Wyre, Nameless na Jua Cali kutengeneza bendi ya muziki
Msanii mkongwe nchini, Wyre amedokeza mpango wa kuunda bendi ya muziki itakayojumuisha wasanii wa kizazi kipya pamoja na wa zamani. Kupitia ukurasa wake wa Twitter, amepost video akitoa tangazo hilo ambapo amesema wameungana na kutengeneza timu ya malejendari wa muziki. “Kuna nini jamani. Kwa kawaida sifanyi hivi. Imekuwa zaidi ya miaka 20 katika kufanya jambo hili la muziki na nadhani ni kuhusu wakati huu ambao umefika…. Unajua kila kitu kinafikia hatua hiyo ya kufika mwisho. “Kwa hivyo nimeamua.. Tumeamua kuwa tunaunda bendi ya wasanii wa kitambo,” Msanii huyo aliweka wazi hilo huku akihamishia kamera kwa wasanii wengine ambao ni Nameless na Jua Calie pamoja na Kenzo.
Read More