NBA YoungBoy Kuachia Albamu Mpya Siku ya Uhuru Marekani

NBA YoungBoy Kuachia Albamu Mpya Siku ya Uhuru Marekani

Rapa maarufu wa Marekani, NBA YoungBoy, ametangaza kupitia Insta Story yake kuwa ataachia albamu mpya tarehe 4 Julai 2025, siku ya Uhuru wa Marekani. Tarehe hiyo ina uzito mkubwa kihistoria, na tangazo hilo limeibua hisia tofauti kwa mashabiki wake. Wengi wamelitafsiri tangazo hilo kama njia ya kuadhimisha uhuru wake binafsi, baada ya kuachiwa kutoka gerezani Machi 2025, alikokuwa akitumikia kifungo cha mwaka mmoja kwa kosa la kumiliki silaha bila kibali. Ingawa hajafichua jina la albamu, mashabiki wanatarajia kazi hiyo itagusia maisha, mapambano, na matumaini yanayoendana na safari yake ya maisha. Kwa sasa, mashabiki wake wanasubiri kwa hamu ujio wa albamu hiyo, wakiamini itathibitisha uwezo wake wa kurudi kwa nguvu kwenye muziki baada ya changamoto nyingi.

Read More
 NBA YoungBoy Afutiwa Makosa na Trump, Asema: ‘Ni Mwanzo Mpya wa Maisha’

NBA YoungBoy Afutiwa Makosa na Trump, Asema: ‘Ni Mwanzo Mpya wa Maisha’

Rapa maarufu wa Marekani NBA YoungBoy amemshukuru Rais wa Marekani, Donald Trump, kwa kumpa msamaha wa kisheria unaofuta rekodi za makosa ya jinai na kumpa nafasi mpya ya kisheria na kijamii. Kupitia ujumbe wa hadharani alioutoa hivi karibuni, YoungBoy, alieleza shukrani zake kwa hatua hiyo ya Trump, akisema kwamba imekuwa mwanga mpya katika maisha yake na itamuwezesha kuendelea mbele bila mzigo wa kihistoria wa makosa ya zamani. “Nashukuru kwa msamaha huu. Ni mwanzo mpya, na nitautumia vizuri,” alisema YoungBoy. Msamaha huu kwa YoungBoy umetafsiriwa na mashabiki kama njia ya kuufungua ukurasa mpya katika maisha yake. Rapa huyo ambaye amepitia changamoto mbalimbali za kisheria, sasa ana nafasi ya kuimarisha maisha yake binafsi na kazi yake ya muziki bila kuandamwa na rekodi ya makosa ya awali. Hata hivyo, hatua hiyo pia imezua mjadala. Wengine wanasema msamaha kwa watu maarufu huonyesha upendeleo, huku wengine wakisisitiza kwamba kila mtu anastahili nafasi ya pili, hasa pale wanapoonyesha mabadiliko ya kweli. Kwa sasa, mashabiki wa YoungBoy wanasubiri kuona ikiwa msamaha huu utakuwa mwanzo wa awamu mpya ya muziki safi, maisha bila migogoro ya kisheria, na ushawishi chanya kwa vijana.

Read More
 BINTI WA FLYOD MAYWEATHER AKIRI KOSA LA  KUMCHOMA KISU MZAZI MWENZA WA NBA YOUNGBOY

BINTI WA FLYOD MAYWEATHER AKIRI KOSA LA KUMCHOMA KISU MZAZI MWENZA WA NBA YOUNGBOY

Binti wa Floyd Mayweather,Yaya Mayweather amekiri kuwa na hatia ya kutenda kosa la kumchoma Kisu mzazi mwenza wa Rapa NBA YoungBoy, tukio lililotokea Aprili mwaka 2020. Yaya ambaye bado anadaiwa kuwa kwenye mahusiano na NBA YoungBoy, amekiri kosa hilo mbele ya waendesha mashtaka wa mahakama ya kitongoji cha Harris mjini Houston. Kosa hilo linabeba hukumu ya kifungo cha hadi miaka 20 Jela. Waendesha mashtaka wamependekeza kwamba ahukumiwe kifungo cha nje miaka 6 ambacho hutolewa kwa wakosaji wa mara ya kwanza na pia kufanya shughuli za kijamii chini ya uangalizi.

Read More
 BIFU LA RAPA LIL DURK NA NBA YOUNGBOY LACHUKUA SURA MPYA

BIFU LA RAPA LIL DURK NA NBA YOUNGBOY LACHUKUA SURA MPYA

Rapa kutoka nchini Marekani Lil Durk amevunja kimya chake kuhusu kinachoendelea mtandaoni kati yake na NBA Youngboy. Lil Durk kupitia ukurasa wake wa instagram amepost picha akiwa amelalia pesa nyingi na kuandika ujumbe “mpuuzi” uliotafsiriwa kuwa ni jibu kwa NBA Youngboy Lil Durk ametoa kauli hiyo baada ya rapa NBA Youngboy kum-diss pamoja na label ya O’block kwenye ngoma yake mpya Bring The Hook & Know Like I Know ambapo amewatolea kauli chafu lakini pia kumtishia lil durk kwamba atakufa “young n**ga gone die…stay safe” Lakini pia kupitia ngoma hiyo amem-diss rapa nlechoppa kwa kuingilia bifu kati yake na watu wa (o’block) label inayomilikiwa na lildurk, akidai kwamba anaingilia bifu lisilomhusu NBA Youngboy kupitia ngoma hiyo amesikika kwenye mstari akisema (you could say i was you favourite n**ga better stay up in your place b****h) yaani ulisema kwamba ulikuwa unanikubali lakini ni bora ukabaki katika nafasi yako mpuuzi wewe. Utakumbuka NBA Young aliachia disstrack hiyo kufuatia NLE Choppa kumtwanga ngumi shabiki yake baada ya kuingia kwenye ugomvi  wakiwa uwanja wa ndege. Sababu ya ugomvi huo inasemekana kuwa ni baada ya NLE Choppa kufanya moja ya interview hivi karibuni na kusema kwamba hapo awali NBA Young boy alikuwa moja kati ya wasanii wake anaowakubali zaidi lakini kutokana na ngoma yake mpya “Bring the Hook” aliyowa-diss  genge la O’block na marehemu King Von ameamua kumkataa

Read More
 RAPPER NLE CHOPPA AZICHAPA NA SHABIKI WA NBA YOUNGBOY BAADA KURUSHIANA MANENO MAKALI WAKIWA AIRPORT

RAPPER NLE CHOPPA AZICHAPA NA SHABIKI WA NBA YOUNGBOY BAADA KURUSHIANA MANENO MAKALI WAKIWA AIRPORT

Rapa NLE Choppa kutoka nchini Marekani wamerushiana makonde na shabiki wa rapa NBA YoungBoy baada ya kuingia kwenye ugomvi  wakiwa uwanja wa ndege. Inasemekana kuwa ngumi ya kichwa na ya shingo vilitosha kumuangusha chini shabiki huyo ambaye alibamiza kichwa chini baada ya kuanguka na kulala hapo hapo. Sababu ya ugomvi huo inasemekana kuwa ni baada ya NLE Choppa kufanya moja ya interview hivi karibuni na kusema kwamba hapo awali nba young boy alikuwa moja kati ya wasanii wake anaowakubali zaidi lakini kutokana na ngoma yake mpya “Bring the Hook” aliyowa-diss  genge la kihalifu la O’block na marehemu King Von ameamua kumkataa

Read More