIFA LINAPOJIANDAA KWA UCHAGUZI MKUU

Lejendari wa muziki nchini Nameless amewaonya vijana dhidi ya kutumiwa na baadhi ya wanasiasa ili kuwakuza kisiasa. Katika mahojiano na Mpasho Nameless amesema ahadi zinazotolewa na baadhi ya mirengo ya kisiasa ni njama ya kuwahadaa vijana ili kuwaunga mkono katika uchaguzi mkuu wa Agosti 9 mwaka huu. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Back It Up” amewataka vijana kujiepusha na siasa za chuki na ukabila na badala yake kuwa mstari wa mbele kuhubiri amani kote nchini. Nameless amesema hayo kwenye uzinduzi wa mpango wake wa Pride ya Kenya ambao unalenga kuwahimiza vijana kutokubali mawazo hasi kuathiri ndoto zao katika maisha kupitia sanaa.

Read More