RASMI: NICCAH THE QUEEN ATHIBITISHA KUACHANA NA DJ SLAHVER

RASMI: NICCAH THE QUEEN ATHIBITISHA KUACHANA NA DJ SLAHVER

Msanii wa nyimbo za injili nchini Niccah The Queen ameweka wazi kuwa yeye na mchumba wake DJ Slahver wameachana. Niccah amebainisha hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo amesema amechukua maamuzi ya kuachana na mpenzi wake huyo baada ya kuafikia makubaliano ya pamoja huku akimtakia kila la kheri kwenye maisha yake mpya. Hata hivyo Niccah The Queen hajatoa maelezo zaidi kuhusu kiini cha uhusiano wake na DJ Slahver kuvunjika  ila walimwengu kwenye mitandao ya kijamii wamehoji kuwa huenda msanii huyo anatengeza  mazingira ya kumzungumziwa nchini Kenya kabla ya ujio wa ngoma yake mpya Ikumbukwe kuwa penzi la Niccah The Queen na DJ Slahver lilianza rasmi mwishoni mwa mwaka jana miezi kadhaa baada ya kuachana na aliyekua mpenzi wake Dkt. Ofweneke.

Read More
 NICAH THE QUEEN AWAPA SOMO WANAWAKE KUHUSU UTARATIBU WA ULEZI WA PAMOJA KWA WATOTO (CO-PARENTING)

NICAH THE QUEEN AWAPA SOMO WANAWAKE KUHUSU UTARATIBU WA ULEZI WA PAMOJA KWA WATOTO (CO-PARENTING)

Female singer kutoka Kenya Nicah The Queen ametoa changamoto kwa wanawake wenzake kujishusha na kushirikiana na wapenzi wao wa zamani kuwalea watoto wao waliozaa nje ya ndoa badala ya kuendekeza kiburi na majivuno. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Nicah The Queen amesema kiburi na majivuno imewaponza wanawake wengi na kuwafanya kuona utaratibu ulezi wa pamoja yaani, Co-parenting kuwa mgumu kwao jambo ambalo anadai limepelekea watoto wengi kukosa upendo wa baba katika maisha. Hitmaker huyo wa ngoma ya “Na Wewe” amesema kila mtoto ana haki ya kupata upendo na mahitaji ya msingi kutoka kwa mama na baba mzazi licha ya utofauti wao. Kauli ya Nicah The Queen imekuja mara baada ya kukutana baby daddy wake Dr. Ofweneke kwenye hafla ya kufuzu kwa mtoto wao ambapo walimuonyesha upendo licha ya kutengana na kuingia kwenye mahusiano mengine tofauti.

Read More