Nicholas Kioko Apinga Madai ya Kuachana na Wambo Ashley
Mtangazaji na content creator Nicholas Kioko amejitokeza wazi kukana tetesi za kuvunjika kwa mahusiano yake na mpenzi wake Wambo Ashley. Kupitia InstaStories, Kioko alifafanua kuwa mapenzi yao bado ni imara na hayatikisiki, akiongeza kwa utani kuwa hakuna uchawi au presha ya mitandaoni itakayomfanya amuache Wambo. Alisisitiza kuwa wao ni moja ya wapenzi wanaoendana zaidi na kwamba wanaotumai kuona wakiachana “watangoja sana.” Uvumi huu ulianza baada ya shabiki mmoja kudai kuwa Kioko na Wambo wangekuwa wanandoa wa pili kuachana, kufuatia misukosuko ya mahusiano iliyoikumba wanandoa wa karibu nao akiwemo Commentator 254 na Moureen pamoja na Vinny Flava na Ng’ang’a. Hata hivyo, Kioko ameweka wazi kuwa yeye na Wambo hawaguswi na tetesi hizo na mapenzi yao yanaendelea kuimarika.
Read More